Zitto alifanya move mzuri. Tatizo tu ni ubinafsi. Suala hili liko kwenye mpangowa chama. Wamelihubiri kwenye mikutano yao mingi, na kama mnakumbuka vizuri alilianza Dk. Slaa akiwa mbunge. Pia limo kwenye bajeti yao mbadala ya fedha. Alikuwa na haraka gani kuandika barua peke yake, hata kabla hiyo bajeti hajaisoma (mwenyewe) wiki ijayo? Na atueleza hiyo taasisi ya KDI ni ya nani kama si yake mwwnyewe?
Kabla hamjaenda mbali na mjadala hii hapa chini ndiyo barua ya zitto sasa cha muhimu kwa sasa ni ku-assess kama hayo majibu ya bunge yanakidhi maombi ya Zitto. Kwa maoni yangu bunge limeplay politics at its best, maana wao kama waajiri hawampi zitto hizo posho mikonomi sasa kuna ugumu gani kuzideposit huko KDI anakotaka. After all hii haitainvolve any bunge official to do it manually. Kwamba et labda spika itabidi akapange foleni benki....... inasikitisha kuona bunge linashindwa kuaddress hata ishu ndogo kama hizi.
ninawasiwasi kuhusu baadhi ya wabunge wa chadema,as far as suala zima la teamwork linavyohusika. kama tunavyowasikia wenyewe kuhusu suala kufutwa posho inaonekana ni suala la kichama na kambi yao nzima ya upinzani. sasa iweje mtu mmoja aanze ku execute mpango mzima wa chama peke yake? ndo maana zinajengeka hisia za ubinafsi ndani ya chama na hata uzito wa issue yenyewe unapungua inapapelekwa hoja na mtu mmoja mmoja tofauti na ambavyo ingepelekwa na kambi ya upinzani kama hoja ya pamoja. 2. tukiangalia majibu ya ofisi ya bunge, kwamba utaratibu uliopo sasa ni" kumlipa mbunge moja kwa moja" hatuoni kwamba kuna umuhimu wa kupeleka hoja kwanza bungeni au popote panapohusika ili kuubadili kwanza utaratibu huo ili hoja ya kuzifuta iweze kupata nguvu?Mimi naona Bunge linajichanganya kwa sababu Jumanne Asubuhi wiki hii kupitia vipindi vya asubuhi vya TBC1 nilimsikia Naibu Spika Ndugai akisema kuwa kama kweli kambi ya upinzani iko serious kutokutaka posho basi waliandikie barua bunge nalo litawakata hizo posho mara moja. Sasa, nashangaa majibu haya kwa Zitto.
Zitto ana nia njema lakini sidhani kama mtu unaweza kukataa sehemu ya stahili yako kama muajiriwa. Yeye angeweza kuiambia benki yake ipeleke hiyo posho kila ikiingia kule anakotaka wakati akiungana na wenzake kupigana ili hiyo posho iondolewe kwenye stahili ya nafasi ya ubunge.
Amandla......
SOURCE: Zitto na Demokrasia
Update: Posho za Vikao- Majibu ya Ofisi ya BUNGE na Uamuzi Wangu Update: Posho za Vikao- Majibu ya Ofisi ya BUNGE na Uamuzi Wangu « Zitto na Demokrasia
MAJIBU YA OFISI YA BUNGE
Scribd
UAMUZI WANGU-MAJIBU KWA OFISI YA BUNGE
Scribd
ishu si kusema sizitaki. Ni kuelekeza zitumike kufanya nini, na seikali/bunge ikubali kufanya hivyo, vinginevyo utamwachia fisi bucha.Alivyojibiwa sawa sawa, sasa tunamngoja Zitto atangaze aseme mimi sizitaki na kuanzia leo nisilipwe, hapo ndio tutajuwa kweli.
Mimi naona Bunge linajichanganya kwa sababu Jumanne Asubuhi wiki hii kupitia vipindi vya asubuhi vya TBC1 nilimsikia Naibu Spika Ndugai akisema kuwa kama kweli kambi ya upinzani iko serious kutokutaka posho basi waliandikie barua bunge nalo litawakata hizo posho mara moja. Sasa, nashangaa majibu haya kwa Zitto.