Pinda: Wanaopinga kodi ya simu hawana jema

Pinda: Wanaopinga kodi ya simu hawana jema

Ni jambo la kushangaza sana January kulalamika kwenye vyombo vya habari. Unafiki tu

Kama kweli Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mnatafuta fedha kwa ajiri ya kuongeza mapato ya kuwa wezesha kusambaza umeme vijijini nashauri serikali iache ubaguzi wa kimatabaka kati kodi ya PAYE.... Wa heshimiwa wabunge wote na baraza lote la Mawaziri nao walipe PAYE kama tunavyo lipa sisi wafanyakazi hohe hahe. Pia walipe withholding tax ( asilimia 15%) kwa allowances zao. Mathalani wabunge wanapokea mshahara wa zaidi ya sh 11,000,000/=. Kila mbunge atachangia sh 3,189,700/= na tufanye bunge letu lina wabunge 345... serikali itakusanya sh 1,100,446,500/= au kwa urahisi ni bilioni 1.1. hiki ni chanzo kabla ya kuhusisha baraza la mawaziri[/QUOTE]

Thubutu!! Mwenye nacho anaongezewa
 
hiyo sio hela ya kampeni ya 2015 inatafutwa? wajanja sana hawa watu, wanaanzia mbaliiiiii
 
HAWA JAMAA NI WATU WA AJABU SANA, WAMEANDIKA KICHWA CHA HABARI kwa malengo ya kushusha hadhi lakini wakasahau kwamba ccm nao walitoa kauli ya kupinga, baada ya mjadala wamekimbilia kutoa hiyo HEADING kwenye mtandao wao, lakini UJINGA ni mzigo wakajisahau kwamba GAZETI liko mtaani na watu wameshachukuwa picha zake, matokea yake ni kwamba hii habari sasa inavichwa viwili vya habari

LINAVYOONEKA SASA KWENYE MTANDAO WAO KWENYE HABARI HIYO NI HIVI
Screen Shot 2013-07-22 at 11.13.29 AM.png Screen Shot 2013-07-22 at 11.13.29 AM.png

HABARI YA MWANZO NA AMBAYO HIKO KWENYE HARD COPY NI HIVI


DSC_0050_dc090.jpg
 
Nimegundua: Huyu mzee anaongea chochote kinachomjia kinywani kwake hakuna uratibu kati ya ubongo na mdomo. Kwa nini hakuona kama ni vema akaongeza hiyo 1000 kwa kila gram au kilo ya madini yoyote au kwa kila mtalii anaeingia nchini? Watanzania wanatakiwa wajue pia kuwa hawana watetezi katika watawala tulionao.
 
hivi madini aina zote pekee na gesi tulivyonavyo tukivitumia kisawasawa kweli hatuwezi kufikia malengo ??
hivi mpaka tuwakamue masikini na kwenye simu tena?

mie napendekeza heri tukarudi kwenye kodi ya kichwa kama zamani hata kama itakuwa 20000 lakini bora ieleweke kwa mwaka mie nachangia kiasi gani vinginevyo hapa tunawasaidia watu kuishi huku sie tukibaki hoehae ..hapana tumenyonywa kupindukia.
 
Hela ya simu ukaendeleze umeme? Hivi huyu baba alisoma wapi?
 
Hapo ndo siwaelewi CCM kabisaaaa... hebu cheki
1. Makamba anadai alizidiwa nguvu mpaka tozo ya line ya simu ikaingia bungeni...
2. Wabunge wa CCM wasema NDIYOOOOOOO ipite, na ikapita....
3. Ilipoanza kulalamikiwa, NAPE akaema CCM inapinga uwepo wa tozo hiyo......
4. Makamba akarudi kwa Mnyika na mkumwambia aache unafiki wa mitandanoni.... na akaonyesha kama vile tozo hii itasitishwa...
5. Pinda naye anakuja na maneno yanayoonyesha kuwa tozo hiyo ipo na itatozwa kama kawaida

MASWALI...
1. Hivi, kwa nini Pinda, Makamba na Nape hawana kauli moja juu ya hili...??
2. Aliyemfanya Makamba ashindwe wakati anapinga tozo hii hadi ikaingia bungeni... NI PINDA..???
3. Hawana vikao vya kiserikali ili kutoa kauli moja..???
4. Nani msemaji wa jambo hili..??? Kwamba akitoa taarifa yeye ndo tuiamini..??

mkuu kwa hili andiko lako WEWE NI BINADAMU AU NI MTU.
 
