Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,815
- 11,992
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawatahadharisha wananchi kuhusu taarifa zinazozagaa kutoka kwa mtu mmoja kuwa kutakuwa na maandamano siku ya Jumatatu Juni 19, 2023 kwenda Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam.
Taarifa hiyo anayodai kuwa aliifikisha Polisi, tayari amejibiwa kwa kuyapiga marufuku maandamano aliyokuwa anataka kuyaratibu na kushauriwa kama ana jambo la msingi atumie vyombo mbalimbali vya kisheria anavyoweza kufika na kuwasilisha hoja zake bila maandamano ili haki zingine za wananchi za kufanya kazi wakiwa huru zisiingiliwe.
Jeshi la Polisi linawatahadharisha watu kutoshiriki hicho kinachodaiwa maandamano na badala yake mnahimizwa kuendelea na shughuli zenu za kiuchumi na kijamii bila hofu. Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kwa mtu au kundi la watu linalotaka kuzusha taharuki kwa kuzuia watu wengine kufanya kazi zao.
Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa 10 wanaodaiwa kuhujumu kwa kuiba miundombinu ya vifaa mbalimbali vya minara ya mawasiliano ya simu. Watuhumiwa hao wamekanatwa kufuatia opeshereni maalum kali iliyoanza tarehe Juni 5, 2023 na inaendelea katika Jiji la Dar es Salaaam na mikoa ya jirani.
Waliokamatwa ni pamoja na Husein Ally @ Kijingo (32) Mkazi wa Mbande Kisewe akiwa na wenzake 7 ambao wamekuwa wakiiba betri muhimu na vifaa mbalimbali vya minara ya mawasiliano ya simu katika maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na mikoa jirani.
Jeshi la polisi limekamata pia Simon Mangu (33) mkazi wa Ubungo na mwenzake mmoja baada ya kukutwa na vifaa vya minara ya masawailiano ya simu vya wizi vinavyoibwa na kuvificha maeneo ya Mbezi Luis.
Jeshi la polisi katika Operesheni hiyo limekamata jumla ya betri 68 zenye thamani ya Tsh 163,200,000 na vifaa mbambali vya minara ya mawasiliano ya simu vilivyoibwa magari mawili
(2) yanayotumiwa na wezi hao kubebea vifaa hivyo yamekamatwa ambayo ni Toyota Hilux T.850 BDR, Toyota Carina T.112 BRN na pikipiki MC.901 DJQ, pia vifaa mbalimbali vya kuvujia vimekamatwa. Watuhumiwa wote watapelekwa mahakamani haraka iwezekavyo.
Taarifa hiyo anayodai kuwa aliifikisha Polisi, tayari amejibiwa kwa kuyapiga marufuku maandamano aliyokuwa anataka kuyaratibu na kushauriwa kama ana jambo la msingi atumie vyombo mbalimbali vya kisheria anavyoweza kufika na kuwasilisha hoja zake bila maandamano ili haki zingine za wananchi za kufanya kazi wakiwa huru zisiingiliwe.
Jeshi la Polisi linawatahadharisha watu kutoshiriki hicho kinachodaiwa maandamano na badala yake mnahimizwa kuendelea na shughuli zenu za kiuchumi na kijamii bila hofu. Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kwa mtu au kundi la watu linalotaka kuzusha taharuki kwa kuzuia watu wengine kufanya kazi zao.
Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa 10 wanaodaiwa kuhujumu kwa kuiba miundombinu ya vifaa mbalimbali vya minara ya mawasiliano ya simu. Watuhumiwa hao wamekanatwa kufuatia opeshereni maalum kali iliyoanza tarehe Juni 5, 2023 na inaendelea katika Jiji la Dar es Salaaam na mikoa ya jirani.
Waliokamatwa ni pamoja na Husein Ally @ Kijingo (32) Mkazi wa Mbande Kisewe akiwa na wenzake 7 ambao wamekuwa wakiiba betri muhimu na vifaa mbalimbali vya minara ya mawasiliano ya simu katika maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na mikoa jirani.
Jeshi la polisi limekamata pia Simon Mangu (33) mkazi wa Ubungo na mwenzake mmoja baada ya kukutwa na vifaa vya minara ya masawailiano ya simu vya wizi vinavyoibwa na kuvificha maeneo ya Mbezi Luis.
Jeshi la polisi katika Operesheni hiyo limekamata jumla ya betri 68 zenye thamani ya Tsh 163,200,000 na vifaa mbambali vya minara ya mawasiliano ya simu vilivyoibwa magari mawili
(2) yanayotumiwa na wezi hao kubebea vifaa hivyo yamekamatwa ambayo ni Toyota Hilux T.850 BDR, Toyota Carina T.112 BRN na pikipiki MC.901 DJQ, pia vifaa mbalimbali vya kuvujia vimekamatwa. Watuhumiwa wote watapelekwa mahakamani haraka iwezekavyo.