Polisi wamempora/kumpiga mwanangu

Polisi wamempora/kumpiga mwanangu

Zimefika mkuu, nasikitika mabadiliko hayaji kama zali... Ni lazima tuyalete!

Pole sana mkuu! Polisi wetu hawana u karibu kabisa na raia,umenikumbusha zamani Enzi za Udogo kwa sisi tuliokulia life ya uswazi polisi walikuwa walipiga doria lazima tufungishwe mashati tunasongeshwa kituoni huko kutolewa ni mpaka mapene,hapo tushabambikiwa vipisi vya bange...ilikuwa uonevu sana
 
Kuna kapolisi kamoja kamekuja kuulizia chumba cha kupanga kwangu nimekatimulia mbali, nimekaambia sipangishi vipolisi vya sirikali iliyopo sasa hadi baada ya oktoba itakapotolewa out!
 
Swala ni kwamba hanamkumbuka huyo police na kama anamkumbuka mumsubilieni mtaani au mumfate mkachome nyumba yake full stop tumechoka sasa na hawa ccm

swissme
Kwa sasa hatujafikiria hivyo, lakini kama hali ikiendelea hivi jamaa watakuwa hawakai kwa amani maana hakuna atakayewapa ushirikiano, kuwapangisha nyumba, kuwapa mke wala chochote.

Sina mazoea na Polisi, na hata ndugu yangu akiwa poti basi undugu wetu uko mashakani!
 
Dawa ni kutojibizana na polisi! Kwanini wapishane kiswahili? Kwani mwana hajui vizuri kiswahili?
Polisi haswa wa kituo cha Oysterbay ni wababe!
Niliwahi kushuhudia vijana wawili wakipigwa na mipini ya majembe kama wanauwa nyoka na polisi mmoja janamke kubwa kama nyumba!
Aisee nilisikitika mno mpaka wanalia Kama watoto kisa eti wamehisiwa kutoroka pale counter!
Sijui ndiyo sheria zinawaruhusu kufanya hivyo?
Mwanangu akishaweka vitu vyake kichwani ana majibu fulani ya shombo, lakini sidhani kama alistahili kipigo kikubwa na kuporwa ukizingatia tayari walikuwa wameshamkamata.

In fwakti jamaa aliokolewa na poti mwingine ambaye alimtoa mlango wa nyuma baada ya kuhisi atakufa kwa kipigo! Akina poti hata ukiwa baa kaa nao meza ya mbali, sio binadamu!
 
je unaamini vipi ni polisi wamemkamata?
je kama kafumaniwa na mke wa mtu?
je kama ni kibaka kakamatwa huko akapigwa mpaka akakimbia?
je kama kakutwa ananunua changudoa?

isije ikawa anatafuta kisingizio
Boi hawezi kunitafutia visingizio mimi maana sio mtu wa hivyo, angefumaniwa au angekutwa na scenario ingine ya aibu zaidi angeniambia pasi na shaka, ni mtu wangu wa nguvu!
 
Raia msela anayekaa bila sababu usiku kwenye kituo cha daladala nae anatakiwa kulindwa?.. hawa masela ndio chanzo cha uhalifu! . Hongera polisi na endeleeni na moto huo huo mpaka masela wote wanaozagaa zagaa hovyo usiku waishe
Wamemkuta peke ake, sioni tatizo hapo. Na pengine alikuwa na vifaa vya michezo kwenye begi lake.

Haya twende unavyotaka wewe, tufanye wamemshuku muhalifu je walipomsachi walimkuta na silaha yoyote au wamemkuta na kitu chochote kinachoweza kumdhuru mtu mwingine? jibu hapana.

Kwahiyo walichotakiwa polisi kufanya ni kumsachi na kwa vile wamemkuta yuko safi basi wamuulize anapoelekea na ikiwezekana wamsaidie usafiri mpaka nyumbani kwake, mafuta ya serikali na ukumbuke kodi ya mlalahoi ndio inayonunua mafuta hayo, sasa kuna tatizo gani kumsaidia raia wake!

