Polisi: Benki bongo zimeajiri majambazi

Polisi: Benki bongo zimeajiri majambazi

Kama tahira ni wewe kwani wafanyakazi wangapi wa benki wameisha kamatwa kwa kushirikiana na majambazi acha kutetea kitu usichokijua au kwa maslahi yako.
Kama una ushahidi peleka polisi sio kutuhumu watu bila sababu kana kwamba kuchukua pesa benki ni jambo la siri sana
 
MziziMkavu kilio chako hatimaye kimetua kwa mamlaka husika , but nina wasiwasi kama kweli kesi ya mbuzi hakim akiwa fisi haki itatendeka .
View attachment 316339
Baadhi ya benki nchini zinadaiwa kuajiri baadhi ya wafanyakazi walio kwenye mtandao wa majambazi kutokana na wateja wengi kupigwa risasi na kufa wakitoka kuchukua pesa, uchunguzi wa baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi Tanzania umebaini.

Hayo yalisemwa na baadhi ya askari hao wiki iliyopita walipozungumza na mwandishi wetu na kusema kwamba, waajiri wasipokuwa makini katika kuajiri watashangaa kuona wateja wao wanapigwa risasi na kuuawa kila kukicha.

“Haiwezekani kuwa wanaonyang’anywa fedha ni wale wanaotoka kuchukua benki kuliko wanaopeleka! Ina maana wezi wapo katika baadhi ya mabenki hivyo kunatakiwa kuwepo na umakini wakati wa kuwaajiri,” alisema askari mmoja kutoka makao makuu ya jeshi hilo, Dar akiomba hifadhi ya jina lake kwa vile yeye si msemaji.

Afande huyo aliendelea kusema kuwa, baadhi ya wafanyakazi wasio waaminifu wa benki hizo wanapoona mteja anachukua fedha nyingi hufanya mawasiliano kwa njia ya simu kuwaeleza majambazi walio nje namna alivyovaa mteja huyo na kiasi cha fedha alichochukua.

Uchunguzi zaidi unaonesha kuwa, endapo hali hiyo haitadhibitiwa haraka huenda wananchi wakapatwa na hofu ya kuweka fedha zao benki kwa kuogopa kuporwa na kupigwa risasi wakienda kuzichukua.

Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita, lilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, DCP Simon Sirro (pichani) ambapo alikiri kuwepo kwa baadhi ya wafanyakazi wenye mtandao na majambazi huku akisema jeshi lake limeweka mikakati kuhakikisha mtandao huo unasambaratishwa mara moja.

“Ni kweli kwamba, baadhi ya mabenki, si yote, yameajiri baadhi ya wafanyakazi, si wote wenye mtandao na majambazi. Kwa hiyo hata wao ni majambazi tu.

“Sasa tumejipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kukamata pikipiki zinazohusika katika uhalifu. Pia tumeamua kuweka makachero nje na ndani ya mabenki, wapo polisi wa miguu, pikip iki na magari. Nina uhakika tutawadhibiti,” alisema Kamanda Sirro.

Aliendelea kusema kuwa, majambazi waliopo katika Kanda ya Dar es Salaam waanze kufunga virago kwani bila kufanya hivyo wajue watakamatwa wote na mtandao wao kumalizika. Pia aliwataka wamiliki wa mabenki kuwa makini wakati wa kuajiri wafanyakazi ili kuwapata wenye sifa njema na kuweka imani kwa wateja wao.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Suleiman Kova aliwahi kutamka kuwa, baadhi ya wafanyakazi wa ndani wa baadhi ya benki wana ushirikiano na majambazi. Akawatahadharisha wamiliki kuwa makini wakati wa kuajiri.


Chanzo: Gazeti la Uwazi
 
Hivi unafikri kuna mtu anaweza kumpa siri jambazi kwa shilingi milioni kumi ambapo ikijulikana atafukuzwa kazi na kufungwa.
hata laki tano tu wanatoa siri, ndo iwe m10 zote hizo??!!
 
Kama una ushahidi peleka polisi sio kutuhumu watu bila sababu kana kwamba kuchukua pesa benki ni jambo la siri sana
Mbona umelishikia bango sana humu tunajidili kwa njinsi matukio yanavyotekea mfululizo lakini kwa sasa mashine za kuhesabu pesa zilivyowekwe siyo rahisi mtu aliyembali kuona.
Isitoshe matukio ya chamazi na Barclays maafisa wa benki walikamatwa sasa wewe unachopinga nini
 
Mbona umelishikia bango sana humu tunajidili kwa njinsi matukio yanavyotekea mfululizo lakini kwa sasa mashine za kuhesabu pesa zilivyowekwe siyo rahisi mtu aliyembali kuona.
Isitoshe matukio ya chamazi na Barclays maafisa wa benki walikamatwa sasa wewe unachopinga nini
Kwanini mnatuhumu wafanyakazi wa benki tu bila kuangalia upande wa pili
 
