Pole January Makamba

Pole January Makamba

Kaka nimekulewa. Nadhani ni suala la "methodology" iliyotumika. Wewe unashauri alete maswali na majibu. Upo sahihi. Lakini nadhani mleta mada alikuwa anahofia usalama wake. Manake siku hizi watu wanamwagiana tindikali mchana kweupe.


Wabheja ngalooo
 
Chamviga et al,

Maendeleo ya Bumbuli kwetu siyo issue, suala kubwa hapa ni suala la ukoo wa panya. Tupo hapa tulipo kwa sababu za kipuuzi za kulindana kwa koo za watawala. Sidhani kama itakuwa 2015, and you should join this effort kuakikisha ilo halitokei.
 
mtunzi wa riwaya anapaswa kua makini sana ili wasomaji wake wasijue kua ni hadithi!
 
Kwi kwi kwi kwi kwi kimtu chenyewe kilivyo kama kimebemendwa kisiasa sijui kiburi cha uprsidaaa kamapa nani?
 
kwa kuwa alikua mwandishi wa hotuba za rais, sasa naye anajiona anaweza.
 
Mchungaji nakulize na wwe. ulikula? ulikunywa? ulilazwa? je hiyo 50 ulichukua? naomba nijibu na mimi
 
Chamviga et al,

Maendeleo ya Bumbuli kwetu siyo issue, suala kubwa hapa ni suala la ukoo wa panya. Tupo hapa tulipo kwa sababu za kipuuzi za kulindana kwa koo za watawala. Sidhani kama itakuwa 2015, and you should join this effort kuakikisha ilo halitokei.

Mimi nimemjibu huyu ajitae mchungaji kuhusu hizi propaganda zake. Mimi nimuumini wa mabadiliko lakini si kupitia vyama vya kilaghai na ubabaishaji. Hivi ni vyama hatari zaidi ya chama tawala. Vyama vinavyoshindwa kujiendesha na kusimamia taratibu na kanuni bila bias vitawezaje kuhimili kuliongoza taifa?. Akhsanta.
 
Na wewe uliotoa post hii ni mdini!tena ni mtu hatari sana kwa taifa hili, kwanini usingemuuliza palepale na akupe majibu kisha utume humu? ulilizika kugonganae glssssssss!
 
Huyu sio mtumishi wa bwana,, labda bwana mwingine na si huyu wa majeshi aliye hai,,, umekula pilau,, ukanywa na koka "haramu" na fweza ukabeba,, na kitanda chako cha telemka tukaze ukakisahau,, na choo cha dumbukiza pia ukakipa kisogo japo kwa siku moja,, leo mtumishi baada ya kumnanga palepale kikaoni unatuletea huku kama sio unafiki ni nini kwakweli,, ndo maana nchi haiedelei maana wanafiki mpaka watumishi wa Mungu (sio wote) tumechoka na uzandiki,, kwanza kuwaita nyie watumishi sio kosa,, maana watumishi ni wawakilishi wa makundi ya kijamii kama walivyo wengine!!! msigeuze JF kuwa ukumbi wa taarabu


Kama ulikuwa kwenye hicho kikao si ungemuuliza hayo maswali?kama sio unafiki ni nini..
 
Ndugu wana jf na wa Tanzania kwa ujumla ,leo katika sikukuu hizi za Noel na Mwaka mpya na taka niwapashe yaliyo jili katika jijij la Mwanza .Jana nili bahatika kukutana na January Makamba katika hotel ya Victoria Palace,alitukusanya tulikuwa Wachungaji na Wainjilisti 152 kutoka kakitika madhebu mbalimbali ya kikristo katika mikoa ya Mwanza,Geita,Shinyanga,Mara,na Kagera.Kikao kilianza saa mbili na dakika hamsini na tisa usiku na kumalizika saa tano na dakika ishilini na tatu usiku.Katika kikao hicho January alikuwa amevalia suti yake nyeusi na shati nyeupe ikiambatana na tai nyekundu, kweli kijana ulipendeza kwa vazi hilo cha kunisiki tisha ni pale ulipo anza kujifananisha na nabii Yeremia,nilikusikiliza ukisoma kitabu cha Yeremia moja na kwamba kwa maneno yaliyomo katika kitabu hicho yanakushawishi kutangaza nia ya kugombea uraisi mwaka 2015 vivyo unatuomba sisi watumishi wa Bwana tukuunge mkono na tuwashawishi waumini wetu pia.Ndugu January nikweli unashauku ya kuwa Raisi wa Tanzania lakini naomba nikuulize kupitia waraka huu maswali yafuatayo

1. Watanzania wameshuudia chama chako kupitia wabunge wake mkimzushia mmoja wa viongozi wakuu wa upinzani kwamba alifanya siasa za udini kwa kukutana na watumishi wa Bwana kule Arusha ,sasa hiki ulicho kifanya jana ni Kuharalisha udini au ulikuwa unabadili dini?.

2.Mfuasi wako uliye mtuma kuandaa kikao hicho,Bwana Mustafa kada wa chama cha mabinduzi nikati ya watuhumiwa ,wa mipago hovu ya kuandaa vijana waliyo kwenda na nia ya kudhuru kule Kigoma hivi majuzi sasa nikuulize unapata wapi mamlaka ya kimahadili ya kuandaliwa kikao na mtuhumiwa wa utesi tena kikao na watumishi wa Bwana uoni kwamba unamsanifu Mungu?.

