Polisi: Benki bongo zimeajiri majambazi

Polisi: Benki bongo zimeajiri majambazi

namba 5 ongeza wengine hawako kwa kutoa wala kuweka bali wanawasindikiza watu wao benk!!

Jigo
...Ahsante,na wale wanaoenda kufungua AKAUNTI MPYA ,kuuliza MIKOPO,...polisi wakitumia WELEDI wao wanaweza kuzuia hii KITU
 
HUO UFUKUNYUZI WENU UWAZI NA SHIGONGO UTAWATOKEA PUANI. INAWAHUSU!?, SIKU YAJA. NNA HASIRA NA WEWE ERICK!. TIME WILL TELL...
 
Mi nazani hatua hizi zifanyiwe kazi ili kupunguza au kama si kuzima kabisa mtandao huu!

1:kutoruhusu sim Na Pia kuwe na system ya kuharibu Network ya sim kwa kile aliye na sim ndan ya benk

2:kuwe na kamera nje na ndan ya benk

3:sehem ya kudraw na kudeposit hisiwe ya wazi yaan mtu akitoa au kuweka hela kuwe na kachumba kama ka ATM ni yeye na TELLER wake Tu Au kama unavyoenda kumuona daktari hospitalin

Ni Hayo tu wakuu! Inauma sana hela zako mwenyewe zikukoseshe amani jinsi ya kuzitoa!

Jigo
 
View attachment 316339
Baadhi ya benki nchini zinadaiwa kuajiri baadhi ya wafanyakazi walio kwenye mtandao wa majambazi kutokana na wateja wengi kupigwa risasi na kufa wakitoka kuchukua pesa, uchunguzi wa baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi Tanzania umebaini.Tusiwasahau wale wanaotunza kamera za benki,tunaweza kuwaangalia bankers tu,kumbe kuna wale walinzi wanaohusika na kamera
kumbuka mle ndani ya benki na zinaona na kurekodi kila kitu kinachofanyika,kama kuna jambazi miongoni mwa wanaoshughulika na kamera
huyo ni hatari kuliko hata hao wanaotoa fedha.
nashauri nao waangaliwe kwa jicho la tatu.

Hayo yalisemwa na baadhi ya askari hao wiki iliyopita walipozungumza na mwandishi wetu na kusema kwamba, waajiri wasipokuwa makini katika kuajiri watashangaa kuona wateja wao wanapigwa risasi na kuuawa kila kukicha.

“Haiwezekani kuwa wanaonyang’anywa fedha ni wale wanaotoka kuchukua benki kuliko wanaopeleka! Ina maana wezi wapo katika baadhi ya mabenki hivyo kunatakiwa kuwepo na umakini wakati wa kuwaajiri,” alisema askari mmoja kutoka makao makuu ya jeshi hilo, Dar akiomba hifadhi ya jina lake kwa vile yeye si msemaji.

Afande huyo aliendelea kusema kuwa, baadhi ya wafanyakazi wasio waaminifu wa benki hizo wanapoona mteja anachukua fedha nyingi hufanya mawasiliano kwa njia ya simu kuwaeleza majambazi walio nje namna alivyovaa mteja huyo na kiasi cha fedha alichochukua.

Uchunguzi zaidi unaonesha kuwa, endapo hali hiyo haitadhibitiwa haraka huenda wananchi wakapatwa na hofu ya kuweka fedha zao benki kwa kuogopa kuporwa na kupigwa risasi wakienda kuzichukua.

Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita, lilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, DCP Simon Sirro (pichani) ambapo alikiri kuwepo kwa baadhi ya wafanyakazi wenye mtandao na majambazi huku akisema jeshi lake limeweka mikakati kuhakikisha mtandao huo unasambaratishwa mara moja.

“Ni kweli kwamba, baadhi ya mabenki, si yote, yameajiri baadhi ya wafanyakazi, si wote wenye mtandao na majambazi. Kwa hiyo hata wao ni majambazi tu.

“Sasa tumejipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kukamata pikipiki zinazohusika katika uhalifu. Pia tumeamua kuweka makachero nje na ndani ya mabenki, wapo polisi wa miguu, pikip iki na magari. Nina uhakika tutawadhibiti,” alisema Kamanda Sirro.

Aliendelea kusema kuwa, majambazi waliopo katika Kanda ya Dar es Salaam waanze kufunga virago kwani bila kufanya hivyo wajue watakamatwa wote na mtandao wao kumalizika. Pia aliwataka wamiliki wa mabenki kuwa makini wakati wa kuajiri wafanyakazi ili kuwapata wenye sifa njema na kuweka imani kwa wateja wao.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Suleiman Kova aliwahi kutamka kuwa, baadhi ya wafanyakazi wa ndani wa baadhi ya benki wana ushirikiano na majambazi. Akawatahadharisha wamiliki kuwa makini wakati wa kuajiri.


Chanzo: Gazeti la Uwazi
walinzi wa benki wanaohusika na kamera nao waangaliwe kwa jicho la tatu,hao ni wabaya kuliko hata teller
endapo wameamua kufanya ujambazi,maana kamera zinaona kila mahali ndani ya benki
 
View attachment 316339
Baadhi ya benki nchini zinadaiwa kuajiri baadhi ya wafanyakazi walio kwenye mtandao wa majambazi kutokana na wateja wengi kupigwa risasi na kufa wakitoka kuchukua pesa, uchunguzi wa baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi Tanzania umebaini.

Hayo yalisemwa na baadhi ya askari hao wiki iliyopita walipozungumza na mwandishi wetu na kusema kwamba, waajiri wasipokuwa makini katika kuajiri watashangaa kuona wateja wao wanapigwa risasi na kuuawa kila kukicha.