Hii statement ni ya kuitilia maanani sana.........Nimeshuhudia watu wengi wanakuja benki kuweka hela kwa mifuko ya rambo ila wanaopigwa risasi wengi ni wanaotoa hela hata milioni tatu tu!
statement rahisi sana,unapowinda lazima uwe na strategy ni wapi unaweza ua. kuanzia fedha zinapotoka ni rahisi kutrack hata kwa jambazi anaejifanya pia ni mteja ndani ya benki. wingi wa wateja katika benki mara nyingine inakuwa vigumu kubaini nani yupo kupata taarifa. Kusema wafanyakazi inaweza kuwa ni sehemu ndogo sana hasa kwa namna wanavyo hudumia maana huwa ni mmoja baada ya mwingine asa huyo muhudumu hadi apige simu na kutoa maelekezo mbele ya mteja mwingine?
 
statement rahisi sana,unapowinda lazima uwe na strategy ni wapi unaweza ua. kuanzia fedha zinapotoka ni rahisi kutrack hata kwa jambazi anaejifanya pia ni mteja ndani ya benki. wingi wa wateja katika benki mara nyingine inakuwa vigumu kubaini nani yupo kupata taarifa. Kusema wafanyakazi inaweza kuwa ni sehemu ndogo sana hasa kwa namna wanavyo hudumia maana huwa ni mmoja baada ya mwingine asa huyo muhudumu hadi apige simu na kutoa maelekezo mbele ya mteja mwingine?
Wafanyakazi wa benki sio teller tu.
 
Kwanini mnatuhumu wafanyakazi wa benki tu bila kuangalia upande wa pili
Wewe utakuwa miongoni mwao na ipo siku utanaswa maana hata kamanda wa kanda maalumu anapozungumzia hilo we bado hutaki itafika wakati utataka tu
 
Sio wafanyakazi wa benki tu,hawa polisi nao si washirika wa majambazi?
 
Wewe utakuwa miongoni mwao na ipo siku utanaswa maana hata kamanda wa kanda maalumu anapozungumzia hilo we bado hutaki itafika wakati utataka tu
Wewe ni mpumbavu sana ina maana kila analolisema kamanda wa polisi ni kweli, hivi uchukuaji Pesa benki ni jambo la siri mbona mtu anachukua pesa wazi.
 
Wewe ni mpumbavu sana ina maana kila analolisema kamanda wa polisi ni kweli, hivi uchukuaji Pesa benki ni jambo la siri mbona mtu anachukua pesa wazi.
Lazima ikuume maana ni mmoja wao we tukuna tu damu huwa haipotei ipo suku na hao walikamatwa kwa kuzima kamera Chanika ni wateja au na wale waliokamatwa Barclays Kinondoni acha kutetea hoja isiyokuwa na mshiko kwa maslahi yako
 
Ilitakiwa mteja akipigwa risasi basi hilo tawi la hiyo benki ambayo mteja ametoka linatakiwa kufungwa kwa muda kupisha uchunguzi wa polisi...

Na wafanyakazi wote wanatakiwa wapelekwe mahabusu hadi wamtaje aliyechonga hilo deal...

Inasikitisha mtu unakuwa mtumwa wa hela zakoo..
kweli ni rahisi sana, unaanza na teller aliyemuhudumia huyo anashtakiwa kwa first degree murder. ikishatikea mara 2 au 3 mchezo utaisha wenyewe.
 
Lazima ikuume maana ni mmoja wao we tukuna tu damu huwa haipotei ipo suku na hao walikamatwa kwa kuzima kamera Chanika ni wateja au na wale waliokamatwa Barclays Kinondoni acha kutetea hoja isiyokuwa na mshiko kwa maslahi yako
Mkiwa na simu zenu majasiri kweli mnatuhumu watu bila ushahidi kwa hiyo mimi ni jambazi? Na kwanini uwatuhumu watu wa benki bila kuangalia upande wa pili wa wateja wengine, ulishawahi kwenda benki kweli.
 
Mnaweza kulaumu wafanyakazi bure kumbe kuna majambazi yanakuwa ndani ya benki yanatoa taarifa kwa wenzao nje yaani siku hizi benki watu wanatumia simu ndani mule.


Kwel kabisa mkuu .bank zenye wateja wengi unakuta mtu anaingia km mteja anazugazuga then anatoa mchongo kwa waarifu
 
View attachment 316339
Baadhi ya benki nchini zinadaiwa kuajiri baadhi ya wafanyakazi walio kwenye mtandao wa majambazi kutokana na wateja wengi kupigwa risasi na kufa wakitoka kuchukua pesa, uchunguzi wa baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi Tanzania umebaini.

Hayo yalisemwa na baadhi ya askari hao wiki iliyopita walipozungumza na mwandishi wetu na kusema kwamba, waajiri wasipokuwa makini katika kuajiri watashangaa kuona wateja wao wanapigwa risasi na kuuawa kila kukicha.

