Polisi wamempora/kumpiga mwanangu

Rugby Union

JF-Expert Member
Nov 21, 2012
402
249
Police1.jpg

Picha linaanza mwanangu ametoka kwenye Sherehe za timu ya soka ya Texas Dume waliokuwa wanashangilia ushindi wao wa Kombe la Diwani wa kata ya Mikocheni, Mchezo ambao ulichezwa jana katika uwanja wa Shule ya Msingi Mikocheni na Texas kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Morning Star.

Jamaa anakaa Kinondoni Mkwajuni, majira ya saa 5 unusu akawa kituo cha daladala cha Chama/TANESKO akingoja usafiri, ama daladala au walau bajaj ya kudandia juu kwa juu.

Difenda ya polisi ikapaki pale kituoni na kumuuliza boi anaenda wapi na anatoka wapi, walipopishana Kiswahili jamaa wakamtia ndani ya Difenda na kumpeleka kituo Kikubwa cha OysterBay.

Kufika huko jamaa akavuliwa suruali, mkanda, waleti na pesa pamoja na kupokea kichapo kikali sana... Kisha akaachwa aondoke na boxer na tisheti iliyoloa damu bila kuchukuliwa maelezo yoyote wala kurudishiwa mazaga ambayo polisi walikwala kutoka kwake.

Mwana akaja gheto asubuhi yuko chapachapa damu, hana nguo zaidi ya boxer na hiyo tisheti iliyoloa damu na kunipa mkasa kama nilivyowaletea ninyi.

Kituo cha Ostabei ndipo yalipo makao makuu ya Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, na raia wanatendwa unyama huu na jeshi linalotakiwa liwalinde tena kwenye ofisi rasmi za usalama.

Swali: Kuna mahali popote ambapo mwana anaweza kupeleka malalamiko, jamaa wakashughulikiwa na bado ikawa salama kwake?
 
Swala ni kwamba hanamkumbuka huyo police na kama anamkumbuka mumsubilieni mtaani au mumfate mkachome nyumba yake full stop tumechoka sasa na hawa ccm

swissme
 
Dawa ni kutojibizana na polisi! Kwanini wapishane kiswahili? Kwani mwana hajui vizuri kiswahili?
Polisi haswa wa kituo cha Oysterbay ni wababe!
Niliwahi kushuhudia vijana wawili wakipigwa na mipini ya majembe kama wanauwa nyoka na polisi mmoja janamke kubwa kama nyumba!
Aisee nilisikitika mno mpaka wanalia Kama watoto kisa eti wamehisiwa kutoroka pale counter!
Sijui ndiyo sheria zinawaruhusu kufanya hivyo?
 
je unaamini vipi ni polisi wamemkamata?
je kama kafumaniwa na mke wa mtu?
je kama ni kibaka kakamatwa huko akapigwa mpaka akakimbia?
je kama kakutwa ananunua changudoa?

isije ikawa anatafuta kisingizio
 
Lugha na uandishi wako unaonyesha (kama ni kweli) huyo mwanao ameambukizwa tabia zako za kihuni na lugha mbovu na huenda aliwakebehi polisi ndio maana wakafanya hivyo (japo sio sheria). BTW wewe una mtoto wa umri mkubwa namna hiyo halafu unatumia lugha za wavuta bangi?
 
Umeandika lugha gani wewe??

huyo mwanao hajapigwa na polisi na alisahau tuu alikamatwa na mzee kifimbo cheza akamchezeshea kichapo kwa lugha yake.

ww mwenyewe umekiri kuwa mwanao walipishana kiswahili na polisi.??

like father like son.
 
Lugha na uandishi wako unaonyesha (kama ni kweli) huyo mwanao ameambukizwa tabia zako za kihuni na lugha mbovu na huenda aliwakebehi polisi ndio maana wakafanya hivyo (japo sio sheria). BTW wewe una mtoto wa umri mkubwa namna hiyo halafu unatumia lugha za wavuta bangi?

Huyo ndio baba sijui mtoto yupo vipi? pili kituo cha daladala saa tano atoke kwenye sherehe ina maana huko anakokaa yupo peke yake? utanisamehe mkuu siamini. mkuu amchunguze sana mwanae. ushauri wangu ampeleke mabatini akatoe maelezo vile vile alivyomueleza asibadili hata herufi moja
 
Huyo ndio baba sijui mtoto yupo vipi? pili kituo cha daladala saa tano atoke kwenye sherehe ina maana huko anakokaa yupo peke yake? utanisamehe mkuu siamini. mkuu amchunguze sana mwanae. ushauri wangu ampeleke mabatini akatoe maelezo vile vile alivyomueleza asibadili hata herufi moja
Haa haa haa. Huyo sio baba mzazi. Ni ile staili ya mateja ya kuitana ''mwanangu vipi''!
 
Huu ni uonevu wa hali ya juu na ni udhalilishaji kwa raia.

Raia anatakiwa kulindwa na si kunyanyaswa na kudhalilishwa
 
Huu ni uonevu wa hali ya juu na ni udhalilishaji kwa raia.

Raia anatakiwa kulindwa na si kunyanyaswa na kudhalilishwa

Raia msela anayekaa bila sababu usiku kwenye kituo cha daladala nae anatakiwa kulindwa?.. hawa masela ndio chanzo cha uhalifu! . Hongera polisi na endeleeni na moto huo huo mpaka masela wote wanaozagaa zagaa hovyo usiku waishe
 
Mwana=msela nondo, mchizi, kachaa, niga etc! Kwa ambao hamkumuelewa mtoa post
 
Mkuu pole subiri wataalam wa sheria watakuja na ushauri ila "the swahili language used here is suggests the kind of dad you're. Tumia kiswahili sanifu
 
Ni bora ukakutana na jambazi lakini sio polisi kwasababu jambazi anaweza akachukua hela akakuacha sio polisi wanachukua hela. Nguo alizo vaa na kichapo juu
 
Back
Top Bottom