Zakumi
JF-Expert Member
- Sep 24, 2008
- 5,063
- 2,471
Katika mijadala mingi inaonyesha, inaonyesha kuwa watanzania wengi wanakubaliana kuwa chanzo cha matatizo ya nchi yetu ni uongozi. Wengine wanasema kuwa ni nchi inaongozwa bila dira. Wengine wanasema kuwa viongozi ni mafisadi. Na wengine wanasema kuwa viongozi sio wacha Mungu.
Swali langu je tukipata kiongozi mwenye sifa zote hapo juu tutaweza kuondokana na matatizo? Jibu ni 50/50. Tanzania inaweza kupata kiongozi mwenye sifa zote watanzania wanazoziotea ndoto na bado nchi ikaboronga. Sifa zinazotajwa na watanzania wengi sio sifa za kuondoa umasikini na kuboresha maisha ya watanzania wengi. Nasema hivyo kwa sababu kuondoa umasikini na kuboresha maisha kwa nchi masikini kama Tanzania ni Result Oriented Business.
Nikikutana na maadui zangu wanaopenda siasa za Ujamaa, siku zote wananitolea mifano ya mafanikio ya China. Tofauti kubwa kati ya China na Tanzania ni kuwa wa-China are result oriented and Tanzanians aren't. Miaka kama saba iliyopita China na India walikuwa wanashindana kwenye ujenzi wa reli za kasi kwenda kwenye viwanja vya ndege vilivyopo kwenye wilaya za viwanda (Industrial Districts). Katika kipindi cha chini ya miaka mitatu waChina walimaliza ujenzi. Sijuhi wahindi wamefikia wapi. Ujenzi wa viwanja na Olimpiki na uendeshaji wa michezo hiyo nchini China na Ujenzi wa viwanja vya michezo kwa ajili ya jumuia za madola nchini India ni vitu viwili tofauti.
Kwa kutumia mifano hii, inaonyesha safari ya China na Tanzania ni tofauti japokuwa nchi hizi mbili ziliwahi kufuata siasa zinazofanana.
Kuwa mpenda matokeo katika kazi sio siasa. Hivyo kama utajiingiza kwenye mdahalo huu, ningependa mambo ya siasa yakae pembeni. Na jaribu kuelezea uzoefu wako wa kazi au taaluma yako hili tunaweza kubadilisha utamaduni wetu na kuwa watu wa kufanya kazi zenye kuleta matokeo.
Tunaendelea.............................................
Swali langu je tukipata kiongozi mwenye sifa zote hapo juu tutaweza kuondokana na matatizo? Jibu ni 50/50. Tanzania inaweza kupata kiongozi mwenye sifa zote watanzania wanazoziotea ndoto na bado nchi ikaboronga. Sifa zinazotajwa na watanzania wengi sio sifa za kuondoa umasikini na kuboresha maisha ya watanzania wengi. Nasema hivyo kwa sababu kuondoa umasikini na kuboresha maisha kwa nchi masikini kama Tanzania ni Result Oriented Business.
Nikikutana na maadui zangu wanaopenda siasa za Ujamaa, siku zote wananitolea mifano ya mafanikio ya China. Tofauti kubwa kati ya China na Tanzania ni kuwa wa-China are result oriented and Tanzanians aren't. Miaka kama saba iliyopita China na India walikuwa wanashindana kwenye ujenzi wa reli za kasi kwenda kwenye viwanja vya ndege vilivyopo kwenye wilaya za viwanda (Industrial Districts). Katika kipindi cha chini ya miaka mitatu waChina walimaliza ujenzi. Sijuhi wahindi wamefikia wapi. Ujenzi wa viwanja na Olimpiki na uendeshaji wa michezo hiyo nchini China na Ujenzi wa viwanja vya michezo kwa ajili ya jumuia za madola nchini India ni vitu viwili tofauti.
Kwa kutumia mifano hii, inaonyesha safari ya China na Tanzania ni tofauti japokuwa nchi hizi mbili ziliwahi kufuata siasa zinazofanana.
Kuwa mpenda matokeo katika kazi sio siasa. Hivyo kama utajiingiza kwenye mdahalo huu, ningependa mambo ya siasa yakae pembeni. Na jaribu kuelezea uzoefu wako wa kazi au taaluma yako hili tunaweza kubadilisha utamaduni wetu na kuwa watu wa kufanya kazi zenye kuleta matokeo.
Tunaendelea.............................................