Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane

Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane

Taarifa yoyote ikishakuwa na jina Tanzania Daima inakuwa ya UDAKU.
Wakati mwingine tumieni hata akili kidogo tu kama mnazo. Sasa wahusika wa polisi wamethibitisha kufanya hivyo, wewe una judge gazeti badala ya kujadili hoja! Suala hapa ni kweli au si kweli kuwa polisi walivamia nyumbani kwa Mbowe si nani karipoti uvamizi huo!
 
Mkuu Polisi wanatumika tu kutekeleza matukio ya wakubwa zao, pamoja na hayo wao pia wanastahili lawama. Haya yote yanayoendelea DHAIFU atakuwa anayafahamu hivyo yeye ndio anastahili lawama nyingi zaidi. Nchi iko katika njia panda bila hekima na busara za hali ya juu inaweza kutumbukia kwenye machafuko ya kutisha.

Watawala wa sasa wanawaharibia sana hawa vijana makamanda wa Polialsi kwasababu kwa utaratibu unaopendekezwa ktk rasimu ya Katiba Mpya hawataweza pita mchujo mkali utaokuwa unafanyika kuwapata wakuu wa Taasisi muhimu za Serikali na Ulinzi na Usalama.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Polisi wana haki ya kumkamata mtu muda wowote wanaopenda.

Kwa sheria gani?

Unajua kwamba kila PUMBA unayoandika unajisogeza karibu zaidi na Jehanam?

Hakika kauli zako ni zaidi hata ya Lucifer! Una laana gani we mtoto?

Hebu jirudi kabla hujachelewa, kwani Mungu akikuita wakati wowote, hutauona mlango wa pepo. Si mimi nasema. Kauli zako zinakuhukumu!
 
Polisi wana haki ya kumkamata mtu muda wowote wanaopenda.
-------- wewe! Tanzania ina taratibu zake kisheria na sio polisi wanapojisikia!
Polisi wafuate sheria kama ambavyo wanataka raia wafuate sheria!
 
Kuna tofauti kati ya video ya Arusha na video za CDM kupanga ugaidi, elewa hilo.
Arusha, crime imetokea, watu wamekufa halafu unaficha ushahidi?
Pia, itakuwa ni uzembe wa kufikiria ukidhani kuwa mtu kama mwigulu hayuko under surveillance .... of course he is!!
Kuna intelligence CDM, CUF, NCCR hata CCM. Ukiwa kiongozi wa kisiasa most likely utakuwa under surveillance, hata baadhi ya wachangiaji humu wapo under surveillance, huwezi kuniaminisha mtu kama Maxence, au Mchambuzi asiwe spied? Au hata Dr. Slaa na wengineo .. tofauti ni who is spying who.

iT'S A DIRTY GAME!
Kobello, kesi ya kuku hapelekewi jogoo!
 
Last edited by a moderator:
uongozi wa kisiasa ukibadilika nchi hii polisi watakuwa kwenye nafasi gani?
 
Mkuu tuombe tupate hiyo katiba ambayo Watanzania wengi tutaikubali. Inaweza kabisa kuandikwa katiba ambayo wengi hatutaiafiki kwa kuwa inaweza kuwa na madudu mengi yaliyomo kwenye hii katiba ya sasa iliyojaa viraka vya kutisha. Tumeshaziona dalili za hali ya juu za CCM kuhakikisha inaandikwa katiba ambayo wanaitaka wao ili waendelee kuiangamiza nchi milele.

Watawala wa sasa wanawaharibia sana hawa vijana makamanda wa Polialsi kwasababu kwa utaratibu unaopendekezwa ktk rasimu ya Katiba Mpya hawataweza pita mchujo mkali utaokuwa unafanyika kuwapata wakuu wa Taasisi muhimu za Serikali na Ulinzi na Usalama.
 
Polisi ndio wanaiharibu hii nchi.
Bila juhudi za makusudi Polisi wanafanya siasa za hatari za kuvuruga nchi.

naona wamechoka na ccm hivyo wanafanya hivyo ili tuichukie ccm zaidi..
 
Kwakweli matendo ya aina hii hayafai, yatasababisha uvunjifu wa amani. Mi naamini kama Mbowe anatakiwa, aitwe kwa taratibu zilizowekwa!

Yeye si gaidi wala jambazi. Anastahili heshima yake. Lakini pia matendo kama haya yakiendelea, tunu ya amani yetu itapotea.

Kwa sasa TZ inao maadui wengi, naomba tuwe makini na matendo ya kutugawa, tusimpe adui fursa ya kupenyeza mamluki kirahisi!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
wewe waache waendelee kutugawa na kujenga chuki kuu dhidi ya polisi, ccm na JWTZ.Fursa ya kupata uhuru kamili wakati mwingine inaweza kutoka nje. kwani waganda walivyo choka kunyanyaswa na IDD AMINI SI WALISHUKURU SANA TANZANI ilipo ingia kuwakomboa na ndio maana vita ile ilikuwa ya muda mfupi sana. ipo siku tutasema sasa baaasi.
 
Tanzania Daima ni gazeti la UDAKU.

Ukweli kidogo na uwongo mwingi.

Hili gazeti ni mwendelezo wa siasa za kilaghai za CHADEMA.
 
sheria za Tanzania zinaruhusu polisi kuua anapojisikia kutiokana na kwamba population ya nchi inaongezeka bila mpangilio
 
Polisi hawana haki ya kumkamata mtu muda wowte wanaopenda. Sheria za kukamata watu ovyo ni za wapindambavu tu waliokosa usataarabu. Polisi wanaowajibu wa kuwakamata wahalifu wote wa sheria za nchi lakini hadi leo hawajamkamata pinda wala mwigulu kwa kauli za kichochezi na za kutishia amani lakini wanabidii ya kuwakamata wanaotaka kuwaonea. Hii ina mwisho pia.
 
