ABEDNEGO
Senior Member
- Aug 20, 2009
- 109
- 30
Ilikuwa majira ya saa nne na nusu usiku wa jana,Polisi wa kituo cha Oysterbay walipotumia risasi za moto kuumua kijana Octavian fundi magari eneo la Victoria karibu na nyumba za viongozi.Polisi aliyehusika na tukio hilo anajulikana kwa jina moja la Constable Crycipin.Ambaye alitumia bastola yake kumpiga na kumuua kwa mabishano yasiyomhusu kijana huyo.Mashuhuda waliokuwa katika eneo la tukio wanadai kuwa polisi hao waliletwa kwenye gari mbili aina ya RAV 4 na cresta(Namba zimehifadhiwa) na wasichana wawili (Changudoa) waliokuwa wakimsaka mtoto wao waliyedai alichukuliwa na babake bila ya ridhaa yao.Ndipo katika majibishano ya mdomo askari huyo alichomoa bastola na kumuua fundi magari huyo ambaye alikuwa hahusiki na ugomvi huo.Cha kushangaza na kukatisha tamaa ni jinsi polisi walivyolichukulia kwa urahisi jambo hilo kiasi ya kwamba Muuaaji hakufanyiwa gwaride la utambulisho wala kutoa maelezo kituoni.
Askari Muuaji Constable Cricipin huyu hapa (Angalia attachment):mad2:
Askari Muuaji Constable Cricipin huyu hapa (Angalia attachment):mad2: