Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane

Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane

polisi wa tanzania hawana uhuru kikatiba na wamekua kama honi ya gari hadi wabonyezwe ndio wanalia kwa mantiki hiyo polisi hutumwa na wakuu wao kwenda kufanya ujinga na kwa kua walitumia vyeti feki na wengine walifeli kabisa wanaogopa kukataa kwa kuamini watafukuzwa kazi,TUSITEGEMEE ATA SIKU MOJA JWTZ LIJE LIFANYE KAMA WAMISRI LABDA WANYIMWE POSHO NA MISHAHARA KITU AMBACHO AKIPO.
 
siku hizi huwezi kujua nani polisi nani jambazi, wote wanasare za polis,wote wanavitambulisho vya polisi na wote wanasilaha za moto.
 
Uvamizi mi neno linalotumiwa vibaya na baadhi y wanasiasa uchwarakwa malengo ya FITINA. uvamizi ni lugha inayotumika kuelezea hujuma inafanywa na Jambazi au kikundi chenye lengo la kupora mali ya mtu/Watu. Polisi ni chombo kilicho anzishwa kwa misingi ya kisheria na kina mamlaka ya kukamata, kuhoji, kukagua mtu yeyote anayetiliwa shaka kwa uharifu.

Kuita utekelezaji wa Kazi za kipolisi ni uvamizi huo ni upotoshaji wenye lengo la Kufitini ili kuonewa huruma. inasikitisha chombo cha habari makini kama Mwananchi kinapokubali kupotoshwa na kuripoti habarikwa kutumia Lugha za wanasiasa.
 
Tanzania siyo kama tuijuavyo.

Polisi wanaenda kumkamata mtuhumiwa, wanafika getini, wanakuta walinzi, walinzi wanawaambia Mh. Mbowe hayupo. Wanaamini maneno ya walinzi na kuacha namba ya simu ili akirudi awapigie simu. Just like that?.

Maswali la msingi:
Kama walifahamu mawasiliano ya simu ni njia mbadala ya kumpata Mh. Mbowe, kwa nini hawakumpigia simu kabla ya kwenda nyumbani kwake?.

Kama walikuwa na nia ya kumkamata, kwa nini waliishia getini badala ya kuingia ndani kama wafanyavyo na ikichukuliwa kuwa walikuwa wamejiandaa na siraha kama ilivyofanyika kwa polisi Arusha wakati wanamtafuta Mh. Lema?.

Kama walikuwa ni polisi, ni kwa nini viongozi wa polisi wanakanusha na kusema hivi,

Ina maana kuna vikundi/kikundi kinajifanya ni polisi kwa ajiri ya kufanya uhalifu kwa manufaa ya kisiasa?.

Kikubwa zaidi, matatizo haya yanatokea kwa sababu Tanzania kuna OMBWE la vyombo vya kuangalia usalama wa raia. Kunafikia hatua ambapo kwa sasa inakuwa ni vigumu kutofautisha kazi ya polisi na kazi ya watu wabaya wanaojifanya polisi.

Matukio kama haya yataendelea kutokea na yataongezeka zaidi kadri tunavyoelekea kwenye uchaguzi mkuu kama hakutafanyika UAMUZI mapema wa kuvisuka upya vyombo vya ulinzi nchini.

Is this happening because of Arusha local election?. Jibu wanalifahamu wale "polisi" walioenda "kumkamata" Mh. Mbowe.

Pamoja na kwamba kuna mada nyingine imeanzishwa mapema kabla ya hii, "Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane," napenda kuchangia hii tokana na maelezo yako yenye kuakisi kitu kisicho cha kawaida kinachoendelea kufanywa na vyombo vya usalama wa raia nchini.

Mbunge, kiogozi wa chama cha kisiasa na kiongozi wa kambi ya upinzania bungeni akiwa ni mmoja katika mlolongo wa watumishi wa umma inashangaza hatua za kuvizia usiku nyumbani wakati wana mawasiliano ambayo ni rahisi kumpata katika ofisi za bunge, ofisi za chama, maeneo ya shughuli zake za kibishara, na kama ikibidi afuatwe nyumbani kuna utaratibu wa kufikia local authority yaani uongozi wa serikali ya mtaa anakoishi mhusika bila kuparamia kwa kuruka ngazi zilivyoainishwa kwa taratibu za kisheria.

