Profesa Tibaijuka, Apson Mwang'onda na Mradi wa Kuuza Kigamboni kwa Marekani

Mama Amon

JF-Expert Member
Mar 30, 2018
2,021
2,478
1687781609511.png

Hayati Apson Mwang'onda akisalimiana na Mwamba

Kuna wakati Profesa Tibaijuka, Waziri wa Ardhi wakati huo, alikuwa anaratibu mradi kabambe wa Kigamboni.

Wamarekani ndio walitaka kuujenga kwa mfumo wanaoutaka wao ili wautumie kwa namna wanavyotaka wao.

Ndani ya kivideo cha awali kwa ajili ya kuunadi mradi huo kulikuwa na sentensi kwamba kuna eneo litakuwa "a university for whites only."

Baada ya kelele za wananchi, "eagle eyed guys" walifuta hiyo sentensi.

Lakini pia Wamarekani walitaka kuitumia Kigamboni kama kituo chao cha ukachero wa kijeshi duniani.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, wa wakati huo, Hayati Apson Mwang'onda aliuchinjia baharini mradi huu.

Profesa Tibaijuka alikubaliana na hoja za Apson.

Na sasa kwa sababu ya uzoefu huo, Prof anatwambia kwamba huu Mkataba wa Dubai na Tanzania ni "zimwi" kama lile "dude" la Kigamboni. Anashauri tuachane na mkataba wa Dubai.

Tunaomba busara za Apson zimtembelee DG wa TISS wa sasa tunapojadili mkataba wa awali wa DP World.

 
kwani inahusiana vipi na bandari yetu,

PROFESA ANNA TIBAIJUKA ASEMAVYO KUHUSU MKATABA WA DP WORLD.

(Mahojiano ya Tarehe 19/06/2023)

Sisi tunaojua tuna mzigo mzito kuliko wasiojua, wajukuu zetu watakuja kusema na nyinyi mlikuwepo, hata mbele za Mungu tutakosa cha kuwajibu.

Nimekuja na mkataba huu hapa, ukiuangalia unajiuliza huu mkataba ulipataje sahihi za Serikali!? Hili zimwi liliingiaje Ikulu na likapita hadi bungeni!?

Mimi ni mstaafu ila sijastaafu kwenye Jamii kulitumikia taifa langu, nikiona jambo linahitaji ufafanuzi natoka kulielezea, kwenye Jamii tunastaafishwa na Mungu.

Kwa uzee wangu, kwa uzoefu wa kufanya kazi kimataifa, Mimi si shabiki, nawajibika kutoa ufafanuzi kwenye mambo mazito yanayohitaji ufafanuzi.

Watangazaji wa Wasafi; Mama hii ni kama Fei Toto alivyotoka Yanga akaenda Azam,alii..

Profesa Tibaijuka; Ninyi vijana acheni kuingiza mambo ya mpira kwenye mambo mazito yanayohusu nchi, watoto na wajukuu na vitukuu vyetu kama jambo hili..!

Mkataba unahusu "territory" yaani mkataba utaanzia kwenye mipaka ya Tanzania Nungwi, Pemba na unguja, mkataba utakuwa juu ya territory ya Tanzania anga, bahari na nchi kavu, mkataba unasema Tanzania itaijulisha Dubai juu ya fursa zozote zilizopo, na zitakazokuwepo, hili ni tusi kubwa sana.

Vijana hapa nazungumzia kupokonywa Sovereignty, yaani haki ya nchi kutoingiliwa katika mambo yake, tumejikabidhi na tutakabidhi kila fursa zetu, kwa sasa inaweza kuonekana ni sawa lakini fursa zitakapokosekana watakapobaki wajukuu wetu, ndipo athari zitaonekana, ni sawa tumetega bomu litalipuka siku za usoni.

Watangazaji Wasafi; Profesa muda ni mdogo kuchambua vifungu vya kwenye mkataba, umetueleza kwa uchache tutakutafuta tena.

Profesa Tibaijuka; Uwingi wa maneno si bora kuliko uzito wake.
 
