Prof Janabi awekwa mtu kati

Prof Janabi awekwa mtu kati

Kanatumia Kodi zetu Boss! Na kalivyo kakavu sasa mpaka WHO inaweza kuogopa!😁😁😄
Ni ujinga sana, Sioni faida ya huyo kutumia kodi zetu kutafutiwa ajira. Kama anaweza afanye hapa Tanzania kwanini wampiganie kwa pesa zetu?
 
Yaani ogopa mtu anaongea facts kwa taratibu maana yake amekudharau sana kiasi anataka kila neno lisikike. Pamoja siyo mtaalam wa afya ila nilishaonaga huyu Janab hana kichwa kizuri.
 
Mwafrika anavyo jichukia ni balaa hasa akiona mafanikio ya mwenzake.
Huyo mzungu zuzu hana lolote ajuwayo. Hapa mjadala ulikua juu ya madhara ya sukari kwa mwili wa binaadamu na sio kemia ya sukari
Kwani maelezo ya huyo mzungu kupitia kemia anatoa jibu gani kama si uwingi wa sukari mwilini?.

Pasipo kemia bado huwezi elezea tatizo, ufanisi au madhara ya sukari.
 
Sasa ndugu yangu hiyo si Biology ya form two?

Mbona mnakuza kama kitu kinachohotaji maarifa makubwa mno
wengine walichora panzi wakaishia hapo wakaanza kujifunza mambo ya akina kinjeketilengwale
 
Kiongozi, naona unajitahidi kumtetea Prof lakini naona kama utetezi wako hauja kaa sawasawa
Mfano; Mimi nikiwa shambani hula papai moja zima (msimu wa papai) pengine lenye uzito wa 750g
Sasa kama nikiwa nyumbani kikachanganya matunda na kupata pengine uzito wa 350g nikala
ni yupi amekula sukari nyingi?

Itoshe kusema kuwa, Kuchanganya matunda hakuna madhara yoyote ILA KINACHOTAKIWA ni kula kwa kiasi - ule tunda la aina moja au mchanganyiko (yasiwe mengi sana). Wakati wa msimu, wakulima huku mashambani hula tunda la aina moja hadi kushiba kabisa kwa hiyo bora hata wangechanganya.

Nafikiri Prof sio mtaalam wa lishe ILA anaijua lishe kiasi kutokana na kuwa mbobezi wa masuala ya moyo hivyo, lishe ya prof ni respect to heart health na sio Afya ya kawaida ya mwili wa binadamu.....
Kuhusu sucrose (sukari ya jikoni, miwa nk) nafikiri ni vizuri kutumia Sucrose kuliko Glucose anayoitumia ambayo ni sukari iliyochakatwa...
Maongezi ya Prof. hayalengi watu kama wewe ambao mnafanya kazi za kutumia nguvu mashambani (au wale ambao wanashughulisha mwili mara kwa mara). Wewe hata ukila mapapai matatu kwa siku, yanabadilika tu kuwa energy na unayatumia kwenye kazi unazofanya.

Prof. ni mtaalamu wa moyo uko sahihi, na hakuna afya ya mwili bila afya ya moyo.
Sukari za aina zote kama hazitatumika kama energy zikishachakatwa kwenye umengenywaji, end product yake ni fat, ambayo itaenda kutunzwa kwenye mwili, utanenepeana, utapata fatty liver, utakuwa na high cholestrol, utajaa mafuta kwenye mishipa ya damu na matatizo mengineyo mengi.

Umesema vizuri kwenye kula kwa kiasi. Kuchanganya matunda hakuna madhara ya moja kwa moja, ila ukishachanganya most likely utakula mengi kuliko ukila moja na utakula yenye viwango tofauti tofauti vya sukari. Fructose, sukari inayotokana na matunda inachakatwa na ini, small amounts kutoka kwenye matunda hazina shida kabisa ila ukiwa na tabia ya kuzidisha bila kujua, tegemea matatizo.

Shida ya magonjwa yasiyoambukiza yanayotokana na ulaji wa hovyo ni slow progression conditions, inaweza kuchukua miaka 10-20 tokea umeanza kutengeneza tatizo mpaka utakapoona symptoms. Kuna sababu kwanini watu wengi Tanzania wanakufa in their 60's. Mara nyingi shida ya afya utakayoipata ukiwa na miaka 50 au 60, imetokana na ulivyoishi ukiwa na miaka 20, 30, na 40. The body keeps a count, Again, za kuambiwa changanya na zako!

Cc:
Hassanjk
Poor Brain
 
Mambo ya kutufanye tukonde mpk tupeperushwe na upepo hapana hatuwezi kumvumilia..m
 
Mtu muongo hafai kabisa kuwa mkurugenzi wa Kanda wa WHO.
 
Back
Top Bottom