Prof. Maghembe amekalia kuti kavu

Prof. Maghembe amekalia kuti kavu

Katika siku zote leo ndio nimekuona kichwa! hongera sana mkuu

hata mimi nimeshangaa ile taarifa ya kuachiwa kwa mifugo bila masharti yoyote
Ulitaka hiyo mifugo iachiwe kwa masharti gani..?
 
Hatua ya proff maghembe inashangaza. Eneo hilo linafahamika kuvamiwa na wafugaji wanyarwanda wa jamii ya kitutsi. Wanatoa rushwa kwa vigogo na huwafanyia wenyeji vitendo vya kinyama ikiwa ni pamoja na kufanya mauaji ya wale wenye ujasiri kuwapinga. Uamuzi wa proff yafaa kuchunguzwa kama ni kwa manufaa ya nani.
Hizo chuki za kikabila peleka kwenu. Ng'ombe zilikuwa detained kwa kosa gani..?
 
Sijui nisemeje ila sijawahi kumkubali Prof Maghembe. Magumashi matupu
 
Rafik issue ya kagera huyo jamaa aliyetumbuliwa alikiuka agizo la serikali la kutoshika ngombe ambazo ziko kwenye hifadhi hadi pale watapata maeneo ya kulisha hiyo mifugo na hilo lilisemwa bungeni in June
 
Maghembe hachomoki....ni vyema viongozi wetu wakajua sasa hivi kila linalofanyika popote linanaswa na vyombo vya usalama na ikibidi linatua mezani kwa Rais haraka. Acheni kufanya kazi kwa mazoea ....JPM hatanii na ana full support ya vyombo vyote vya ulinzi na usalama. Dawa ni moja tu ....fata sheria hata uwe nani ....this is very serious ......wanaofikiri ni nguvu ya soda wataumia bure ....
 
--SIONI TATIZO LAKE/
TUACHE CHUKI BINAFSI...
Hebu chukulia Waziri kaagiza ng'ombe wasikamatwe had wafugaji watakapotengewa maeneo mbadala, halafu Mhifadhi akakaidi unadhan kuna kuheshimiana hapo..? Watu wanapenda kula nyama kila siku lakn hawatak kujua hao ng'ombe wanatoka wapi na wanakula nin. Shiiida..!
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Binafsi nilikuwa ni miongoni mwa watu ambao tulionesha wasiwasi wetu mara tu baada ya Prof Maghembe kuteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii. Wasiwasi wangu haukutokana na location ambayo Prof Maghembe anatoka bali ni kutokana na ugumu wa Wizara hiyo na uwezo wa Maghembe kukabiliana na changamoto za Wizara.

Hakika nilikuwa sahihi kumjudge negatively. Huko Kagera, Mhifadhi Mkuu wa Pori amefukuzwa kazi kutokana na kuwaondoa watu waliovamia pori hilo kwa kukata miti na kuingiza mifugo mingi. Mhifadhi huyo amefukuzwa kutokana na amri ya Mamlaka ya Juu ya Wizara.

Kama hiyo haitoshi, kuna operesheni inayoendelea ya kuwakamata vibompa wa Meno ya Tembo. Operesheni hiyo imeanza juzi. Hata hivyo, mamlaka ya Juu ya Wizara ya Maliasili na Utalii ikaingilia kati ili wanaohusika na biashara hiyo akiwemo jamaa mmoja anayejulikana kwa jina la Mpemba asikamatwe. Bahati nzuri Mheshimiwa Rais aliinyaka hiyo hewani na akasimama yeye mwenyewe kuongoza Operesheni hiyo. Hivi tunavyozungumza hali ni mbaya sana kwa hao jamaa ambao walidhani kuwa kwa nguvu ya pesa waliyonayo hawawezi kukamatwa.