Hao ndio polisi wetu badala ya kumlinda raia wake badala yake wanamwonea au kumdhalilisha
 
Wamemkuta peke ake, sioni tatizo hapo. Na pengine alikuwa na vifaa vya michezo kwenye begi lake.

Haya twende unavyotaka wewe, tufanye wamemshuku muhalifu je walipomsachi walimkuta na silaha yoyote au wamemkuta na kitu chochote kinachoweza kumdhuru mtu mwingine? jibu hapana.

Kwahiyo walichotakiwa polisi kufanya ni kumsachi na kwa vile wamemkuta yuko safi basi wamuulize anapoelekea na ikiwezekana wamsaidie usafiri mpaka nyumbani kwake, mafuta ya serikali na ukumbuke kodi ya mlalahoi ndio inayonunua mafuta hayo, sasa kuna tatizo gani kumsaidia raia wake!

Hao ndio polisi wetu badala ya kumlinda raia wake badala yake wanamwonea au kumdhalilisha


Huwajui masela wa kinondoni Mkwajuni wewe!...
 
Huwajui masela wa kinondoni Mkwajuni wewe!...
Labda tunashindwa kuelewana padogo.

Mimi siwatetei wahalifu na wala sitaweza kuwatetea hata siku moja sababu sikubaliani na wanachokifanya.

Hapa sikubaliani na polisi wetu kwa kitendo walichomfanyia mtoto wa ndugu yetu hapo juu.

Kunikuta saa tano za usiku halafu niko peke yangu sio sababu ya kusema mimi ni mwalifu, inaweza kumtokea mtu yoyote na si kwa michezo tu, pengine nauguza hospitalini na muda wa kurejea nyumbani umekuwa usiku, sasa katika harakati za kusubiri chombo cha usafiri ndio iwe kosa kwakuwa ni usiku?
 
Kama baba mwana ndiyo hivi, basi hapana budi huyo mwana kupishana lugha na vijana Mangu.
 
Wapigwe tu maana hakuna namna nyingine
Eeenh! Wapigwe tu na mimi nasema muwapige tu
 
Huyo mwanao ana miaka mingapi inaonekana hukumpa malezi bora kipindi cha utoto wake na una ushahidi upi kama katoka kituoni muulize vizuri labda katoka kufumaniwa..!!
 
Nawashangaa sana Polisi wa tz yaani wanajiona kama waungu hi ilimtokezea mdogo wangu pia Wakati anarudi kwenye mizunguko Yake usiku alikua na pikipiki Hafla akasimamishwa na mapolisi Wakata kumpiga katika purukushani alifanikiwa kukumbia ndio ikawa salama Yake.......kitu alichowalipiza ni hatari na kinachekesha sana
 
polisi kawaida wana maswali ya maudhi

ukiwa kma sisi tuliovurugwa lazima umpe vipande vyake

mwisho wa siku wanaleta ubabe

kwa jinsi polisi wetu walivyo waonevu hata nikisikia kituo kimelipuliwa na bomu sitasikitika
 
HARUFU

Wewe ndio unashindwa kuelewa panogo sana!!..huyo sio mwanawe wa kumzaa! Ni msela wake na ushaambiwa akishavuta huwa anaweza kufanya chochote!..sasa huelewi nini hapa?

Jadili tukio usitoke nje ya mada
 
Last edited by a moderator:
Lugha na uandishi wako unaonyesha (kama ni kweli) huyo mwanao ameambukizwa tabia zako za kihuni na lugha mbovu na huenda aliwakebehi polisi ndio maana wakafanya hivyo (japo sio sheria). BTW wewe una mtoto wa umri mkubwa namna hiyo halafu unatumia lugha za wavuta bangi?
Lugha ya mvuta bangi ni ipi mkuu. Sisi wanazuoni wa lugha tumefunzwa kuwa maneno yote katika lugha ni matakatifu na hakuna ubaya kuyatumia...

Niliposema mwanangu sikumaanisha zao la viuno vyangu, bali mtu wangu wa karibu, simela, homeboi, kichaa wangu...
 
Back
Top Bottom