Polisi: Benki bongo zimeajiri majambazi

Polisi: Benki bongo zimeajiri majambazi

Ilitakiwa mteja akipigwa risasi basi hilo tawi la hiyo benki ambayo mteja ametoka linatakiwa kufungwa kwa muda kupisha uchunguzi wa polisi...

Na wafanyakazi wote wanatakiwa wapelekwe mahabusu hadi wamtaje aliyechonga hilo deal...

Inasikitisha mtu unakuwa mtumwa wa hela zakoo..
Hujui upelelezi wewe kima bora ukae kimya si kila kitu lazima ufungue domo
 
Namna huduma inavyotolewa nayo inachangia tatizo,unakuta mteja anakaa muda mrefu halafu bank teller anamuita mteja kwa jina!(kimantiki kama kuna mtu mbaya,ataanza kumfuatilia huyo aliyeitwa kwa jina)
Namna nyingine ni kuwa na watu wanaokaa muda mrefu bila kupewa huduma,na wala hawaulizwi wanasubiri nini?!
Shida nyingine askari hawaangalii waingiao,wanaotoka wala kuhoji watu wanaokaa muda mrefu maeneo ya benki bila kupata huduma.
Vile vile unaweza kukuta askari anapiga stori au anasoma gazeti kwenye lindo!
Tatizo lingine,mtu anayechukua pesa nyingi anajulikana maana anaenda room ya Bulk Teller na kila mmoja anaona,hakuna usiri,wateja walio folen wooote wanamuona aidha na begi au fuko la kaki
 
Wakiamua kuwafutilia watakamatwa tu kwani ndani ya bank kila teller huwekewa camera so mi rahisi kuwatrak
 
Ilitakiwa mteja akipigwa risasi basi hilo tawi la hiyo benki ambayo mteja ametoka linatakiwa kufungwa kwa muda kupisha uchunguzi wa polisi...

Na wafanyakazi wote wanatakiwa wapelekwe mahabusu hadi wamtaje aliyechonga hilo deal...

Inasikitisha mtu unakuwa mtumwa wa hela zakoo..



Hapa cha msingi ni kumfuata mtu wa mwisho kutoa hela kwa mteja (marehemu). Akipatikana anakamatwa na kuhojiwa kwa kina, lazima atamtaja aliyehusika hata kama ni bosi wake. This is true ni inside job hufanywa na makalani wa benki wenyewe kushirikiana either na mabosi wao pamoja na mapolisi.
 
Police hawajajipanga kabisa nguvu sana kuriko akili..robery zipo wawe wafanyakazi wa benk au wafanyakazi wa jeshi la police wao jeshi la police wana kikosi gani special cha kukabiliana na majanga kama hayo..Nchi za kusini zambia,zimbabwe,Botswana,Namibia na South Africa wana vikosi kwa ajili ya matukio ya uporaji wa kutumia siraha hao wakikutafuta huwezi ruka..kulikua na uporaji wa barabarani kati ya kapirimposhi na Mkushi miaka mitatu iliyopita wageni ndio walikua wahanga leo hii ni salama labda gari ipinduke kwanza ukikamtwa jambazi hai unapigwa risasi..leo hii vijana wanazunguka na boxer na bunduki wameficha usalama upo wapi..hakuna check point yoyote hata ya kushtukiza na kutumia pia jeshi la wanainchi kama wanavyofanya kwa kaburu na pia kupata ile BMW X 5 yenye Antenna 6 juu ukipishana nao wanajua aina ya bunduki uliyobeba kama imesajiliwa au la dunia imebadilika police badilikeni msiishi mpaka matukio yatokee....
 
Yani ni hatari sana siku hizi ku draw pesa nyingi. Kheri ufanye tranfer au utoa na kumlipa mtu hapo hapo...
 
