Raha ya wageni kutoka Dalisalamu

Raha ya wageni kutoka Dalisalamu

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,752
Reaction score
830,870
Kuna ukarimu fulani wa kiafrika... Mgeni anapewa heshima kubwa sana.. Kwa baadhi ya makabila mgeni kama ni mwanaume hupewa na mlimbwende kabisa amtoe baridi... Ila sijui kuhusu wageni wa like wanapewa nini🤣
Kuna mwaka Rais Bush wa Marekani alipokuja Tanganyika Dalisalamu barabara zote alizopangiwa kupita zilidekiwa

Kule vijijini wageni wa dalisalamu.. Maarufu Kama wageni wa dar wana nafasi yao maalum kwenye shughuli yoyote iwe
Msiba
Harusi
Send off
Matanga
Kusanyiko la ndugu nknk
Wenyeji kama sehemu za kulala hazitoshi watawapisha wageni wa Dar..!
Leo kuna kituko nimekishuhudia mahali wenyeji wa dar wakiwapisha wageni wa dar kwenye nyumba yao..
Nikaona hapa sio bure kuna namna maana si kwa ukarimu huo
Watu wa dar wana nyodo sana mpaka akupishe kwakwe ni lazima uwe mnonošŸ˜‚
Sasa sijui ndio moja kwa moja ama ndio mgeni karibu .. Mgeni siku ya kwanza?
 
Nimekumbuka hili shairi

Mgenisikuyakwanza, mpemchele na panza,
mtilie kifuani, mkaribishe mgeni,

Mgenisikuyapili, mpe maziwa na samli, mahaba
yakizidia, mzidie mgeni,

Mgeni siku ya tatu, jumbani hamuna kitu, mna
Kibaba tatu, pika ule na mgeni,

Mgeni siku ya nne, mpe jembe akalime, akirudi
muagane ,aende kwao mgeni,

Mgeni siku ya tano, mwembamba kama
sindano, hauishi musengenyano, asengenyao mgeni,

Mgeni siku ya sita, mkila mkajificha, mwingine
vipembeni, afichwae yeye mgeni,

Mgeni sikuya saba, simgeni ana baa, hata moto
mapaani, hutia yeye mgeni,

Mgeni siku ya nane ,njoo ndani tuonane,
atakapotokea nje, tuagane mgeni,

Mgeni siku ya kenda ,enenda mwana
kwenenda, usirudi nyuma, usirudi mgeni,

mgeni siku ya kumi, kwa mateke na mangumi,
hapana afukuzwaye ,ni yeye mgeni.šŸ˜€šŸ˜€šŸ˜€šŸ˜€
Tulitunze vema hili shairi
 
DAR: Kufuatia makubaliano yanayoendelea kati ya #CHAUMMA na makada waliotoka #CHADEMA, Hashim Rungwe anaendelea kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Makamu wake (Bara) anakuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Kati, Devotha Minja

Aidha, nafasi ya Katibu Mkuu amepewa Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu Bara amepewa Benson Kigaila, upande wa Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu amekuwa Mohamed Masoud

Mgawanyo huo umekuja baada ya waliokuwa Viongozi wa #CHAUMMA kujiuzulu nafasi zao leo Mei 19, 2025 akiwemo aliyekuwa Katibu Mkuu, Mohammed Masoud Rashid, Naibu Katibu Mkuu Bara, Rahman Rungwe na Makamu Mwenyekiti Bara, Kayungo Mohammed
20250519_200107.jpg
 
Wana imani na nini!?šŸ˜‚
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Ubwabwa wa Spunda - chauma hoyee
 
Umenikumbusha kisa kimoja.
Mpare mmoja alikuja kumtembelea mdogo wake hapa Dar.
Mdogo mtu akachinja kuku kwa ajili ya kaka yake kutoka Mamba Miamba.
Ilipofika muda wa msosi mke wa mwenyeji alitenga chakula. Kawaida kule upareni kukiwa na mgeni mama anakulia jikoni na mabinti zake huku sitting room anakua baba , mgeni na vijana wa kiume.
Mgeni alipoona mila na desturi imezingatiwa akajua na ile mila ya kumuachia mkubwa aanze kuokota nyama itazingatiwa hakujua kuwa wapare waliozakiwa Dar hata hicho kipare hawakijui. mgeni wakati anaanza na tonge la ugali watoto wa mdogo wake walianza na vipaja na nyama kubwa na nzuri. Kufumba na kufumbua kwenye sahani ya nyama ilibaki shingo na air tanzania moja.
Furaha mgeni ilitoweka ghafla.
(Air tanzania ni kipapatiko kwa wanyakyusa au mkono wa kuku)
 
Nimekumbuka hili shairi

Mgenisikuyakwanza, mpemchele na panza,
mtilie kifuani, mkaribishe mgeni,

Mgenisikuyapili, mpe maziwa na samli, mahaba
yakizidia, mzidie mgeni,

Mgeni siku ya tatu, jumbani hamuna kitu, mna
Kibaba tatu, pika ule na mgeni,

Mgeni siku ya nne, mpe jembe akalime, akirudi
muagane ,aende kwao mgeni,

Mgeni siku ya tano, mwembamba kama
sindano, hauishi musengenyano, asengenyao mgeni,

Mgeni siku ya sita, mkila mkajificha, mwingine
vipembeni, afichwae yeye mgeni,

Mgeni sikuya saba, simgeni ana baa, hata moto
mapaani, hutia yeye mgeni,

Mgeni siku ya nane ,njoo ndani tuonane,
atakapotokea nje, tuagane mgeni,

Mgeni siku ya kenda ,enenda mwana
kwenenda, usirudi nyuma, usirudi mgeni,

mgeni siku ya kumi, kwa mateke na mangumi,
hapana afukuzwaye ,ni yeye mgeni.šŸ˜€šŸ˜€šŸ˜€šŸ˜€
Tulitunze vema hili shairi
Hata sikumbuki vizuri sijui lilikuwa la darasa la 4 B?
 
Leo kuna kituko nimekishuhudia mahali wenyeji wa dar wakiwapisha wageni wa dar kwenye nyumba yao..
Nikaona hapa sio bure kuna namna maana si kwa ukarimu huo
Muda si mrefu wakaanza kulia maana mgeni mwenyewe aliyepishwa amekuja ananinginiza kengele zake tu hana watu kama alivyoahidi!
 
Wanakohamia wageni wamekuta wenyeji nao wanahama.

#MkulimaWaSiasa
FB_IMG_1748602789176.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom