Pole January Makamba

Pole January Makamba

Ndio maana nikasema kukata mzizi wa fitina na kukomesha uongo we tuwekee hiyo Sauti na kama una Video itakuwa vizuri zaidi, pia barua ya mwaliko.
Hawezi kuthubutu kuleta hivyo vitu ,January Makamba kupitia baba yake walihakikisha anapita bila kupingwa Bumbuli,kwanza waligawa jimbo ,juzi kuna mwenyekiti kachaguliwa kwa kishindo na kwa kura nyingi akamtisha jamaa akasepa kujiponya ni tapeli la kisiasa
 
bado tuna safari ndefu sana maana sijui hata hayo makosa ya matumizi sahihi ya lugha tatizo ni shule au nini? pia umefanyiwa yooote then unakuja kumuuliza maswali huku si bora ungeomba namba yake ya simu.
 
Tena aeleze kwanini alimwambia Pinda kuwa kiwanda cha chai - Bumbuli hakiwezi kufanya kazi hata angekuja rais? kwanini anadhani akianzisha yeye ushirika wa wakulima wa chai utafaa kuliko ule ulioanzisha na baba pamela (makai) aka shelukindo?
Kwanini halmashauri mpya ya bumbuli inaitwa halmashauri ya wilaya wakati hakuna wilaya inaitwa bumbuli?
MKAMA6 i-join kwenye thread pale juu
 
Last edited by a moderator:
Natamani Kambarage angekuweko upuuzi kama huu wa kuhonga mapesa kwa wajumbe,ili aje kuwa Raisi angemuuliza wee mtoto umeyatoa wapi haya mapesa ya kuhonga....????
Bahati mbaya kabisa kwa sasa 'Nyumba Haina Msimamizi'watoto wanafanya lolote walitakalo.....loooooooooohhhh,kweli ni janga la Kitaifa.
 
Hivi mtu mlikiwa nae masaa yote pale kwanini haya maswala usimuulize pale pale nadhani angekupa majibu stahiki,sasa umeyaleta hapa kutaka kumdhalilisha au kutaka nini? Sijaelewa nia yakuleta haya hapa
NIA ni moja na kubwa: Operesheni Fichua Ouzo! tutawatafuta, tutawaibua na kuwaripoti.
 
Hivi mtu mlikiwa nae masaa yote pale kwanini haya maswala usimuulize pale pale nadhani angekupa majibu stahiki,sasa umeyaleta hapa kutaka kumdhalilisha au kutaka nini? Sijaelewa nia yakuleta haya hapa
JF ni mahali ambapo we dare talk openly. Nafurahi mwanzisha uzi kuleta uzi huu hapa ili na sisi ambao hatukuwepo pale Mwanza tuweze kujua yaliyojiri. Siwalewi ninyi ambao mlitaka maswali haya yaulizwe kimya kimya
 
Wamarekani wanataka Makamba Jr awe Rais, wanaamini chini ya Makamba Jr Masilahi yao yatakuwa salama...Fedha za kumuwezesha tayari zipo...
Wamarekani as a government hawatoagi hela kwa kampeni za viongozi wa mataifa ya nje. Unless amepewa hela na CIA.
 
Haya ni yaleyale.50 umechukua, hotel, chakula, usafiri umeshiriki na kukaa na January akaeleza yake ukasikiliza na hukumuuluza maswali.umemaliza 50 maswali unakuja uliza kwenye Jf wengine hata 10 hatujaona.wewe koma bana hukohuko.
 
bado tuna safari ndefu sana maana sijui hata hayo makosa ya matumizi sahihi ya lugha tatizo ni shule au nini? pia umefanyiwa yooote then unakuja kumuuliza maswali huku si bora ungeomba namba yake ya simu.

Mleta mada amefanya vizuri kuleta hii habari public... Angempigia simu yangeishia hukohuko na tusingepata fursa ya kujadili uovu was matumizi ya viongozi was dini kwenye siasa
 
Haya ni yaleyale.50 umechukua, hotel, chakula, usafiri umeshiriki na kukaa na January akaeleza yake ukasikiliza na hukumuuluza maswali.umemaliza 50 maswali unakuja uliza kwenye Jf wengine hata 10 hatujaona.wewe koma bana hukohuko.

Acha upuuzi we we kiazi... Pesa zao ziliwe... Na kuwalipua walipuliwe


Tusitetee divisive means
 
Mimi nimemjibu huyu ajitae mchungaji kuhusu hizi propaganda zake. Mimi nimuumini wa mabadiliko lakini si kupitia vyama vya kilaghai na ubabaishaji. Hivi ni vyama hatari zaidi ya chama tawala. Vyama vinavyoshindwa kujiendesha na kusimamia taratibu na kanuni bila bias vitawezaje kuhimili kuliongoza taifa?. Akhsanta.
Tunakujua sana kwa mabandiko yako humu. Unaendeshwa pia na itikati ileee!
 
Na wewe uliotoa post hii ni mdini!tena ni mtu hatari sana kwa taifa hili, kwanini usingemuuliza palepale na akupe majibu kisha utume humu? ulilizika kugonganae glssssssss!

sio lazima umpangie namna ya yeye kuhandle situation dhalimu kama hii

amefanya vyema kuileta hadharani kila mtu ajue kinachoendelea
 
Huyo mwandishi wa thread!!! Full kuchanganya R na L, maana hadi kichwa kinauma(ROWASA-LOWASA)
Mleta Uzi ni mnafiki Fulani tu, si mlikuwa nae huyo January makamba kwa nini usumulize Huko huko, Leo unaleta maswali kwenye forum
 
Huyo mwandishi wa thread!!! Full kuchanganya R na L, maana hadi kichwa kinauma(ROWASA-LOWASA)
Mleta Uzi ni mnafiki Fulani tu, si mlikuwa nae huyo January makamba kwa nini usumulize Huko huko, Leo unaleta maswali kwenye forum
ujumbe umefika kwa jamii... kukosea R na L ni janga la kitaifa, lakini kamwe usitake tuhamie huko na kusahau hoja ya msingi ya kijana January kupitia milango ya nyuma
 
Back
Top Bottom