Hivi wewe unaakili kweli?
Hivi unaweza muonyesha MTU kitu kinachoonekana?
Yaani upo baharini alafu unataka uonyeshwe bahari?
Ndio maana mnaambiwa ninyi ni matapeli, na wadhulumaji.
Mwenye upendo hafundishwi kupenda, na mwenye kupenda haonyeshwi Upendo.
Bado utatoa macho😂😂
Kwa sababu mmezoea kutapeliana,
Uonyeshwe upendo kwani wewe ni kipofu?
Mapenzi hayajifichi mpaka yafichuliwe. MTU kama hakupendi hakupendi unataka mpaka akuonyshe 😂😂
Upendo wa maonyesho ndio Utapeli wenyewe huo tunaouzungumzia hapa.
Ndio ninyi mkianza mahusiano mnakuwa na Kasi Kwa sababu mnaonyeshana ATI UPENDO 😂😂yaani uhuni uhuni tuu! Baada ya miaka mitatu mayowe! Ooh! Umebadilika, sijui siku hizi haunipenda, hivi tangu lini upendo ukabadilika au ukachuja?
Bado unamengi ya kujifunza, ukijifanya mbishi endelea na ubishi wako.
Maana wengine kunielewa inawachukua miaka na miaka