Huyu babu sasa naona anazeeka vibaya maana amekuwa akibwabwaja hovyo as days goes by, like i always say this government has poor communication channels na uongo wanao utumua kila siku ndio utakao waumbua wenyewe ni majuzi waziri kanukuliwa akisema hivi katika moja ya midahalo yao.

SERIKALI imeweka wazi miradi ya umeme ya kipaumbele, itakayotoa matokeo ya haraka ifikapo 2015/2016, na kunufaisha wananchi katika mikoa 13 nchini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisema hayo jana mbele ya wadau waliokusanyika katika mkutano wa siku moja wa kukusanya maoni kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo. Alisema wizara hiyo imedhamiria kuhakikisha miradi hiyo kwa kipindi hicho, inaleta matokeo muafaka yatakayoonekana wazi kwa Watanzania wote.

Kuhusu umeme vijijini, Muhongo alisema kupitia mpango wao walioainisha wa umeme vijijini, watahakikisha kila mwaka kwenye kila mkoa, vijiji kadhaa vitakavyobainishwa kulingana na idadi ya watu wake, vitapatiwa umeme na tayari Sh bilioni 330 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Kuna kipindi niliona jamaa alikuwa anaropka mpaka basi mbele ya wawekezaji, bosi wake ikabidi aingilie kati and this is what he had to say "gentlemen i assure you Peter Griffin is not being paid for ideas in this organisation".

Ndio Pinda kiongozi gani wajuu asiejua what is subordinates are saying regarding the same issues, poor liaison and coordination within.
 
Waziri mkuu Mizengo Pinda amesema tozo hiyo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini.

Alisema hayo alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Songea juzi, katika ziara yake ya wiki moja mkoani Ruvuma.
Pinda '' ni kama vile tozo iliyoongezwa kwenye mafuta ya petrol, ambayo imetupa fedha nyingi katika mfuko wa barabara, za kuunganisha miji na mikoa''.

Aliongeza '' Nani asiyetaka vijiji vipate umeme kama miji, ili usaidie kuondoa giza, uendeshe viwanda vidogo vidogo na usaidie kukuza uchumi? Wanaopinga tozo hii, hawatutakii mema'' alisema Pinda.

source: Habari leo

Ataaminikaje wakati ni MWONGO?
 
Huyu mtoto wa mkulima sasa hivi naona amekuwa mtoto wa fisadi. Juzijuzi wametangaza kuanza kupeleka umeme nje ya nchi na reli kupeleka nchini kongo drc ila umeme wa kwenda vijijini inabid tuuchangie 1000. Halaf hajatueleza marundo ya kodi tunayolipa yanakwenda wapi
 
Hii kitu wakiendelea kuikomalia yaweza kuwa kaburi lao zuri sana 2015, hiyo kitu ina athari ya moja kwa moja hadi kwa kwa wale wazee kule vijijini ambao ni mtaji wao mkubwa.
 
Hapo ndo siwaelewi CCM kabisaaaa... hebu cheki
1. Makamba anadai alizidiwa nguvu mpaka tozo ya line ya simu ikaingia bungeni...
2. Wabunge wa CCM wasema NDIYOOOOOOO ipite, na ikapita....
3. Ilipoanza kulalamikiwa, NAPE akaema CCM inapinga uwepo wa tozo hiyo......
4. Makamba akarudi kwa Mnyika na mkumwambia aache unafiki wa mitandanoni.... na akaonyesha kama vile tozo hii itasitishwa...
5. Pinda naye anakuja na maneno yanayoonyesha kuwa tozo hiyo ipo na itatozwa kama kawaida


MASWALI...
1. Hivi, kwa nini Pinda, Makamba na Nape hawana kauli moja juu ya hili...??
2. Aliyemfanya Makamba ashindwe wakati anapinga tozo hii hadi ikaingia bungeni... NI PINDA..???
3. Hawana vikao vya kiserikali ili kutoa kauli moja..???
4. Nani msemaji wa jambo hili..??? Kwamba akitoa taarifa yeye ndo tuiamini..??
hao ndio wanasiasa,,,tufanye yetu wao wala haiwahusu hii na hitawakwaza
 
