Polisi wengi wanatengwa na Jamii na kuishi kwa msongo mawazo

Boss la DP World

JF-Expert Member
Dec 12, 2021
1,997
7,551
Utafiti wangu mdogo umebaini Watanzania wengi hawana urafiki na polisi, yaani ule urafiki kama wa mtu na mshkaji wake, mfano kupigiana simu kujuliana hali, kutembeleana, kubadilishana mawazo, kushirikiana katika biashara na kupeana michongo.

Mapolisi wengi wanakuwa na urafiki wao kwa wao na kwavile wengi hukutana kazini tu tena ukubwani, basi urafiki wao huwa wa juu juu tu. Vipo visa kadhaa vya askari polisi kuchukua hatua za ajabu kutokana na msongo wa mawazo.

Niliwahi kuzungumza na mkuu mmoja wa FFU katika mkoa fulani akaniambia anaongoza vijana walevi, wagomvi, wenye madeni na mzigo mkubwa wa familia, alinieleza vijana wake ni kama wanaishi kwenye dunia yao.

Nilivyo muuliza hatua gani huzichukua kuwasaidia akasema huwa anajitahidi kuwasaidia wale walio katika hali mbaya zaidi kwa kuwapangia malindo kwenye taasisi za fedha au sehemu nzuri nzuri ili wapate posho ya ziada, pia huwa anawafariji kwa neno la Mungu.

Anasema laiti raia wangekuwa na huruma na upendo kwa polisi huenda jamii ingefuta uhalifu.

Mnaonaje tukianza utaratibu wa kuwatembelea polisi kwenye kota zao, kupiga nao ma stori, kuoa watoto wao, mnadhani itapunguza hizi kelele huku mtaani?
 
Siku nilipo ona polisi ni wapumbavu ni siku polisi niliye mpokea mjini na kumpa malaya asogeze siku alipo pewa kibunda akaja nikamata uso wa mbuzi kisa tulipishana kauli na mdada (mchepuko wa bosi flani )

Tangu hapo siwaamini hawa njagu japo kwenye ukoo wetu 50% ni askari
 
Utafiti wangu mdogo umebaini Watanzania wengi hawana urafiki na polisi, yaani ule urafiki kama wa mtu na mshkaji wake, mfano kupigiana simu kujulian
a hali, kutembeleana, kubadilishana mawazo, kushirikiana katika biashara na kupeana michongo.
Tena siku hizi ni afadhali sana.

Mkoloni na awamu ya kwanza waliwekwa kwenye sehemu zao maalum, ilikuwa ni mwiko kabisa polisi kuishi na raia na kuwa na urafiki na raia.

Naamini hizo kanuni zao bado zipo sema zinafungiwa macho tu siku hizi.
 
siku nilipo ona polisi ni wapumbavu ni siku polisi niliye mpokea mjini na kumpa malaya asogeze siku alipo pewa kibunda akaja nikamata uso wa mbuzi kisa tulipishana kauli na mdada (mchepuko wa bosi flani )

tangu hapo siwaamini hawa njagu japo kwenye ukoo wetu 50% ni askari
Polisi hatakiwi kuwa rafiki yako hata kama rafiki yako wa kweli toka wadogo.Nina majamaa yangu nimesoma nayo O level & Advance walivyoapa tu na mazoea na machizi yamepungua.Ma pot muda wote wanabadilika hao kama asipokuja yeye atakuchomesha kwa mwanae.Ma pot wakuda.
 
Polisi mmoja tulisoma nae O level....alipokuja Dar akaenda ofisi ya classmate wetu....eebanaeeh huyo classmate alimruka kwamba hamjui...polisi anakumbusha na kututaja,jamaa anasema kweli hao nawakumbuka lakini wewe sikukumbuki asilani.🤪🤪🤪
 
Utafiti wangu mdogo umebaini Watanzania wengi hawana urafiki na polisi, yaani ule urafiki kama wa mtu na mshkaji wake, mfano kupigiana simu kujuliana hali, kutembeleana, kubadilishana mawazo, kushirikiana katika biashara na kupeana michongo.

Mapolisi wengi wanakuwa na urafiki wao kwa wao na kwavile wengi hukutana kazini tu tena ukubwani, basi urafiki wao huwa wa juu juu tu. Vipo visa kadhaa vya askari polisi kuchukua hatua za ajabu kutokana na msongo wa mawazo.