PROFESA ANNA TIBAIJUKA ASEMAVYO KUHUSU MKATABA WA DP WORLD.

(Mahojiano ya Tarehe 19/06/2023)

Sisi tunaojua tuna mzigo mzito kuliko wasiojua, wajukuu zetu watakuja kusema na nyinyi mlikuwepo, hata mbele za Mungu tutakosa cha kuwajibu.

Nimekuja na mkataba huu hapa, ukiuangalia unajiuliza huu mkataba ulipataje sahihi za Serikali!? Hili zimwi liliingiaje Ikulu na likapita hadi bungeni!?

Mimi ni mstaafu ila sijastaafu kwenye Jamii kulitumikia taifa langu, nikiona jambo linahitaji ufafanuzi natoka kulielezea, kwenye Jamii tunastaafishwa na Mungu.

Kwa uzee wangu, kwa uzoefu wa kufanya kazi kimataifa, Mimi si shabiki, nawajibika kutoa ufafanuzi kwenye mambo mazito yanayohitaji ufafanuzi.

Watangazaji wa Wasafi; Mama hii ni kama Fei Toto alivyotoka Yanga akaenda Azam,alii..

Profesa Tibaijuka; Ninyi vijana acheni kuingiza mambo ya mpira kwenye mambo mazito yanayohusu nchi, watoto na wajukuu na vitukuu vyetu kama jambo hili..!

Mkataba unahusu "territory" yaani mkataba utaanzia kwenye mipaka ya Tanzania Nungwi, Pemba na unguja, mkataba utakuwa juu ya territory ya Tanzania anga, bahari na nchi kavu, mkataba unasema Tanzania itaijulisha Dubai juu ya fursa zozote zilizopo, na zitakazokuwepo, hili ni tusi kubwa sana.

Vijana hapa nazungumzia kupokonywa Sovereignty, yaani haki ya nchi kutoingiliwa katika mambo yake, tumejikabidhi na tutakabidhi kila fursa zetu, kwa sasa inaweza kuonekana ni sawa lakini fursa zitakapokosekana watakapobaki wajukuu wetu, ndipo athari zitaonekana, ni sawa tumetega bomu litalipuka siku za usoni.

Watangazaji Wasafi; Profesa muda ni mdogo kuchambua vifungu vya kwenye mkataba, umetueleza kwa uchache tutakutafuta tena.

Profesa Tibaijuka; Uwingi wa maneno si bora kuliko uzito wake.
nisaidie nexus yake na bandari za Tanganyika
 
View attachment 2669384
Hayati Apson Mwang'onda akisalimiana na Mwamba

Kuna wakati Profesa Tibaijuka, Waziri wa Ardhi wakati huo, alikuwa anaratibu mradi kabambe wa Kigamboni.

Wamarekani ndio walitaka kuujenga kwa mfumo wanaoutaka wao ili wautumie kwa namna wanavyotaka wao.

Ndani ya kivideo cha kuunadi mradi huo kulikuwa na sentensi kwamba kuna eneo litakuwa "a university for whites only."

Lakini pia Wamarekani walitaka kuitumia Kigamboni kama kitui chao cha ukachero wa kijeshi duniani.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, wa wakati huo, Hayati Apson Mwang'onda aliuchinjia baharini mradi huu.

Profesa Tibaijuka alikubaliana na hoja za Apson. Mungu amlaze mahali pema peponi.

Tunaomba busara za Apson zimtembelee DG wa TISS wa sasa tunapojadili mkataba wa awali wa DP World.

Amina.
Mmebuma na mnalo.
Mama Tibaijuka kawavua nguo hadharani.
Chutama basi kuficha aibu.
 
View attachment 2669384
Hayati Apson Mwang'onda akisalimiana na Mwamba

Kuna wakati Profesa Tibaijuka, Waziri wa Ardhi wakati huo, alikuwa anaratibu mradi kabambe wa Kigamboni.