“Haiwezekani kuwa wanaonyang’anywa fedha ni wale wanaotoka kuchukua benki kuliko wanaopeleka! Ina maana wezi wapo katika baadhi ya mabenki hivyo kunatakiwa kuwepo na umakini wakati wa kuwaajiri,” alisema askari mmoja kutoka makao makuu ya jeshi hilo, Dar akiomba hifadhi ya jina lake kwa vile yeye si msemaji.

Afande huyo aliendelea kusema kuwa, baadhi ya wafanyakazi wasio waaminifu wa benki hizo wanapoona mteja anachukua fedha nyingi hufanya mawasiliano kwa njia ya simu kuwaeleza majambazi walio nje namna alivyovaa mteja huyo na kiasi cha fedha alichochukua.

Uchunguzi zaidi unaonesha kuwa, endapo hali hiyo haitadhibitiwa haraka huenda wananchi wakapatwa na hofu ya kuweka fedha zao benki kwa kuogopa kuporwa na kupigwa risasi wakienda kuzichukua.

Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita, lilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, DCP Simon Sirro (pichani) ambapo alikiri kuwepo kwa baadhi ya wafanyakazi wenye mtandao na majambazi huku akisema jeshi lake limeweka mikakati kuhakikisha mtandao huo unasambaratishwa mara moja.

“Ni kweli kwamba, baadhi ya mabenki, si yote, yameajiri baadhi ya wafanyakazi, si wote wenye mtandao na majambazi. Kwa hiyo hata wao ni majambazi tu.

“Sasa tumejipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kukamata pikipiki zinazohusika katika uhalifu. Pia tumeamua kuweka makachero nje na ndani ya mabenki, wapo polisi wa miguu, pikip iki na magari. Nina uhakika tutawadhibiti,” alisema Kamanda Sirro.

Aliendelea kusema kuwa, majambazi waliopo katika Kanda ya Dar es Salaam waanze kufunga virago kwani bila kufanya hivyo wajue watakamatwa wote na mtandao wao kumalizika. Pia aliwataka wamiliki wa mabenki kuwa makini wakati wa kuajiri wafanyakazi ili kuwapata wenye sifa njema na kuweka imani kwa wateja wao.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Suleiman Kova aliwahi kutamka kuwa, baadhi ya wafanyakazi wa ndani wa baadhi ya benki wana ushirikiano na majambazi. Akawatahadharisha wamiliki kuwa makini wakati wa kuajiri.


Chanzo: Gazeti la Uwazi
Labda niulize huyo ulomweka picha ni nani kama askari aliyeongea hautaka hata jina litajwe
 
..ndani ya benki kuna
1..mteja aliyeenda kuweka hela
2..mteja aliyekwenda kutoa hela
3..mfanyakazi wa benki ..(teller)
4..baadhi ya benki kunakua na mlinzi ndani (anasimama au kuzunguka zunguka
Nje ya benki kuna Polisi

kwakua wanaobiwa na kuwawa wanakua walio kwenda kutoa hela,uchunguzi ufanyike zaidi kwa walio ndani
 
Hivi unafikri kuna mtu anaweza kumpa siri jambazi kwa shilingi milioni kumi ambapo ikijulikana atafukuzwa kazi na kufungwa.
uko sahihi, mfumo wa utoaji huduma Ni Mbovu..yani mko benki kama Mko buchani kusubir Mpimiwe nyama..Kuna Wateja wengine wapowapo tu ukimuuliza eti kuna m2 anamsubr! Mi naona tatzo laweza kuwa moja kat ya wateja au walinz wa benk husika!
Teller mda wote yuko biz hyo sim atashka mda gn?..vlevle kama ni sim TCRA si ipo , mbona kuwatrack ni rahisi!!?

Jigo
 
..ndani ya benki kuna
1..mteja aliyeenda kuweka hela
2..mteja aliyekwenda kutoa hela
3..mfanyakazi wa benki ..(teller)
4..baadhi ya benki kunakua na mlinzi ndani (anasimama au kuzunguka zunguka
Nje ya benki kuna Polisi

kwakua wanaobiwa na kuwawa wanakua walio kwenda kutoa hela,uchunguzi ufanyike zaidi kwa walio ndani
namba 5 ongeza wengine hawako kwa kutoa wala kuweka bali wanawasindikiza watu wao benk!!

Jigo
 
Ilitakiwa mteja akipigwa risasi basi hilo tawi la hiyo benki ambayo mteja ametoka linatakiwa kufungwa kwa muda kupisha uchunguzi wa polisi...

Na wafanyakazi wote wanatakiwa wapelekwe mahabusu hadi wamtaje aliyechonga hilo deal...

Inasikitisha mtu unakuwa mtumwa wa hela zakoo..
Swadaktaaa....yaani hapa sina cha kuongeza.
 
Back
Top Bottom