Niliwahi kuzungumza na mkuu mmoja wa FFU katika mkoa fulani akaniambia anaongoza vijana walevi, wagomvi, wenye madeni na mzigo mkubwa wa familia, alinieleza vijana wake ni kama wanaishi kwenye dunia yao.

Nilivyo muuliza hatua gani huzichukua kuwasaidia akasema huwa anajitahidi kuwasaidia wale walio katika hali mbaya zaidi kwa kuwapangia malindo kwenye taasisi za fedha au sehemu nzuri nzuri ili wapate posho ya ziada, pia huwa anawafariji kwa neno la Mungu.

Anasema laiti raia wangekuwa na huruma na upendo kwa polisi huenda jamii ingefuta uhalifu.

Mnaonaje tukianza utaratibu wa kuwatembelea polisi kwenye kota zao, kupiga nao ma stori, kuoa watoto wao, mnadhani itapunguza hizi kelele huku mtaani?
Kutoka kwenye familia za kawaida.halafu madaraka makubwa na fedha, vinawachanganya.
 
Kuna jamaa mmoja polisi tulikutana bar nikaona sura hii ya nyumbani si unajua watu wa kanda ya manyara singida na arusha tuna kamfanano fulani.kweli sikuona noma nishalewa nimechangamka nikapiga naye stori nikajitambulisha mastori mengi ya mkoa wetu ugenini..tukabadilishana na namba ....sasa ikapita kama week 2 kuna ishu ikatokea kuna dogo nilimpa simu yangu anishikie akaja kukamatwa kwenye Doria usiku kosa la uzururaji jumamosi hiyo....asubuhi me naitafuta simu nikaambiwa dogo yuko ndani ikabidi niende polisi wakagoma kunipa simu mara ooh ipo chini ya upepelezi nikawasihi sana nikajielezea sana...



Imagine yote hayo yanayokea kituoni jamaa yangu ye kala buyu tu hata kuwashawishi wenzake waniamini hajasema lolote duh nikaona kumbe hakunaga urafiki na PT..

Run murife wakimbie kama unaweza pia uhamiaji na fire..wakimbie
 
Nishawahi kudate na Binti mmoja Kwa kipindi Fulani na tulipendana kweli kweli aisee, alikuwa ananificha kuhusu Mzee wake Kuna siku akaja funguka kuhusu Mzee wake kuwa RPC mkoa Fulani huwezi amini moyo wangu uliyeyuka wote ndio ikawa chanzo Cha kubwagana. Niliogopa wanangu huko mbeleni wasije ishi na laana za Babu Yao Kwa kweli
 
Utafiti wangu mdogo umebaini Watanzania wengi hawana urafiki na polisi, yaani ule urafiki kama wa mtu na mshkaji wake, mfano kupigiana simu kujuliana hali, kutembeleana, kubadilishana mawazo, kushirikiana katika biashara na kupeana michongo.

Mapolisi wengi wanakuwa na urafiki wao kwa wao na kwavile wengi hukutana kazini tu tena ukubwani, basi urafiki wao huwa wa juu juu tu. Vipo visa kadhaa vya askari polisi kuchukua hatua za ajabu kutokana na msongo wa mawazo.

Niliwahi kuzungumza na mkuu mmoja wa FFU katika mkoa fulani akaniambia anaongoza vijana walevi, wagomvi, wenye madeni na mzigo mkubwa wa familia, alinieleza vijana wake ni kama wanaishi kwenye dunia yao.

Nilivyo muuliza hatua gani huzichukua kuwasaidia akasema huwa anajitahidi kuwasaidia wale walio katika hali mbaya zaidi kwa kuwapangia malindo kwenye taasisi za fedha au sehemu nzuri nzuri ili wapate posho ya ziada, pia huwa anawafariji kwa neno la Mungu.

Anasema laiti raia wangekuwa na huruma na upendo kwa polisi huenda jamii ingefuta uhalifu.

Mnaonaje tukianza utaratibu wa kuwatembelea polisi kwenye kota zao, kupiga nao ma stori, kuoa watoto wao, mnadhani itapunguza hizi kelele huku mtaani?


Nafikiri hawajatengwa inavyopaswa vizuri
 
Back
Top Bottom