Polisi Michael Rasha Atoa ujumbe kwa IGP Wambura. Rais Samia ampe Ukuu wa Wilaya

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Kumbe sio kila Polisi ana roho mbaya wala katili. Wapo Polisi baadhi wema.

Yupo Rasha mmoja kwa Polisi 1,000. Sema watu kama hawa wanakomolewa kwa kupelekwa Vijiji vya ndani ili wasionekane kitaifa.

Rasha alitakiwa ahudumie japo Wilaya nzima sio kata tu.

Wanaotenda mema bila kujali mapito yao, tuwatie moyo

Nilimshuhudia akivusha wanafunzi kwenye mto uliofulika wengine akiwabeba Mgongoni.

Mungu amlipe nini?
Screenshot_20231122-211019.png

Polisi Kata wa Kata ya Usangule Wilaya ya Malinyi Mkoani Morogoro Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Michael Rasha akiongea na kumfariji mtoto Erick Hongera (6 ) ambaye amekuwa akikaa kwa upweke katika maeneo ya Shule.

Mtoto Erick amekuwa na mazoea ya kwenda shule ya Msingi Manda Juu na kukaa nje ya jengo la shule hiyo kwa upweke na mfadhaiko kutokana na wazazi wake kutokumpeleka shule.

Mkaguzi Rasha ameongea nae na kumfariji ili kuona ni jinsi gani anaweza kumsaidia aweze kujiunga na watoto wenzake ili kupata haki yake ya msingi ya kusoma.

Katika harakati za kumsaidia mtoto huyo, Mkaguzi Rasha amechukua hatua ya kwenda kuongea na wazazi wake ili kujua changamoto na kuitafutia ufumbuzi ili mtoto huyo aweze kwenda shule kama wanafunzi wenzake.

Credit: Picha na caption nimeitoa Channel ten
 
Hongera kwake huyu jamaa,ni mfuatiliaji mzuri wa mambo akionekana atafika mbali.

Nime-zoom kumtizama huyo mtoto nikamtizama na mwanangu hapa pembeni yangu hadi huruma,Tanzania tuna hali ya umaskini mbaya sana viongozi angalao wawakumbuke watoto kama hawa wanaotafuta faraja ya kupata hii elimu yetu ya kuunga unga.
 
Mkuu heshima kwako.

Kweli kuna mapolisi wana roho ya kiungwana sana.

Nimemkumbuka mmoja Kati ya Igunga na Nzega wakati barabara ya lami inajengwa..alisaidia watu tuliokuwa tunasotea kazi.

Kila siku chakula cha mchana tulikula kwake.

Pia ni mkulima alikuwa na TATA jeupe...bakhti mbaya jina limenitoka.
 
Hongera kwake huyu jamaa,ni mfuatiliaji mzuri wa mambo akionekana atafika mbali.

Nime-zoom kumtizama huyo mtoto nikamtizama na mwanangu hapa pembeni yangu hadi huruma,Tanzania tuna hali ya umaskini mbaya sana viongozi angalao wawakumbuke watoto kama hawa wanaotafuta faraja ya kupata hii elimu yetu ya kuunga unga.
Tumuombee manake chuki fitna na majungu...vitamwandama hivi punde.
 
Kwa hakika Nampongeza kabisa kwa moyo wake huo wa upendo na ukarimu mkubwa sana wa kumsaidia mtoto huyo . Hiyo ni sadaka kubwa sana mbele za Mwenyezi Mungu ambayo anaipokea moja kwa moja.

Mungu atamlipa kwa wema wake na uungwana wake alioutenda kwa mtoto huyo.atamlipa zaidi ya msaada anaoutoa.

Nasi wengine hatuna budi kuiga moyo wa namna hiyo kwa kuwatendea wengine wema na hivyo kuwapatia nuru, matumaini, tabasamu na furaha katika mioyo yao iliyokuwa imekata Tamaa,kuvunjika moyo,kuona giza mbele,kuwa na upweke na kukosa matumaini.
 
Mkaguzi kachukua hatua sahihi kabisa, kwanza, kwenda kusikiliza tatizo kwa Wazazi. Hivi ndivyo suluhu ya jambo inavyotatafutwa

Kwa upande mwingine sisi kama Taifa tumefeli. Huyu mtoto 'akiwa Ali Dangote' ( Mungu saidia asiwe) tunalaumu Wazazi na mtoto. Tunashindwa kuelewa hatukumuandaa kuanzia utotoni.

Tupo bize kuangalia ma V8 mangapi yatanunuliwa kwa viongozi gani.
Tupo Bize kushabikia Wabunge wanaogawa kofia na vitenge
Tupo Bize kutunga sheria za kuwalipa Wapenzi wanapostaafu kwa kisingizo cha '' wenza wa viongozi''

Tunapata wapi fedha za kuhudumia hayo hapo juu! kutoka kodi za Baba na Mama wa huyu mtoto au huyu mtoto mwenyewe siku atakapoweza kubeba gunia sokoni kwa mgongo.