3.Ulitupatia posho ya shillingi elfu hamsini kwa kila mmoja wetu,ulitupatia chakula na vinywaji ,ulitukodishia hoteli, ulitukudishia gari aina ya costa no T926 BDP mali ya bwana Mukeshi ambayo ndiyo ili beba mabaunsa wa Matata kwenda Kigoma hivi majuzi,gharama zote ni takribani millioni ishilini tunashukuru lakini tujiulize,hizo pesa za kutuonga ulipata wapi?,kwanini unataka kununua Uraisi?,Je kwa pesa hiyo unge chonga madawati mangapi kwa ajili ya watoto wanao kaa chini uko Bumbuli? na je unafikili kutuonga sisi utakuwa umewaonga na waumini wetu?.

4.Wewe ni mshilika wa Bwana Rowasa,ambaye pia anakiu ya Uraisi kama wewe lakini pia wewe pia ni mshilika wa Ngeleja ambaye pia kiu ya Uraisi sasa niku ulize tumpigie debe nani kati yenu? ,au mnatafuta kura za sambusa yaani wawili tujitoe mmoja apite?.

5.Umelifanyia nini taifa mpaka uone unaweza kuwania Uraisi,wakati suala la tozo za simu ambalo ni mzigo wa dhambi kwa wananchi,limekushinda ukiwa kama naibu waziri wa wizara usika au una maslahi na makampuni ya mawasiliano,kama sivyo uoni ukiwa Raisi utaleta na kodi ya kusikiliza redio.

6.Unalisemeaje suala la operationi tokomeza ujangili ambayo imetesa na kuuwa wasiyo na atia wakati watuhumiwa wa ujangili akiwemo kinana katibu mkuu wa chama chako bado wana kula bata?.

7'Tuambie nini kimekushawishi kuwa na nia ya kuwa Raisi?.

8.Tuambie nikiongozi ghani wa upinzani unaona anaweza kuwa Raisi kama wewe utopata fursa ya kuwania uraisi?.

9.Kunatetesi kuwa wewe na baba yako mlishiliki kumuondoa Sherukindo kwenye nafasi ya kuwania ubunge jimbo la Bumbulina kukupitisha wewe bila kupingwa kwenye CCM,Sherukindo aliye kuwa mwenyekiti wa kamati yakudumu ya Bunge ya nishati na madini ambaye alisimama kidete juu ya kashfa ya Rich mond iliyo muondoa Rowasa kwenye kiti cha uwaziri mkuu,ambaye ni swahiba mkubwa kabisa wa Mzee Makamba baba yako aliye kuwa katibu mkuu wa CCM?[Comflictof interest] leo ukifanikiwa kuwa raisi si utatengeneza mamlaka ya kifamilia?.

10.Nikumbushe ile divishion four ya formu six kule kigoma uli isafisha lini?.Au na wewe ni muhumini wa division five

11.Niambie leo unawambia nini wa endesha boda boda wa Mwanza au unaomba day waka?.

Mwisho jipime

hayo yote ulimuuliza kwenye kikao hicho?
 
hongera mchungaji kwa kulamba kaposho ka sh 50,000/=!lakini hakuna sababu zozote za kuwashawishi viongozi wa dini kuhubiri siasa tena siasa za kumwagiana tindikali.waacheni viongozi wa dini wahubiri neno la mungu na amani
 
Kama ulikuwa kwenye hicho kikao si ungemuuliza hayo maswali?kama sio unafiki ni nini..

Unawashwa wewe...hujui hata protocol za vikao..tukisema watu waulizane hukohuko magazeti,Jf, Fb, pamoja na wanasiasa, vyombo vyote hivyo vitakuwa na kazi gani? Wachungaji na mashehe nao wamalizane na maandiko matakatifu bila kuonana na waumini wao?Japo sijui jinsi yako lakini nakiri kuchukizwa na mtazamo wako wa kipuuzi..Rudi darasani maana huenda elimu yako ni sawa na ya yule naibu waziri wako wa elimu...
 
Wagombea CCM
1. Edward Lowassa-Ana pesa na watu.
2. Stephen Wassira- Ana watu na ushawishi.
3. January Makamba - Bado mchanga ndo anajitangaza.
4. Bernard Membe-Bado hajaoteshwa anautamani.
5. Emmanuel Nchimbi- Yuko njia panda kwasasa.
6. Fredrick Sumaye-Anajikongoja anautamani
7. William Ngeleja-Msindikizaji.
 
Wakati watu siku ya jana wameitumia kukaa na ndugu na jamaa, wenzetu kumbe mmepanda mabasi kwenda kunywa pombe za bure za mwanasiasa na kupokea posho. Ama kweli njaa kitu kibaya, hivi halafu mtu anapokwita si lazima ujiulize anataka kukwambia nini au wenzetu mlichosikia ni posho tu.

Umeenda, umekunywa na umekula bure, umelipiwa hoteli na ndugu zako umewakimbia kisa umeahidiwa posho were are your morals mtu wamungu, sasa ndio unajiuliza. If you ask me ni umbea tu.
 
Nomaa Sana kateketeza 20m per day!! Kodi zinatumika vibaya!

Siasa inalipa sana Tanzania. Iwapo viongozi wetu wangekuwa na juhudi za kuliendeleza Taifa kama walivyo na juhudi za kutafuta madaraka, nchi hii ingekuwa kisima cha maraha kwani ingekuwa ndiyo "Singapore ya Afrika."
 
Safari hii Ikulu haingiliwi kwa pesa,Watanzani tuweni makini na hao wanaotumia fedha.
Mleta mada anashambuliwa na vibaraka wanaoponea fedha dhalimu za kuwaingiza wenyenazo ikulu.
Hakika hawatashinda na wataishia kutapanya fedha zao na hawata ambulia chochote.Watanzania wameelimika na hawadanganyiki.Mwenye sifa pekee ndie atakaye iingia Ikulu kwa ridhaa ya Watanzania.
 
Back
Top Bottom