Mauzauza ya Misungwi: Sitosahau nilivyotenganishwa na mwanangu kwa masaa 6 na kunusurika kufanywa msukule

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
5,720
10,218
Sikutaka kusimulia kisa hiki lakini nimepatwa msukumo baada ya jamaa yangu kupatwa na jambo lake la kustaajibisha huko Magu.

Miaka ya nyuma nilikuwa nikifanya biashara ya kuuza kemikali za migodini huko kanda ya ziwa.

Nilizunguka Geita, Kahama, Tarime, na sehemu mbalimbali zenye uchimbaji wa dhahabu.

Nikiwa Geita kuna dada nikàwa naupooza moyo wangu. Na niliporudi nyumbani kwa mapumziko, yule mamaa akanitonya kwamba ana ujauzito wangu.

Basi nikamtumia pesa na kumwelekeza hospitali ya jamaa yangu ambapo alianza ku attend clinic.

Baadaye akajifungua salama, na mtoto alipofikisha miaka saba mama yake akasema nikamchukue mtoto, ila ni lazima kwanza nikamilishe taratibu zao za kimila, ikiwa ni pamoja na kulipa ngweke, na vikwerembwezo vingine kibao ili niweze kumkomboa mtoto.

Basi nikiyakamilisha yote, nikapewa mtoto na baada ya siku tatu nikamchukua ili nianz naye safari akakae na ndugu zake wengine niliozaa kwenye ndoa.

Basi usiku mmoja kabla ya safari, mida ya saa nne kasorobo usiku nikapokea simu kutoka kwenye namba nisiyoijua.

Jamaa alikuwa anaongea kwa kunigombeza, huku akifoka na kugandamiza kisukuma, anasema ananidai shilingi milioni moja na nusu kwa kuwa yeye hajapewa mgao wa ngweke.

Nikamwambia uwezo wangu ni kumpa shilingi laki moja anunue mbuzi wawili wakubwa. Jamaa akagoma akakaza kwamba anataka milioni moja unusu.

Nikaona isiwe shida, hawa Wasukuma nikiwaendekeza kila mmoja atakuja na invoice yake isiyo na kichwa wala miguu.

Basi kesho asubuhi safari ikaanza, nikaelekea stand na mtoto wañgu. Tulipofika stand nikaone tupate kifungua kinywa kabisa ili tukianza safari, tusafiri kwa kutulia.

Basi, baada ya kifungua kinywa nikaona tumbo linanivuruga. Kuna duka pembeni na ule mgahawa tuliokula, alkuwa anauza mama wa kama 35 yrs, basi nikamuomba nimuache mwanangu pale ampatie chochote atakacho nami naenda maliwato nikamwachia noti ya 10,000.

Kinbembe kikaanza baadavya kutoka chooni, naona maluweluwe tu, nikajikuta nimetembea pasipo ufahamu wangu, nimetembea kwa miguu kutoka Misungwi Stand hadi Mawe Matatu kwa kina Charles Kitwanga. Mbaya zaidi nilikuwa napita maporini kwa njia zisizo rasmi.

Nikiwa huko mashambani kwenye majaruba ya mpunga akili imeniruka kabisa sikumbuki kuhusu safari, sikumbuki kuhusu mtoto, yaani sikumbuki lolote. Ndio nikakutana na mzee mmoja Akaniongelesha Kisukuma, ulimhola baba, nikajibu mola. Ndio akaanza kunihoji kwa Kiswahili baada ya kugundua kwamba mini sio Msukuma.

Kijàna wangu unaenda wapi? Ndio akili ikafunguka, nikapata ufahamu kwamba natakiwa niwepo safarini. Nikamsimulia kisa kizima.

Mzee akaniambia kwamba ndio nilikuwa nachukuliwa Msukule nikafanywe ndondocha, akanipa dawa fulani hivi nyeusi akanipaka usoni, akaniambia nifumbe macho. Nisifumbue hata atakaposema nifumbue.

Basi ukapita kama muda wa dakika tatu nimefunga tu macho, ila kwa mbali sana nikasikia mtu anasema fumbua macho umefika. Nilipofumbua macho nikajikuta niko stand.

Miguu imejaa tope la kwenye majaruba ya mpunga nikaanza kumtafuta binti yangu.

Muda naenda chooni ilikuwa ni saa mbili kasoro asubuhi, muda huo nimerudishwa stand ni saa 8 mchana.

Kumbe yule mama akaona nimekawia, akaona kama nimemtelekeza mtoto akampele kwenye kituo cha polisi cha hapo Misungwi stand.

Nilipofika pale watu wote wananishangaa kwa jinsi nilivyokuwa valuvalu. Baada ya kujieleza, polisi wakanielewa na kunishauri nianze safari kesho asubuhi.

Dada mmoja polisi alishauri yeye na mtoto wakalale kwake, mimi nitafute guest House ya jirani. Basi dada polisi akampeleka mwanangu nyumbani kwake ambako aliungana na watoto wa afande. Kisha afande akarudi kazini.

Mida ya saa 12, afande akatoka kazini kwake na akataka kujua nipo. Nilimwelekeza kwamba niko kwenye Bar ya Bariadi, basi akaja na kuni join. Akashauri tuhamie Facebook.

Tukaenda huko Facebook, tukanywa mpaka very late hours. Akaniambia anataka kulala, tukachikua chumba tukalala hadi kesho yake.

Asubuhi akawahi kwake, kisha akanda kazini, ambako aliomba ruhusa.

Nikaongeza siku mbili zankuwepo pale Misungwi ndipo nikarudi Dar.

Ukifanya mchezo Usukumani unafanywa msukule kirahisi tu, bila sababu za msingi.
 
Hii ni Moja ya Air port ya jadi pale Kanda ya ziwa
1684320116854.jpg
 
Duh.
Mimi niko kahama, ila sitaki kuzoeana na wanawake wa kisukuma .

Kuna mmoja nilimjunja bila kumpa hela, nikawa na wasiwasi anaweza akanifanyizia ila nikaona kapotezea.

Emu tuma namba ya huyo Afande nibonge naye hapo misungwi si mbali
 
Duh.
Mimi niko kahama, ila sitaki kuzoeana na wanawake wa kisukuma .

Kuna mmoja nilimjunja bila kumpa hela, nikawa na wasiwasi anaweza akanifanyizia ila nikaona kapotezea.

Emu tuma namba ya huyo Afande nibonge naye hapo misungwi si mbali
Wanawake wa kisukuma sio wachoyo hasa wanyantuzu
 
Back
Top Bottom