Wamarekani ndio walitaka kuujenga kwa mfumo wanaoutaka wao ili wautumie kwa namna wanavyotaka wao.

Ndani ya kivideo cha kuunadi mradi huo kulikuwa na sentensi kwamba kuna eneo litakuwa "a university for whites only."

Lakini pia Wamarekani walitaka kuitumia Kigamboni kama kitui chao cha ukachero wa kijeshi duniani.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, wa wakati huo, Hayati Apson Mwang'onda aliuchinjia baharini mradi huu.

Profesa Tibaijuka alikubaliana na hoja za Apson. Mungu amlaze mahali pema peponi.

Tunaomba busara za Apson zimtembelee DG wa TISS wa sasa tunapojadili mkataba wa awali wa DP World.

Amina.
Duh...!, asante sana kwa taarifa hii!, kiukweli kabisa kuna vitu wengi hatuvijui!.
Ubarikiwe sana Mama Amon
P
 
nisaidie nexus yake na bandari za Tanganyika
Mkataba unahusu "territory" yaani mkataba utaanzia kwenye mipaka ya Tanzania Nungwi, Pemba na unguja, mkataba utakuwa juu ya territory ya Tanzania anga, bahari na nchi kavu, mkataba unasema Tanzania itaijulisha Dubai juu ya fursa zozote zilizopo, na zitakazokuwepo, hili ni tusi kubwa sana.
 
View attachment 2669384
Hayati Apson Mwang'onda akisalimiana na Mwamba

Kuna wakati Profesa Tibaijuka, Waziri wa Ardhi wakati huo, alikuwa anaratibu mradi kabambe wa Kigamboni.

Wamarekani ndio walitaka kuujenga kwa mfumo wanaoutaka wao ili wautumie kwa namna wanavyotaka wao.

Ndani ya kivideo cha kuunadi mradi huo kulikuwa na sentensi kwamba kuna eneo litakuwa "a university for whites only."

Lakini pia Wamarekani walitaka kuitumia Kigamboni kama kitui chao cha ukachero wa kijeshi duniani.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, wa wakati huo, Hayati Apson Mwang'onda aliuchinjia baharini mradi huu.

Profesa Tibaijuka alikubaliana na hoja za Apson. Mungu amlaze mahali pema peponi.

Tunaomba busara za Apson zimtembelee DG wa TISS wa sasa tunapojadili mkataba wa awali wa DP World.

Amina.
Mkishaonaga mnabanwa, mnaanzaga chokochoko kama hizi
 
View attachment 2669384
Hayati Apson Mwang'onda akisalimiana na Mwamba

Kuna wakati Profesa Tibaijuka, Waziri wa Ardhi wakati huo, alikuwa anaratibu mradi kabambe wa Kigamboni.

Wamarekani ndio walitaka kuujenga kwa mfumo wanaoutaka wao ili wautumie kwa namna wanavyotaka wao.

Ndani ya kivideo cha kuunadi mradi huo kulikuwa na sentensi kwamba kuna eneo litakuwa "a university for whites only."

Lakini pia Wamarekani walitaka kuitumia Kigamboni kama kitui chao cha ukachero wa kijeshi duniani.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, wa wakati huo, Hayati Apson Mwang'onda aliuchinjia baharini mradi huu.

Profesa Tibaijuka alikubaliana na hoja za Apson. Mungu amlaze mahali pema peponi.

Tunaomba busara za Apson zimtembelee DG wa TISS wa sasa tunapojadili mkataba wa awali wa DP World.

Amina.
Mnahangaika sana. Hii suala ni la miaka zaidi ya mitano iliyopita. Ndio msukumo wa kujenga SGR ulipoanzia.

Hao DPW wameshasaini mikataba huko DRC na Rwanda, unataka kusema kuwa busara za kina Apson wa huko hazijafua dafu mpaka kufikia hao jamaa kukubalika huko?.

Mnajaribu sana kuja na kila mada yenye nia ya kupotosha lakini walio nyuma ya kazi yenu wanajulikana na siku zao zinahesabika.
 
Back
Top Bottom