Pascal Mayalla JokaKuu
 
Kwa hakika Nampongeza kabisa kwa moyo wake huo upendo.kumsaidia mtoto huyo ni sadaka kubwa sana mbele za Mwenyezi Mungu ambayo anaipokea moja kwa moja .Mungu atamlipa kwa wema wake na uungwana wake.atamlipa zaidi ya msaada anaoutoa .Nasi wengine hatuna budi kuiga moyo wa namna hiyo kwa kuwatendea wengine na hivyo kuwapatia nuru, matumaini, tabasamu na furaha katika mioyo yao.
V8 tano zinaweza hudumia watoto kama Hawa nchi nzima.weka Uzi wa kupinga V8,tuhudumie Hawa watoto wa maskini,wako wengii nchini
 
Hongera kwake huyu jamaa,ni mfuatiliaji mzuri wa mambo akionekana atafika mbali.

Nime-zoom kumtizama huyo mtoto nikamtizama na mwanangu hapa pembeni yangu hadi huruma,Tanzania tuna hali ya umaskini mbaya sana viongozi angalao wawakumbuke watoto kama hawa wanaotafuta faraja ya kupata hii elimu yetu ya kuunga unga.
Huyu ana ubinadamu na hata sura yake inaonyesha. Tanzania tuko kwenye lindi la ufukara mkubwa sana lakini watawala wanavyotumbua maraha utadhani hakuna shida. Bora watu waingieni mpirani ili apate umaarufu kuliko mtoto kama huyu kwenda shule. Ila sehemu nyingine.... hivi hata hao waalim wa hiyo shule walishindwa kufanya jambo lolote? Au nisiwalaumu sana kwa sababu huyu ni mmoja tu kati ya wengi shida...
 
Kwa hakika Nampongeza kabisa kwa moyo wake huo upendo.kumsaidia mtoto huyo ni sadaka kubwa sana mbele za Mwenyezi Mungu ambayo anaipokea moja kwa moja .Mungu atamlipa kwa wema wake na uungwana wake.atamlipa zaidi ya msaada anaoutoa .Nasi wengine hatuna budi kuiga moyo wa namna hiyo kwa kuwatendea wengine na hivyo kuwapatia nuru, matumaini, tabasamu na furaha katika mioyo yao.
Unafiki tu ungekuwa na akili kupitia matukio kama haya usingekuwa unasifia sifia viongozi wa serikali wasiojua nini maana ya kuongoza!!!

Miaka 60 ya uhuru bado tuna watoto wanakosa nafasi ya kusoma hata elimu ya msingi kiasi wanasikitikia uwepo wao duniani,I can feel mtoto wa miaka 6 anakaa kwa huzuni kiasi hiko kisa kukosa shule anajisikiaje ktk nafsi yake.
 
Huyu ana ubinadamu na hata sura yake inaonyesha. Tanzania tuko kwenye lindi la ufukara mkubwa sana lakini watawala wanavyotumbua maraha utadhani hakuna shida. Bora watu waingieni mpirani ili apate umaarufu kuliko mtoto kama huyu kwenda shule. Ila sehemu nyingine.... hivi hata hao waalim wa hiyo shule walishindwa kufanya jambo lolote? Au nisiwalaumu sana kwa sababu huyu ni mmoja tu kati ya wengi shida...
Inasikitisha,mara ya mwisho sikumbuki ilikuwa league gani nilimsikia kiongozi wa nchi akisema angenunua goal moja kwa 20mill.

Tuna laana!
 
Kwa hakika Nampongeza kabisa kwa moyo wake huo upendo.kumsaidia mtoto huyo ni sadaka kubwa sana mbele za Mwenyezi Mungu ambayo anaipokea moja kwa moja .Mungu atamlipa kwa wema wake na uungwana wake.atamlipa zaidi ya msaada anaoutoa .Nasi wengine hatuna budi kuiga moyo wa namna hiyo kwa kuwatendea wengine na hivyo kuwapatia nuru, matumaini, tabasamu na furaha katika mioyo yao.
Hali ni mbaya mno viongozi wapo kwa ajili ya maslahi yao ila nashangaa kijana kama wewe ambae ni mfumo umechangia kwenu ni maskini unaoña ccm ndio tumaini
 
Unafiki tu ungekuwa na akili kupitia matukio kama haya usingekuwa unasifia sifia viongozi wa serikali wasiojua nini maana ya kuongoza!!!

Miaka 60 ya uhuru bado tuna watoto wanakosa nafasi ya kusoma hata elimu ya msingi kiasi wanasikitikia uwepo wao duniani,I can feel mtoto wa miaka 6 anakaa kwa huzuni kiasi hiko kisa kukosa shule anajisikiaje ktk nafsi yake.
Acha makasiriko. Hili ni Jukwaa huru kwa kila mtu kusifia apendacho. Sasa unataka usifie upande wako tu. Tuwape nafasi watu waseme. Tukosoane kwa upendo na kuelekezana kwa heshima
 
Back
Top Bottom