Polisi kadhaa wanadaiwa kuvamia nyumbani kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kwa lengo la kumkamata.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mbowe mwenyewe zinaeleza kuwa askari hao waliokuwa na silaha walivamia nyumba hiyo iliyopo eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana wakiwa na silaha.

Mbowe alisema hata hivyo walikwama kumkamata, kwa sababu alikuwa nje ya Dar es Salaam kwa shughuli za chama.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo alikataa kuzungumzia zaidi suala hilo akieleza kuwa anayeweza kulizungumzia zaidi ni Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Camillius Wambura alipoulizwa alisema kuwa hana taarifa za polisi kumtafuta Mbowe.

“Sina taarifa polisi wangu kumtafuta Mbowe,” alisema Wambura.

Lakini Ofisa Habari wa Chadema Tumaini Makene aliliambia Mwananchi Jumapili jana kuwa askari hao walifika nyumbani kwa Mbowe saa 7:16 usiku, wakidai kuwa na hati ya kumkamata Mbowe kutokana na makosa ambayo hata hivyo hawakuyabainisha.

“Ni kweli askari walifika nyumbani kwa Mwenyekiti wakidai walikuwa wakihitaji kumkamata. Kinachotushangaza ni kwamba mtu ambaye anafahamika na wanajua ni mbunge na kiongozi wa chama, lakini wanakwenda kumkamata kama jambazi, usiku wa manane,” alisema Makene.

Alisema kuwa polisi hao walifika nyumbani kwa Mbowe na kukutana na walinzi katika nyumba hiyo, waliowaeleza kuwa mwenyekiti huyo wa Chadema alikuwa safarini.

Makene hakuwataja majina walinzi waliokutwa , lakini nalisisitiza kwamba polisi hao waliacha namba za simu kwa walinzi hao, wakitoa maelezo kuwa pindi Mbowe atakaporejea wamwarifu na kuwapigia polisi kwa kuwa alikuwa akihitajika kituoni.

Ofisa huyo alieleza kuwa wakati wa tukio hilo Mbowe hakuwapo nyumbani na alikuwa safarini mkoani Kilimanjaro, kuhudhuria vikao vya Halmashauri ya Hai.

Makene alisema wanashangazwa na vitendo vya Polisi kusaka viongozi wao usiku wa manane kama majambazi sugu, wakati wakifahamika ni wabunge.

Alisisitiza kwamba skari waliofika wanatoka Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ingawa hakuwataja majina kama alikuwa anawafahamu.

‘‘Tunaelezwa baada ya kumkosa waliacha namba za simu, sasa kama walikuwa wakimhitaji walishindwa nini kumpigia hata katibu wa chama, au yeye mwenyewe na kumweleza kama wanamhitaji polisi?,” alieleza Makene.

Tukio linatokea wakati CHADEMA ikitaka kuanzisha kikosi cha kulinda viongozi wake nchini.


Habari kwa hisani ya Mwananchi.
 
Tanzania siyo kama tuijuavyo.

Polisi wanaenda kumkamata mtuhumiwa, wanafika getini, wanakuta walinzi, walinzi wanawaambia Mh. Mbowe hayupo. Wanaamini maneno ya walinzi na kuacha namba ya simu ili akirudi awapigie simu. Just like that?.

Maswali la msingi:
Kama walifahamu mawasiliano ya simu ni njia mbadala ya kumpata Mh. Mbowe, kwa nini hawakumpigia simu kabla ya kwenda nyumbani kwake?.

Kama walikuwa na nia ya kumkamata, kwa nini waliishia getini badala ya kuingia ndani kama wafanyavyo na ikichukuliwa kuwa walikuwa wamejiandaa na siraha kama ilivyofanyika kwa polisi Arusha wakati wanamtafuta Mh. Lema?.

Kama walikuwa ni polisi, ni kwa nini viongozi wa polisi wanakanusha na kusema hivi,
"Sina taarifa polisi wangu kumtafuta Mbowe," alisema Wambura.
Ina maana kuna vikundi/kikundi kinajifanya ni polisi kwa ajiri ya kufanya uhalifu kwa manufaa ya kisiasa?.

Kikubwa zaidi, matatizo haya yanatokea kwa sababu Tanzania kuna OMBWE la vyombo vya kuangalia usalama wa raia. Kunafikia hatua ambapo kwa sasa inakuwa ni vigumu kutofautisha kazi ya polisi na kazi ya watu wabaya wanaojifanya polisi.

Matukio kama haya yataendelea kutokea na yataongezeka zaidi kadri tunavyoelekea kwenye uchaguzi mkuu kama hakutafanyika UAMUZI mapema wa kuvisuka upya vyombo vya ulinzi nchini.

Is this happening because of Arusha local election?. Jibu wanalifahamu wale "polisi" walioenda "kumkamata" Mh. Mbowe.
 
Tunapungukiwa strategies za kiintelijensia kama nchi, na yaonyesha vyombo vya dola haviwasiliani ipasavyo kitu ambacho ni hatari sana.

Ni vema pia ingebainika the root cause ya kuhitaji kumkamata Mbowe akiwa ni raia mwema wa nchi hii.
 
Back
Top Bottom