Power of VFX bongo sijui tunafeli wapi tu

Power of VFX bongo sijui tunafeli wapi tu

Bro, hapo kwenye gharama sina uhakika sana ila moja kati ya vitu vinavoipa thamani movies za wenzetu ni hy VFX, kuna movies mwanzo mpaka mwisho ni VFX tuu halafu unaambiwa bajeti ni Tsh 50T na ukiangalia hy movie kweli ww mwenyewe unaifurahia, kwahy kwa vyovyote vile VFX ni teknolojia ya gharama sana
Gharama zinategemea na aina ya vfx unayotaka kutumia. Labda tuseme unataka kutengeneza movie ambayo inatumia CGI kwa wingi kuanzia wahusika wenyewe (mfano kama akina hulk), location ( mfano kwenye sci-fi movies), hapa lazima utokwe pesa ndefu mno kwa vifaa na team yenye watu wenye akili.

Lakini kama unataka kutengeneza simple vfx kama labda mtu hana kichwa au mtu anakata kichwa, mtu anapaa au anatua kutoka juu, mtu kutuka kutoka ghorofani, mlipuko wa bomu nk hauhitaji gharama kubwa. Unahitaji utaalamu wa kawaida tu wa kutumia green screen na kupangilia shots vizuri.

Hata hivyo kuna baadhi ya vfx hapo hata hazihitaji green screen; kama hiyo ya mtu kupaa au kukatwa kichwa na kikadondoka chini. Ni kupangilia shots tu.

Tatizo watu walio kwenye industry ya filamu ni wavivu mno, hawataki kusoma na kijifunza. Wao wameng'ang'ana na kuthamini makalio kama ndo sifa kuu.
 
Back
Top Bottom