Nawapongeza sana Die hard fans wa 'vyuo vyenu'. Ukweli ni kwamba hizi rankings zinatumia vigezo mbali mbali hivyo usishangae kuwa hawa wanasema wewe wa 5, wengine wanasema wewe wa 30. Ki ukweli ni faraja sana kuona chuo ulichosoma, unachosoma au unachokipenda kimeshika nafasi za juu. Wakati naanza masomo ya shahada ya kwanza niliamini chuo nnachosoma kinasoko kubwa sana kwenye ajira na ni kweli waajiri wengi walikuwa wanakipenda kwa sababu kadhaa. Lakini nilichogundua ni kuwa pamoja na sababu nyingine, chuo kilikuwa kinapokea bright students; Div 1 na 2 mara chache sana kuona Div 3 kajipenyeza. Pamoja na kuwa elimu iliyokuwa inatolewa ni bora lakini pia wanafunzi wengi wanaochukuliwa ni wale wenye uwezo mzuri. Hii ina advantage sana kwani hata wakimaliza mara nyingi wanafanya vizuri kwenye mitihani ya bodi mbalimbali (NBAA,etc). Hata kwenye usahili wa kazi wanakuwa na advantage zaidi ya wale wanaotoka vile vyuo vinavochukua wanafunzi wenye ufaulu hafifu; nyie mnawaita vilaza. Chuo kina nafasi kubwa ya kumuendeleza mwanafunzi lakini ukweli ni kwamba sehemu kubwa zaidi ya ubora wake ni uwezo binafsi, jitihada, udadisi,kujitofautisha, n.k. Wapo waliomaliza vile vyuo giants TZ UDSM, Mzumbe, SUA (wengine mtajiongeza) lakini miaka nenda rudi hawajaajiriwa, hawajajiajiri, Hawaajiriki, wapo tu. Lakini kuna vijana ambao wametoka vyuo 'dhaifu' (kimtazamo) sitavitaja lakini hawakuchukua round mtaani wakaajiriwa, wakajiajiri na wengine wamefanya mambo makubwa sana kwenye nchi yetu. Chuo kina nafasi kubwa sana ya kukujenga kupitia wahadhiri bora, miundo mbinu, n.k lakini sehemu kubwa sana sio ya chuo ni ya mwanafunzi mwenyewe.
Ikumbukwe pia hata vyuo vipo na 'ubora' kwenye eneo fulani zaidi ya vingine. Ni dhambi kubwa kuilinganisha SUA na Chuo chochote TZ kwenye masuala ya Kilimo, Mzumbe masuala ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimali watu, MoCU na Ushirika, UDSM na Sheria, MuHAS na fani za utabibu, na vinginevyo vingi, japo vipo ambavyo ngumu kuwaelewa kabisa lakini wanakitu wanakifanya. Pia sio ukitoka chuo fulani basi wewe ni Kichwa. Kuna watu tunawafahamu katika siasa, utawala, na mengineyo ambao wametoka UDSM , Mzumbe, n.k lakini wamefanya madudu na kuifilisi hii nchi mpaka aibu hivyo narudi pale pale kuwa mara nyingi ni mwanafunzi mwenyewe.
Chuo kinaweza kukutoa Ujinga kikaukuachia Upumbavu wako ukaenda nao.
Sent using
Jamii Forums mobile app