“Haiwezekani kuwa wanaonyang’anywa fedha ni wale wanaotoka kuchukua benki kuliko wanaopeleka! Ina maana wezi wapo katika baadhi ya mabenki hivyo kunatakiwa kuwepo na umakini wakati wa kuwaajiri,” alisema askari mmoja kutoka makao makuu ya jeshi hilo, Dar akiomba hifadhi ya jina lake kwa vile yeye si msemaji.

Afande huyo aliendelea kusema kuwa, baadhi ya wafanyakazi wasio waaminifu wa benki hizo wanapoona mteja anachukua fedha nyingi hufanya mawasiliano kwa njia ya simu kuwaeleza majambazi walio nje namna alivyovaa mteja huyo na kiasi cha fedha alichochukua.

Uchunguzi zaidi unaonesha kuwa, endapo hali hiyo haitadhibitiwa haraka huenda wananchi wakapatwa na hofu ya kuweka fedha zao benki kwa kuogopa kuporwa na kupigwa risasi wakienda kuzichukua.

Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita, lilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, DCP Simon Sirro (pichani) ambapo alikiri kuwepo kwa baadhi ya wafanyakazi wenye mtandao na majambazi huku akisema jeshi lake limeweka mikakati kuhakikisha mtandao huo unasambaratishwa mara moja.

“Ni kweli kwamba, baadhi ya mabenki, si yote, yameajiri baadhi ya wafanyakazi, si wote wenye mtandao na majambazi. Kwa hiyo hata wao ni majambazi tu.

“Sasa tumejipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kukamata pikipiki zinazohusika katika uhalifu. Pia tumeamua kuweka makachero nje na ndani ya mabenki, wapo polisi wa miguu, pikip iki na magari. Nina uhakika tutawadhibiti,” alisema Kamanda Sirro.

Aliendelea kusema kuwa, majambazi waliopo katika Kanda ya Dar es Salaam waanze kufunga virago kwani bila kufanya hivyo wajue watakamatwa wote na mtandao wao kumalizika. Pia aliwataka wamiliki wa mabenki kuwa makini wakati wa kuajiri wafanyakazi ili kuwapata wenye sifa njema na kuweka imani kwa wateja wao.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Suleiman Kova aliwahi kutamka kuwa, baadhi ya wafanyakazi wa ndani wa baadhi ya benki wana ushirikiano na majambazi. Akawatahadharisha wamiliki kuwa makini wakati wa kuajiri.


Chanzo: Gazeti la Uwazi
Kwa chanzo hicho.. aagh !!!
 
kweli ni rahisi sana, unaanza na teller aliyemuhudumia huyo anashtakiwa kwa first degree murder. ikishatikea mara 2 au 3 mchezo utaisha wenyewe.

Sio teller tu. Inawezekana hata meneja akacheza mchezo.

Au watu wanaokaa kwenye chumba cha CCTV.

Au yule mlinzi au mteja tu anakaa ndani kusoma ramani.
 
Hapa cha msingi ni kumfuata mtu wa mwisho kutoa hela kwa mteja (marehemu). Akipatikana anakamatwa na kuhojiwa kwa kina, lazima atamtaja aliyehusika hata kama ni bosi wake. This is true ni inside job hufanywa na makalani wa benki wenyewe kushirikiana either na mabosi wao pamoja na mapolisi.

Kabisa mkuu.
 
Kuwakamata ni simple tu...likitokea tukio tu, askari waangalie huyo mteja alichukua pesa benki ipi na alihudumiwa na nani hapo benki.

Baada ya hapo huyo banker achunguzwe mawasiliano yake ya simu ya siku hiyo...watajua tu.

MUHIMU: Ipigwe marufuku bankers kutumia simu zao za mkononi muda wa kazi, kada nyingi tu wanazuiwa.

Anaweza akawa mlinzi au meneja au hata mteja mwingine.
 
walinzi wa benki wanaohusika na kamera nao waangaliwe kwa jicho la tatu,hao ni wabaya kuliko hata teller
endapo wameamua kufanya ujambazi,maana kamera zinaona kila mahali ndani ya benki
Hili ndo lakulitolea macho sana
 
Ni ngum matela kuepuka hujuma hii. Kuwanyima wasiwe na simu haisaidii wanachofanya kama unachukua pesa mingi mfano milioni 10 au zaidi wanakupa ela ndogondogo kama elfu mbilimbili au elfu tano tano tupu. Ukitoka pale getini unang'aa na bonge la furushi lazima jamaa 'wakusome'.
Ukiwaambia wakupe ela kubwakubwa kama elfu kumikumi wanakukomalia eti hawana.
 
Gazeti la UWAZI! Habari hii haina ukweli.mtu akitoka benki na mihela raisi kuonekana na mtu aliyenje ya benki anayefanyakazi ya kuvizia wanaotoka na hela benki.huwezi.ukamvamia anayepeleka hela benki hujui atakuja mda gani?atatokea wapi? Wafanyakazi wa benki hawawezi.kushiriki kwenye ujambazi kupora na kuiba millioni.tano,kumi,! mtu.anayefanya mauaji kwa hela ndogo hizo anakuwa hajui.hela zilizochukuliwa benki yeye anajua ni big take tu!
pia utetezi wa polisi ni shallow hawafanyi kazi yao kwa weredi wanatupia lawama mabenki.wao wamejikita.kupiga hela.barabarani.na kuzuia UKAWA.hopeless force.hawaongelea kuhusu umuhimu wa cctv camera maeneo ya mabenki na barabarani wana subiri kuwa reactive badala ya pro active.mbona hawajakamata huo mtandao wa wezi huko kwenye mabenki.kama upo?si waumalize?
 
Back
Top Bottom