Kwa mifano hii michache, sioni wapi ataponea Prof Maghembe. Jipu tayari limeiva na litatumbuliwa soon.
Wewe huyo huyo ndiye uliunga mkono pale ambapo katibu mkuu wa chama chako walipoitwa mawaziri mizigo maghembe akiwa mmoja wa hao mawaziri mizigo!...Alipoteuliwa na mkulu,Ukaonyesha wasiwasi kwa prof!.....Baada ya suku 100 prof.akiwa ofisini kama waziri,Ukasema kuwa prof ana kasi ya utendaji unayoendana nasi ya mkulu!....Leo umeibuka na kusema prof amekalia kuti kavu na hana uwezo wa kuongoza wizara!...Angalia mkuu usije kuwa vuguvugu kwani watakutapika!.....uck mwema
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Binafsi nilikuwa ni miongoni mwa watu ambao tulionesha wasiwasi wetu mara tu baada ya Prof Maghembe kuteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii. Wasiwasi wangu haukutokana na location ambayo Prof Maghembe anatoka bali ni kutokana na ugumu wa Wizara hiyo na uwezo wa Maghembe kukabiliana na changamoto za Wizara.

Hakika nilikuwa sahihi kumjudge negatively. Huko Kagera, Mhifadhi Mkuu wa Pori amefukuzwa kazi kutokana na kuwaondoa watu waliovamia pori hilo kwa kukata miti na kuingiza mifugo mingi. Mhifadhi huyo amefukuzwa kutokana na amri ya Mamlaka ya Juu ya Wizara.

Kama hiyo haitoshi, kuna operesheni inayoendelea ya kuwakamata vibompa wa Meno ya Tembo. Operesheni hiyo imeanza juzi. Hata hivyo, mamlaka ya Juu ya Wizara ya Maliasili na Utalii ikaingilia kati ili wanaohusika na biashara hiyo akiwemo jamaa mmoja anayejulikana kwa jina la Mpemba asikamatwe. Bahati nzuri Mheshimiwa Rais aliinyaka hiyo hewani na akasimama yeye mwenyewe kuongoza Operesheni hiyo. Hivi tunavyozungumza hali ni mbaya sana kwa hao jamaa ambao walidhani kuwa kwa nguvu ya pesa waliyonayo hawawezi kukamatwa.

Kwa mifano hii michache, sioni wapi ataponea Prof Maghembe. Jipu tayari limeiva na litatumbuliwa soon.[/QUOTEU
Ujangiri hauwezi kwisha bila kufuta uwindaji wa kuua wanyama ambao unawahusu vigpgo wa serikali kwa hiyo Mhe Maghembe hana ubavu wa kushindana nao. Mwenye ujasiri wa kutokomeza ujangiri ni rais JPM kwa kufuta hunting safaris full stop.
 
Ila hii habari ni mpasuko kwa kweli. Yaani Waziri anamsimamisha muhifadhi kwa kusimamia sheria!!!

Kuna thread ilikuja humu ya Msukuma kushinikiza jamaa asimamishwe. Ramo Makani naye kaingia mtegoni. Huku unasimamisha muhifadhi wa wanyama wetu, Rais anafanya ziara shtukizi anakutana na vitu Wizarani kwako.

Kama ni mie ningeandika resignation letter mapema sana. Aibu hii ataificha wapi? Na sauti lake lile sasa...
 
Kuna jangili mmoja anaitwa Lazaro Nyalandu sijui wanamuacha vipi. Huu tunaohangaika nao ndio mtandao wake aliomkabidhi Maghembe.
 
rais alikuwa halali anawapima hawa wateule wake afu wewe unasema aliteua wenye uwezo mdogo! huu kama sio uchochezi ni nini?!
 
Haina haja na sidhani kama atamtumbua... wakati anamteua alijua kabisa uwezo wake... na sio Maghembe tu... wapo wengi walioteuliwa kwa kigezo cha ukada...

Na usishangae akitolewa huyo akawekwa Lipumba..
 
Hakuna,, tatizo siyo Maghembe bali ni mamlaka ya uteuzi ndo ina matatizo. Yeye mwenyewe si ndo alitamba kwamba yuko makini kwenye uteuzi? Mbona mambo yanazidi kuharibika tu!! Ila ngoja wamtumbue akalalamike tena huko nje na kuanza kumponda mteuzi wake kwamba hana uwezo!! Yetu macho wacha tushuhudie match kubwa hapa!!
Ili mambo yawe mazuri inabidi yaharibike kwanza!
 
Back
Top Bottom