Hapo ndo siwaelewi CCM kabisaaaa... hebu cheki
1. Makamba anadai alizidiwa nguvu mpaka tozo ya line ya simu ikaingia bungeni...
2. Wabunge wa CCM wasema NDIYOOOOOOO ipite, na ikapita....
3. Ilipoanza kulalamikiwa, NAPE akaema CCM inapinga uwepo wa tozo hiyo......
4. Makamba akarudi kwa Mnyika na mkumwambia aache unafiki wa mitandanoni.... na akaonyesha kama vile tozo hii itasitishwa...
5. Pinda naye anakuja na maneno yanayoonyesha kuwa tozo hiyo ipo na itatozwa kama kawaida

MASWALI...
1. Hivi, kwa nini Pinda, Makamba na Nape hawana kauli moja juu ya hili...??
2. Aliyemfanya Makamba ashindwe wakati anapinga tozo hii hadi ikaingia bungeni... NI PINDA..???
3. Hawana vikao vya kiserikali ili kutoa kauli moja..???
4. Nani msemaji wa jambo hili..??? Kwamba akitoa taarifa yeye ndo tuiamini..??
[MENTION][JFMP3][/JFMP3][/MENTION]

Hahaha sisim sasahivi kila mtu anaongea kivyake imekuwa kama mnara wa babeli ulivyoanguka, hiyo niishara mbaya.
 
swali langu ni moja tu, kwanini yasikabwe makampuni ya hiyo mitandao wanakabwa wananchi? hii kwa lugha nyingine ni kwamba, tusitumie mitando yote, yaani uchague kutumia mtandao mmojawapo tu kwa kuwa kadiri unavyokuwa na mitandao ndivyo unavyozidi kuumia na tozo hiyo
 
Hii kitu wakiendelea kuikomalia yaweza kuwa kaburi lao zuri sana 2015, hiyo kitu ina athari ya moja kwa moja hadi kwa kwa wale wazee kule vijijini ambao ni mtaji wao mkubwa.
usijidanganye mdau,unajua fulana za 2010 na khanga pamoja na kofia vimeisha,watavipokea 2015 na watawarudisha ccm
 
Kama Waziri Mkuu ameridhika na kodi hii mpaka kufika mahali anakuwa mtetezi wake basi huyu si mwenzetu tena!
Sielewi kwa nini alifika mahali akajinasibu na sisi watu wa hali ya chini kwa kujiita mtoto wa mkulima. Sawa, nikubaliane naye kuwa ni matoto wa mkulima kiuhalisia lakini moyoni mwake siyo!
Kwa nini Waziri Mkuu anatetea kodi isoyojua usawa? Waziri Mkuu hajui usawa? Kwa nini anayetumia Tsh 100,000/= kwa mwezi alipe kodi sawa na anayetumia Tsh 2,000/=kwa mwezi? Inawezekana Waziri Mkuu hanunui vocha kwa kuwa simu yake ina air time ambayo tunailipia sisi wavuja jasho.
Njia za kupata hiyo kodi toka eneo hilohilo la mawasiliano zilikuwa zimekwisha?
Kama kampuni za simu zimeweza kuiba umeme wa TANESCO, Waziri Mkuu atuambie zimekwepa kulipa kodi halali ya kiasi gani? Je zinatorosha kiasi gani na kuhifadhi kwenye Tax Havens? Je ungekuwapo usimamizi makini wa ulipaji kodi kwenye Makampuni ya simu tungelipa hii kodi?
Kwa nini Serikali Mh Waziri Mkuu inasuasua kufunga mtambo utakaodhibiti mapato ya Kampuni za Simu ili zilipe kodi halali?
Ni kuwadanganya Wananchi wa Vijiji vilivyoko Ruvuma kuwa kodi hiyo itawapelekea Umeme. Je kodi hii ikifutwa Atakwenda Ruvuma na kuwaeleza watu wale kuwa hatukuwaletea umeme kwa sababu kodi ya kadi za simu ilifutwa?
Nitalipa kodi ya kadi zangu za simu kwa moyo mmoja kama Waziri mkuu ataniondolea mashaka kwa kujibu maswali yangu machache hapo juu. Naufahamu vema wajibu wangu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa langu.
 
Back
Top Bottom