Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 25,485
- 46,309
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemtia mbaroni Tito Onesmo Machibya, maarufu kama “Nabii Tito”, kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo, matusi na uchochezi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi, mtuhumiwa alikamatwa usiku wa Agosti 15, 2026 katika eneo la Sinza Makaburini, wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam.
Polisi wamesema uchunguzi kuhusu tuhuma hizo unaendelea, huku taratibu za kisheria zikikamilishwa ili mtuhumiwa afikishwe katika mamlaka husika kwa hatua zaidi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi, mtuhumiwa alikamatwa usiku wa Agosti 15, 2026 katika eneo la Sinza Makaburini, wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam.
Polisi wamesema uchunguzi kuhusu tuhuma hizo unaendelea, huku taratibu za kisheria zikikamilishwa ili mtuhumiwa afikishwe katika mamlaka husika kwa hatua zaidi.