Ninasoma uzi nikiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM),nikiendelea na harakati za kusaka elimu.Nimepitia maoni ya wachangiaji mbalimbali ya kufurahisaha na kusikitisha kuhusu hili ama lile.
Kusoma UDSM ni fursa adhimu ikiwa lengo ni kuunda ubongo unaofikiri ipasavyo.Jioni,ukipenda,unapata kahawa,mathalani Utawala,pembeni kukiwa na wanataaluma mbalimbali maarufu na kupata uchambuzi juu ya hili ama lile.Wakati huu huo,Vyuo vingine vya elimu ya Juu vinaendelea kutekeleza wajibu ipasavyo,mathalani SUA,Mzumbe nk.
Hata hivyo kusoma UDSM si lazima kumgeuze mtu kifikra na kimtazamo.Mhitimu wa Mzumbe ama SUA ama CBE ama Mipango anaweza kuwa bora kuliko wa UDSM na kinyume chake.Jina la Chuo haliwezi kuchukua nafasi ya juhudi na utambulisho binafsi wa mhusika.