Lowasa alitemwa na Mwalimu kwa tuhuma za ufisadi, wakati huo Rais ana akili timamu na anasikia. Ili awe hapo alipo sasa akasaidiwa na Lowasa aliyetemwa na mwalinu Nyerere. Akalazimisha amweke kwenye nafasi nyeti ya uongozi, wananchi wakamtema kwa sababu zile zile za ufisadi alizotemwa na Hayati Mwl Nyerere.
Sasa jamani tuwe wa kweli, Lowasa ni mchafu kwa nafasi ya uongozi hata kama anabidii katika kazi.
Sifa kuu za kiongozi yeyote wa Kisiasa, jamii, ambazo ni lazima awe nazo zote alipewa Musa, akiongoza wana wa Israeli ( Kutoka 18:19-22) kama ifuatavyo:
1. Mwenye uwezo - Lowasa hana huo uwezo kwa tabia yake ya kukurupuka kufanya vitu au kutamka.
2. Mwenye kumcha Mungu - Lowasa kwa waganga/,wachawi tumeona yupo; msikitini yupo, kanisani yupo nk haeleweki anamwabudu shetani au nani?
3. Mtu mkweli - Lowasa siyo mkweli, hajawahi kuweka hadharani hata sehemu ya mali zake. Jamii yake ni Zitto Kabwe, watu wenye mioyo iliyojaa hadaa na sura za ukarimu.
4. Mtu mwenye kuchukia mapato ya udhalimu- sifa hiyo Lowasa ni ZERO hakuna mtanzania asiyemfahamu kwa kashifa zinazomwandama.
Kumtetea Lowasa kunahitaji mtu ambaye amefunika macho yake kwa magamba ya kobe.
Pili, ukiangalia hao wanaoitwa wachungaji wanao mchawishi hauwakuti kwenye association hata za wachungaji wa pentekoste. Hawajulikani. Ukiangalia picha zao utaona wengine hata kora shingoni haziwatoshi. Najiuliza hivi walipima hizo kora kabla ya kuzivaa? Inaonekana wameshona mashati ya kichungaji na kuokota watu mtaani kisha kuwapachika kora.
Huo usanii umepitiliza. Na kama Lowasa anafikiri anaweza kumhadaa Mungu kwa kutengeneza watumishi feki wa Mungu ili awaaminishe watanzania kwamba anaungwa mkono anajipalia makaa ya moto juu ya nyumba yake.
Nimemaliza.