Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,325
- Thread starter
- #341
Usitake kuchanganya mambo na kuleta hoja zako za udini. Nilisema huko juu kuwa hata kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ambayo imerekebishwa mnamo mwaka 2009, Zanzibar yenyewe imetangaza kuwa mipaka yake ni kama iliyokuwapo kabla ya Muungano. Kwa kutokujua hao wanaojifanya ni wasomi na wanaopigania masilahi ya Zanzibari wamekana haki yao ya Ukanda Tengefu wa Kiuchumi (UTK). Madhari huna haki huwezi ukawa na haki ya kupata Ukanda-Nyongeza wa Kibara (Extended Continental Shelf).
Hoja ya kuvimeza visiwa vya Zanzibar ni hoja isiyo na msingi, kwa muundo wa muungano wetu Tanzania Bara ndiyo imemezwa na Zanzibar kwani, Zanzibar inayo serikali yake na bunge na mahakama yake, wakati Tanzania Bara haina. Wabunge wa Zanzibar wanatoa maamuzi juu ya Tanzania Bara hata kwa mambo yasiyo ya Muungano.
Hoja ya udini inatolewa na watu wasio na hoja na wenye kujua kupayuka, kama wewe na Juha Jussa. Mtu mwenye akili zake zilizotimia(timamu) anajua kuwa njama hiyo haipo na wale wanaoifikiria wanapoteza muda wao. Uislamu na Ukiristu na Uyahudi, si dini ambazo unaweza kuzipatiliza duniani hata ukila njama na shetani. Kama ilishindikana kung'oa Uislamu Ulaya inawezakana kuung'oa Tanzania? Kama imeshindikana kuupatilliza hapa Marekani, na kwa kweli hapa Marekani miji kama ya Minneapolis-St-Paul (Miji Pacha), Dearborn(Michigan) Uislamu unazidi kushamiri sembuse Tanzania. Uchina na Urusi licha ya kufuata Ukomunisti zilishindwa kuipatiliza dini hiyo pamoja na Ukristu, sasa hilo Kanisa Katoliki litaweza hapa Tanzania?
Jibu ni kuwa vioja hivi vya chuki vinasambazwa na watu wenye lengo la kuleta utengano na kujipatia masilahi binafsi kama wewe na Juha Jussa.
Watanzania wenye mapenzi mema hatuwezi kunyamazia upuuzi kama huu na tutambana ha vioja hivi vichafu bila kurudi nyuma.
Kama Wazanzibari hawataki muungano ni vema isemwe hivyo ili kila upande wa muungano ufanye mambo yake kwa uhuru bila kulazimishwa kuzungumzia vioja badala ya hoja za msingi zinazoleta maendeleo.
Rugemeleza,
Nilipo Blue.
Kumbuka kuwa Katiba sio msahafu , kwani inaweza kufanyiwa marekebisho na kuingiza kipengele hicho au kingine chochote kile wakti wowote pindi wakikihitaji. Hivyo hoja yako naomba isihalalishe hata kidogo Tanganyika kuomba eneo la Znz au kuifanyia dhulma zozote kwa kutumia mwanya wa sharia za Znz.
Lakin hoja iliyopo mezani ni Uhalali wa Tibaijuka kama waziri wa Ardhi na makaazi , wizara ambayo si ya Muungano kuiwakilisha Znz katika UN.
Kumbuka kuwa Katiba ya Muunganio haimruhusu kabisa Tibaijuka kuwakilisha Znz kwa aina yoyote ile katika mambo ya kimataifa.
Mamlaka yake Tibaijuka ni kama angeomba UN kuongeza eneo la maji la ziwa victoria, Nyasa au tanganyika lakin sio bahari.
Sasa nakuomba na wewe kama muungwana usome vizuri katiba na kuona mamlaka ya wizara zote za JMT zisizokuwa za muungano kisha tuanze kujadili.