Rafiki yangu kaiba mpenzi wangu

Rafiki yangu kaiba mpenzi wangu

Pigo ulilotakiwa kilifanya ulitakiwa kuchukua chombo chengine kikali zaidi yake..
 
Japo ni chai ila hakuna kitu kinaitwa kuiba mpenzi, mtu mzima anaibwaje kwa mfano...mpenzi wako akichukuliwa na mtu mwingine ni yeye ndio kaamua kukuacha
 
Japo ni chai ila hakuna kitu kinaitwa kuiba mpenzi, mtu mzima anaibwaje kwa mfano...mpenzi wako akichukuliwa na mtu mwingine ni yeye ndio kaamua kukuacha
Sawa ila pombe ndo chanzo
 
Umekosea kupigana sababu ya mwanamke aliyekwambia hakutaki, wanaume hatupiganii wanawake..ungeachana nae ukaendelea na maisha yako
 
Umekosea kupigana sababu ya mwanamke aliyekwambia hakutaki, wanaume hatupiganii wanawake..ungeachana nae ukaendelea na maisha yako
Mkuu nimekuelewa mi mwenyewe huwa sitakagi kupigania Dem but nilijikuta nimepgana tu
 
Kwanza nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kuniponya na hili janga weekend iliyopita. Mimi Kama kijana nipende kuwashauri vijana wenzangu kuwa waache pombe japo ni ngumu sana.

Weekend nilikuwa viwanja fulani nikipata K-Vant na kitimoto kwa vile huwa kuna nyingine naacha ndani basi nilikunywa kidogo tu. Halafu nikasepa geto kupiga mdogo mdogo.

Sasa kipindi nafika geto nikashangaa masela niliyopanga nao wanaanza kucheka sana. Nikauliza shida nini? Moja akajibu kwa kejeli sana kuwa unaenda kulewa wakati demu wako analiwa na mshikaji wa hapa hapa. Bila kuhoji nikachukua siraha nikaenda kusimama kwa mlango wa mshikaji. Aisee nikajaribu kufungua but alikuwa kafunga.

Nikampigia Dem sim nikamuulza upo wapi saiv? "Akanijibu kwani wewe inakuhusu nini" duh! Niliumia sana but ningefanyeje? Nikamwandikia sms ya kumtusi akanirudishia inasema "unalazimisha mapenzi na Mimi sikupendi" Niliumia.

Basi nikapiga fujo pale mpaka watu wakajaa make mtaa wetu Ni Kama uswahilini vile. Wakanishauri mpaka nikatupa zile siraha nilizokuwa nimeshikilia. Ilikuwa kisu, rungu na panga. Aisee baada ya kuzitupa msikaji katoka anajiropokesha na Mimi nilikuwa tungu sana. Nilimuotea ngumi ya shavu mpaka nikaona anatema memo. Akanikaba mpaka chini make nilikuwa nimekunywa pombe nyingi sana. Nikaona anaweza kunioshea sana nikabahatisha nyama ya kung'ata bana aise nimemng'ata mpaka nikatoa nyama.

Vita ilikuwa Kali sana ila sikuumia hata kidogo lkn mpinzani wangu nimemjeruhi sana sana nilipoona atanizidi nguvu nikatumia meno. Kuna kidole chake nikila chite. Na sehemu ya zingine mpaka kaenda kuoshwa hospital. Hapa najua muda wowote naweza kuitwa KITUO CHA POLICE
Tahadhari: Usije kujidhuru au kudhuru mtu mwingine kwa kipande cha nyama ambacho hata ukipewa miaka mia ya kukila, huwezi kukimaliza.
 
Pombe ikikutoka uje tena hapa utueleze ulichokuwa unapigania na mwanaume mwenzako ni nini. Halafu inaonekana bado umelewa hebu sogea hapo jirani unywe hata bakuli la supu ya utumbo akili ikukae sawa
 
Kwani alimbaka? Si aliomba na kapewa? Binti hana heshima kufanya hivyo na rafiki yako . Nadhani wewe ndiyo mwenye tatizo . Unashindwa kumtosheleza binti kwa hiyo ilibidi kuomba msaada .
 
Kwani alimbaka? Si aliomba na kapewa? Binti hana heshima kufanya hivyo na rafiki yako . Nadhani wewe ndiyo mwenye tatizo . Unashindwa kumtosheleza binti kwa hiyo ilibidi kuomba msaada .
Msaada wa nini?
 
Pombe ikikutoka uje tena hapa utueleze ulichokuwa unapigania na mwanaume mwenzako ni nini. Halafu inaonekana bado umelewa hebu sogea hapo jirani unywe hata bakuli la supu ya utumbo akili ikukae sawa
Nimeisharudi kaka mkubwa
 
Wavulana mnakwama wapi girl friend anagombewa
Acha upuuzi maisha yako ni Bora Sana kuliko huo upuuzi
 
Back
Top Bottom