Kuua tu mimi ndio kinanikwaza
kweli mkuu, hicho hata mimi kinanikera sana!! kwanini wasipore hela tu? maana hela katafuta kwa jasho lake wao wanachukua tu so kupora tu ingetosha, sasa kukatisha na uhai wa mwandamu mwenzio mwenye familia inayomtegemea huwa inaniuma sana!!
 
kweli mkuu, hicho hata mimi kinanikera sana!! kwanini wasipore hela tu? maana hela katafuta kwa jasho lake wao wanachukua tu so kupora tu ingetosha, sasa kukatisha na uhai wa mwandamu mwenzio mwenye familia inayomtegemea huwa inaniuma sana!!
Wanakuwa washachanganyikiwa na tayari damu za marehemu waliopita zinawaandama
 
Wanakuwa washachanganyikiwa na tayari damu za marehemu waliopita zinawaandama
kweli mkuu, damu ya mtu si.ya kawaida, ndo maana ni Mungu pekee aliye na idhini ya kutoa uhai wa mwanadamu aliyemuumba, mwingine ukifanya hivyi ndo hayo uliyosema, lazima uchanganyikiwe tu!
 
Mnaweza kulaumu wafanyakazi bure kumbe kuna majambazi yanakuwa ndani ya benki yanatoa taarifa kwa wenzao nje yaani siku hizi benki watu wanatumia simu ndani mule.
Wewe unaweza kuwa mmoja wao mtu aliye kando anawezaje kujua kiasi kilichochukuliwa na mteja
 
JESHI LA POLICE BADO HALIJAKIZI VIWANGO UNAONA HATA JAMII YA SASA INAONEKA IMEJAA VURUGU BADALA YA USTARABU.POLICE IKIAMUA MIEZI SITA HAKUNA JAMBAZI TZ.
 
JESHI LA POLICE BADO HALIJAKIZI VIWANGO UNAONA HATA JAMII YA SASA INAONEKA IMEJAA VURUGU BADALA YA USTARABU.POLICE IKIAMUA MIEZI SITA HAKUNA JAMBAZI TZ.
Ujambazi ukiisha watakula wapi?
 
Kwa mtazamo wangu,haya matukio ya ujambaz ni kama yameshazoeleka kwa sasa na kama vile sasa polisi na maskio yetu yameyazoea kama.ilivyo ufisadi,ajali za barabaran na vifo vya madereva wa bodaboda au matusi Bungeni.
Jamii imeanza kuzoea sasa,uporaj kwa njia ya pikipiki na inaonekana mamlaka husika zimeshindea kudhibiti hilo
 
Wewe unaweza kuwa mmoja wao mtu aliye kando anawezaje kujua kiasi kilichochukuliwa na mteja
Acha utaahira ndugu yangu majambazi yana mbinu nyingi sana kujua umechukua sh ngapi ni kitu chepesi teller anapohesabu pesa pale kaunta kila mtu anaona kama mtu yupo pale kwa kazi hiyo atajua tu kiasi alichochukua mtu, hawa watu wa benki mnawasingizia bure hakuna mtu anaweza risk kazi yake na kufungwa juu kwa milioni kumi kumbuka sasa simu hazina siri tena.
 
napendekeza pia wafanyakazi wa benki wasitumie simu zao mida ya kazii..maana hili nalo hufanikisha michongo kati ya majambazii na wafanyakazi wa benki
Ni kweli wasiruhusiwe kuwa na simu muda wa kazi, hii itasaidia sana kuvunja mawasiliano yao na majambazi
 
Ni kweli wasiruhusiwe kuwa na simu muda wa kazi, hii itasaidia sana kuvunja mawasiliano yao na majambazi
Hivi unafikri kuna mtu anaweza kumpa siri jambazi kwa shilingi milioni kumi ambapo ikijulikana atafukuzwa kazi na kufungwa.
 
Acha utaahira ndugu yangu majambazi yana mbinu nyingi sana kujua umechukua sh ngapi ni kitu chepesi teller anapohesabu pesa pale kaunta kila mtu anaona kama mtu yupo pale kwa kazi hiyo atajua tu kiasi alichochukua mtu, hawa watu wa benki mnawasingizia bure hakuna mtu anaweza risk kazi yake na kufungwa juu kwa milioni kumi kumbuka sasa simu hazina siri tena.
Kama tahira ni wewe kwani wafanyakazi wangapi wa benki wameisha kamatwa kwa kushirikiana na majambazi acha kutetea kitu usichokijua au kwa maslahi yako.
 
Back
Top Bottom