Kuna kitu kisicho cha kawaida kinachoendelea, lakini pamoja na ushindani wa kisiasa ambao ni wakawaida, yanayoendelea sasa na vyombo vya usalama wa raia huku serikali ikitia lijamu kinywani mwake inatia shaka na pengine kuja kusababisha machafuko makubwa siku si nyingi. Uvumilivu una ukomo wake.
 
JK nchi ilishamshinda zamani sana...ni hatari sana kuongozwa na mtu wa uelewa mdogo kama JK maana nchi inatumbukia kwenye matatizo yeye haoni yuko busy kualika watu kula mafutari ikulu
 
Wasiwasi wangu hawa ni polisi wa kweli kabisa. Walitaka kumchukua na kwenda kumdhuru kisha waseme si wao bali ni wahuni tu. Tukumbuke yaliyompata Dr Ulimboka. Viongozi wa CHADEMA lazima wawe makini mno polisi wanapotaka kuwakamata majumbani mwao usiku wa manane. Kamwe wasikubali kwenda "kituoni" bila wapendwa wao katika familia au viongozi wengine wa juu wa CHADEMA ili kuhakikisha hawaendi kudhuriwa.
 
'eti polisi wanahaki ya kumkamata mtu yyte muda WANAPOPENDA...loooh'

St kayumba znatisha. Nin maana ya kuwa na sheria nchini?
 
Siasa zimeharibu kabisa nguvu kazi ya taifa,watu kila tukiamka asubuhi tunaanza kujadili siasa au wanasiasa,wao wanaingiza siku kwa sababu siasa ndio kazi Yao,umri unakwenda miaka inakwenda tutakuja kustuka wanasiasa wameshakuwa matajiri sisi tumebaki na vilema vya maisha bila msaada wa mtu,
Asubuhi twendeni makazini jamani siasa hizi hizi toka enzi za mwalimu mpaka leo hazijatusaidia,tubadilike sasa
 
Polisi wana haki ya kumkamata mtu muda wowote wanaopenda.

Naona sasa Tanzania haina Polisi bali genge la majambazi. Radhia ulijifunzia wapi u-polisi wako? Kule hakukuwa kumkamata bali kumwingilia kijinai. Hawakuwa na sababu wala hati ya kisheria kufanya vile, na kwa jinsi tunavyoifahamu Polisi yeti siku hizi, inawezekana walienda kummaliza kisha waseme.....hakuna. Polisi aliyekwenda kwa Mbowe usiku labda walikuwa CHADEMA wenzake walioenda kumdhuru! Shame to the Tanzanian Police Force!
 
Wanasiasa kwa media coverage si haba. Ili mradi wawe na kitu cha kurubuni wafuasi wao, mbona ashakamatwa mara nyingi tu na mtu wenyewe mwepesi. Ila shongondo nyingi tu

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Hao ndiyo polisi wetu,let us learn this tutazowea tu ila hofu yangu ni kizazi kinachoyakulia haya matukio
 
Vyombo vya usalama vimegeuka na kua vyombo vya kutumiwa kufanya uhalifu kwa viongozi wa kisiasa ili kukwamisha jitihada zao za ukombozi katika nchi yao. Hii ni hatari na kiashiria kibaya kwa uongozi uliopo madarakani kua umezidiwa sasa umeamua kutumia mabavu kudhibiti kwa njia yoyote ile.
 
Ninachoona kitakachofuata ni polisi kumtaka Mbowe atoe ushahidi wa tukio hilo ama sivyo.... Watamwita afike kituoni na akikataa ataambiwe ajisalimishe mara moja. Watabadilisha kibao tu - mtaona.

Polisi wetu jamani -- wanaanza kutuvunjia amani yetu.
 
hivi na hii movie mnaiamini kabisa wenye akili timamu? watu tusikubali kugeuzwa mazuzu na chadema bwana! Huu ni mwendelezo wa mbinu ya kutafuta uhalali wa kuanzisha terrorism org ya RB, Wajanja shitukeni!
 
Ngoja nikanunue AR zangu mbili na magazine 20 siku nikirudi Bongo wimbo wowote wa polisi na mimi naimba
 
Back
Top Bottom