Habari wana JF,
Kuna huu wizi sijui niite utapeli ambao binafsi nimeanza kuushuhudia tangu mwaka 2022 kwa maeneo ya Kariakoo na kila mara nikipita eneo hilo nakuta huo wizi unaendelea utapeli wenyewe unafanywa na jamaa wauza juice ya miwa mitaa ya karume mbele ya TBL (Tanzania Breweries Limited)
Wizi unafanyika kama ifuatavyo:
Muuza juice atakuita na kujifanya amekufananisha kisha atakuuliza ''Vipi mzee daah kitambo sana mwanangu, vipi siku hizi wapi?''
Wewe utajibu labda nipo Magomeni siku hizi.
Muuza juice: Anhaa ndiyo maana kule kitaa sikuoni siku hizi.
Wewe: Wapi? Kule kitunda au?
Basi hapo ndo utakuwa umeyavagaa jamaa atajifanya kukujua sana atakuuliza kuhusu story za vipi wale jamaa wanaopiga matizi uwanjani pale bado wapo?
Actually hakuna sehemu ambayo haina uwanja wa mpira so yote kwa yote jamaa atakuwa amekuteka akili kwa kujifanya anakujua sema ni vile tu umemsahau
Kinachofuatia jamaa atakumiminia juice " karibu juice kaka".
Ukimaliza kunywa tu hiyo juice jamaa anakubadilikia na kuanza kukudai hela ya Juice.
ukishindwa kulipa atakukaba, atakupiga hata kukuumiza.
Wahanga wakubwa wa haya matukio ni wale wa kuja lakini hata kama born town unaweza kujikuta umeingia mkenge vile vile
Kinachonifikirisha ni kuwa Kituo cha polisi Gerezani hakipo mbali na hapo Karume na pia maeneo ya China Plaza, hawa jamaa hawajanusa taarifa za huu ushenzi kweli? Au kuna mgawo, maana hawa jamaa wanafanya hii michezo kuanzia asubuhi hadi jioni tangu 2022 nimewaona hadi leo 2024 wapo.
Picha mojawapo ya mhuhusika wa hiyo michezo ni hiyo hapo huyo muuza juice na hapo alikuwa anamuingiza mkenge jamaa.
Kuna huu wizi sijui niite utapeli ambao binafsi nimeanza kuushuhudia tangu mwaka 2022 kwa maeneo ya Kariakoo na kila mara nikipita eneo hilo nakuta huo wizi unaendelea utapeli wenyewe unafanywa na jamaa wauza juice ya miwa mitaa ya karume mbele ya TBL (Tanzania Breweries Limited)
Wizi unafanyika kama ifuatavyo:
Muuza juice atakuita na kujifanya amekufananisha kisha atakuuliza ''Vipi mzee daah kitambo sana mwanangu, vipi siku hizi wapi?''
Wewe utajibu labda nipo Magomeni siku hizi.
Muuza juice: Anhaa ndiyo maana kule kitaa sikuoni siku hizi.
Wewe: Wapi? Kule kitunda au?
Basi hapo ndo utakuwa umeyavagaa jamaa atajifanya kukujua sana atakuuliza kuhusu story za vipi wale jamaa wanaopiga matizi uwanjani pale bado wapo?
Actually hakuna sehemu ambayo haina uwanja wa mpira so yote kwa yote jamaa atakuwa amekuteka akili kwa kujifanya anakujua sema ni vile tu umemsahau
Kinachofuatia jamaa atakumiminia juice " karibu juice kaka".
Ukimaliza kunywa tu hiyo juice jamaa anakubadilikia na kuanza kukudai hela ya Juice.
ukishindwa kulipa atakukaba, atakupiga hata kukuumiza.
Wahanga wakubwa wa haya matukio ni wale wa kuja lakini hata kama born town unaweza kujikuta umeingia mkenge vile vile
Kinachonifikirisha ni kuwa Kituo cha polisi Gerezani hakipo mbali na hapo Karume na pia maeneo ya China Plaza, hawa jamaa hawajanusa taarifa za huu ushenzi kweli? Au kuna mgawo, maana hawa jamaa wanafanya hii michezo kuanzia asubuhi hadi jioni tangu 2022 nimewaona hadi leo 2024 wapo.
Picha mojawapo ya mhuhusika wa hiyo michezo ni hiyo hapo huyo muuza juice na hapo alikuwa anamuingiza mkenge jamaa.