Mie nasema kweli hapa, watu hao walishakuja kumsachi Bosi wetu ila SIO Usiku ilikuwa mchana. Wana Silaha Na pick up, wakasema Kwa walinzi kwamba tumekuja kumsach Mtu huyu sisi ni polisi Na vitambulisho wakatoa. Kisha wakaingia Ndani wakasach pote Na Watoto walikuwepo. Walinzi wakachukua namba Za gari, kisha wakaitisha cm zote "za gharama" wakasema wanazipeleka kituoni Na laptop mbili.
Walipoondoka bosi wetu kumbe alikuwa nje akawaona Na kunote namba Za gari. Cha kushangaza wakamwachia mlinzi namba ya cm awapigie Bosi akija. Wakaondoka. Nilipopigiwa cm nilitua hapo faster, tukaenda kituo Cha polisi Cha karibu wakasema namba hizo hawazitambui Wala watu hao, tukatumia njia zetu kupata call history ya namba hiyo Na tukafanikiwa, Cha kushangaza inaonekana ni ya Mtu iliyosajiliwa Dodoma, Na Mara nyingi imempigia IGP Mwema. Tukaenda hadi oysterbay Kwa kamanda Kanyela that time akiwa RPC wa Kinondoni, tukakaa nae ofisini Na kumpa vielekezo vyote Kwa Muda sana. Akasema atalishughulikia. Kama kawaida Nchi HII kukosa uwajibikaji kukawa kimya.
Baadae tukasikia walimvamia Mtu mwingine maarufu hotelini ili wamkamate, walinzi wa hoteli wakamficha Na kusema katoka kisha wakawaachia walinzi namba hiyo hiyo. Ukiipiga inaita sana Na kukatika yenyewe.
Kwa upande wetu tuna Hoja 3
1:- AMA mabosi wakubwa Wa Polisi wameunda within respond unit kikosi kingine Cha siri Cha kufanya Kazi zao!! Lakini hoja HII hatuikubali sana Kwa Sababu wasingekuwa wajinga kuacha namba ya cm ambayo mkuu Wa polisi inamwonyesha kwamba naye ni mpiga au mpigiwa.
2:- Ni kikosi Cha ex-polisi wanaofanya uhalifu au ni majambazi yanayojifanya polisi. Hoja hii inaweza kuwa Na nguvu lakini Bado maswali yapo mengi. Ni kweli wanaonyesha vitambulisho vya polisi but hiyo siyo hoja sana siku hizi Mtu anajitengenezea Chochote. Kama ni wahalifu kwanini waache namba Za Cm!?, Na Kama ni majambazi, mzigo wote wa Silaha Na gari Na usumbufu wote ni kwa ajili ya kupora cm Na laptop?!????? Haingii akilini. Na kwanini wafuate watu maarufu wasio Na fedha wakiwaacha matajiri ambao huko wangetoka Na vitita vya fedha. Ni watu wengi maarufu wanetendewa mcheZo huu but Kwa kuwa hawakumdhuru Mtu wala kuiba kitu Chenye samani kubwa wanaamua kuripoti polisi Na kuwa kimya kutoyakuza mambo.
3:- HII ya tatu yaweza kuwa Na nguvu zaidi, yawezekana ndani ya polisi hiyo hiyo wameshaanza kupakana matope au kumpaka matope Mkubwa wao. Inawezekana hao jamaa ni polisi kweli tena Wa quick respond unit (TiGO) , Kama watano hivi but kiongozi wao ndio anaujua mcheZo wengine ni wa kuambiwa tu twende hapa wanaenda. Naamini hivi Kwa Sababu wakifika sehemu wanapack kabisa Na hukaa zaidi ya nusu saa Na hawakurupuki Wala kuonyesha kwamba wana haraka. Wangekuwa Wezi mambo Yao ni faster faster. Wana uhakika Hata mkiita polisi watawakuta wenzao Na watajua wako kazini. Hiyo namba ya cm wanayoacha ndio hasa lengo Lao, wanajua mtaenda polisi Na kuchukua kibali Cha kupatiwa call history Na kugundua he mbona Mzee naye yumo Kwenye list. I think ndio lengo Lao, Na wala SIO namba ya cm ya yeyote within that group.
That's why wameemvamia Chair wa CDM, wakijua jamaa atatambaa na hiyo namba sana Na kuamsha ugomvi Na Mzee Mwema.
Mimi nadhani tabia HII ya polisi kuacha uwajibikaji itagharimu sana ustaarabu Na Amani yetu. Kama tokea that time tumeripoti tukio hili oysterbay wangemtaarifu Mwema hopely hawa watu wangesakwa Na kupatikana. Au Na polisi wanataka tuamini Mwema naye ni miongoni mwa wanaotafuta watu Na kuwaibia cm au laptop?,!?.
Tanzania Ina kiongozi mmoja tu -------- anayetengeneza dili Za kigaidi Kwa kutuma facilitations kwa M-PESA via simu yake halali, sidhani Kama kuna rekodi ya upumbavu mwingine kiasi hiki Tanzania. So hao respond unit AMA ya kweli au kichina wasirichoree Picha Lao la kichina kutuingiza mkenge tusearch users wa hiyo namba. Sijui Kwa Nini polisi Nchi HII imegoma Kufanya Kazi, ukiwaambia fanyeni Kazi wanakusaka wewe uliyewakumbusha wajibu wao, Na kuishia kukamata chokoraa, watu wasio Na Kazi Na kusubiria asubuhi ndugu Na jamaa waje kituoni kuwatoa jamaa zao Kwa kulipia 50,000 hadi laki. Nchi HII ..!?