Wakati Mheshimiwa Rais Magufuli akipigania maendeleo na kufanikiwa kuiingiza Tanzania kwenye uchumi wa kati kabla ya muda uliokuwa ukitarajiwa, jeshi la polisi wilayani Rombo limeendelea kulea na kushirikiana na wezi, wauza gongo, wauza bangi na wakabaji hali iliyosababisha wananchi wa vijiji vya Keni, Manda, Mengwe na Mamsera kuishi kwa hofu na kushindwa kujishughulisha na shughuli za maendeleo
Kutokana na ushirikiano wa karibu uliopo kati ya wauza madawa ya kulevya, majambazi na polisi wa kituo cha Mengwe wananchi wamekuwa hawapeleki ripoti za matukio kituoni hapo kwa kuhofia kulipizwa kisasi na vikundi vya uhalifu vinavyopata taarifa toka polisi wa kituo cha Mengwe
Kwa mfano wiki iliyopita wakala wa Mpesa kwenye soko la Kilesi lililopo kijiji cha Keni alivamiwa na majambazi yenye silaha saa 12 jioni na kupiga risasi hewani na kupora tena umbali wa kilomita 1 kutoka kituo cha polisi Mengwe lakini hakuna msaada uliopatikana.
Wananchi wa Kijiji cha Manda wanajifungia majumbani ifikapo saa 12 jioni kisa uhalifu.
Tunaomba serikali itupie jicho utendaji wa polisi wilayani Rombo hususani kituo cha polisi Mengwe ambacho kimekuwa kituo cha ujambazi badala ya kituo cha polisi.
Wananchi wengi wameumizwa kwa kukatwa mapanga na kuporwa mali zao lakini hawapati msaada wa polisi.
Polisi wa kituo cha Mengwe wamekuwa wakivuruga kesi kwa makusudi hali inayosababisha wahalifu kushinda kesi ambazo walistahili kushindwa, hivyo kuongeza hofu miongoni mwa wananchi.
Polisi wilayani Rombo wanafanya kazi kana kwamba sio sehemu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania chini ya Rais Magufuli.
Tunaomba tafadhali serikali yetu sikivu ichukue hatua za haraka ili kuwanusuru wananchi wasio na hatia dhidi ya uhalifu uliokithiri.
Kutokana na ushirikiano wa karibu uliopo kati ya wauza madawa ya kulevya, majambazi na polisi wa kituo cha Mengwe wananchi wamekuwa hawapeleki ripoti za matukio kituoni hapo kwa kuhofia kulipizwa kisasi na vikundi vya uhalifu vinavyopata taarifa toka polisi wa kituo cha Mengwe
Kwa mfano wiki iliyopita wakala wa Mpesa kwenye soko la Kilesi lililopo kijiji cha Keni alivamiwa na majambazi yenye silaha saa 12 jioni na kupiga risasi hewani na kupora tena umbali wa kilomita 1 kutoka kituo cha polisi Mengwe lakini hakuna msaada uliopatikana.
Wananchi wa Kijiji cha Manda wanajifungia majumbani ifikapo saa 12 jioni kisa uhalifu.
Tunaomba serikali itupie jicho utendaji wa polisi wilayani Rombo hususani kituo cha polisi Mengwe ambacho kimekuwa kituo cha ujambazi badala ya kituo cha polisi.
Wananchi wengi wameumizwa kwa kukatwa mapanga na kuporwa mali zao lakini hawapati msaada wa polisi.
Polisi wa kituo cha Mengwe wamekuwa wakivuruga kesi kwa makusudi hali inayosababisha wahalifu kushinda kesi ambazo walistahili kushindwa, hivyo kuongeza hofu miongoni mwa wananchi.
Polisi wilayani Rombo wanafanya kazi kana kwamba sio sehemu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania chini ya Rais Magufuli.
Tunaomba tafadhali serikali yetu sikivu ichukue hatua za haraka ili kuwanusuru wananchi wasio na hatia dhidi ya uhalifu uliokithiri.