Pinda aonya malumbano ndani ya CCM

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amewashangaa viongozi waandamizi wastaafu serikalini na CCM kuacha kuzungumzia malalamiko yao katika vikao halali kabla ya kukimbilia kwenye vyombo vya habari. “Vyama vina mifumo yao ya kuendesha shughuli zao … vina maeneo ya kusemea mambo yao na huko ndiko kusaidia chama na kuweka mikakati ya kukiendeleza,” alisema Waziri Mkuu alipozungumza na wahariri wa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam jana.

Alikuwa akijibu swali kuhusu viongozi wa CCM wakiwamo wastaafu, kulumbana na umoja wa vijana wa chama hicho hadharani badala ya kutumia vikao halali vilivyopo. Alisema kutoa madukuduku kwa kutumia magazeti kabla hata ya kukataliwa katika vikao halali vilivyopo, si dhamira nzuri. “Kama malalamiko yako uliyatolea katika vikao halali na ukakataliwa kusikilizwa na hivyo ukaamua kutoka na kuyasema nje, hilo halina tatizo. “Na hasa viongozi wastaafu. Hawa wana fursa ya ziada, wana uhuru hata wa kumwona Rais na kusema naye, wakitumia uzoefu walionao kumsaidia hata yeye,” alisema Pinda.

Aliasa kuwa si picha nzuri kuona kana kwamba viongozi hao wanakataliwa kusikilizwa katika vikao na hivyo kuamua kuyasema hadharani. ”Msiwe waoga kusema ndani ya vikao halali kwani huko ndiko hasa pa kujenga na si kusemea kwingine … huko ndiko kukisaidia chama na kupanga mikakati zaidi ya kukiimarisha,” alishauri Pinda.

HabariLeo

hakulia?
 
Angekuwa anacharuka namna hii anapoongea dhidi ya ufisadi uliokithiri nchini, basi ufisadi ungeshakuwa history katika nchi yetu.


03_11_53mswc.jpg

THE Prime Minister, Mr Mizengo Pinda, stresses a point during a meeting with editors in Dar es Salaam on Monday. (Photo by Fadhili Akida)
 
Ingekuwa busara zaidi kabla ya kuongea hayo angewakemea hao watoto wanaopita mitaani wakiongea ovyo na kuwatukana wakubwa wao. Ama yeye Pinda anaona ni sawa hao watoto walivyokuwa wanabwata ovyo!!!
 
hapa tunajadili watu au issues? hata kama mtu humpendi jaribu kusikiliza hoja yake.
 
hapa tunajadili watu au issues? hata kama mtu humpendi jaribu kusikiliza hoja yake.

hana hoja ni utumbo mtupu....

shida yake ni kukosa nguvu ya kisiasa(msingi katika chama) ndiyo sababu anaishia kubwata hovyo..hata majina anaogopa kuyataja

kilimo kwanza...EPA...Meremeta....Richmond kutaja vichache tu vimemshinda ataweza kupambana na Sumaye, Lowasa...anacheza.

maneno yake yatapotelea hewani kama vile vumbi linavyopeperushwa na upepo:juggle:
 
hapa tunajadili watu au issues? hata kama mtu humpendi jaribu kusikiliza hoja yake.
hana hoja na hajaanza leo kushangaa na kulialia

kama mtu anashangaa watu wana nyumba za tope kagera wakati ameacha tope lukuki rukwa unadhani ni wa kutiliwa maanani kweli?

ladba tumshangae yeye kwanini hakulia tena
 
Mh Pinda hapa ana jicontradict. Mbona yeye haya kaya tamka mbele ya vyombo vya habari na si kwenye vikao vya chama? Au na yeye ana ogopa kuwaambia hayo uso kwa uso?
 
ameshiba sasa anajamba hovyo sijawahi kutegemea ushuzi kama huu toka kwa mtu mwenye cheo cha PM anachekelea wenzake wanavyosulubiwa na watoto hawa waliokosa adabu ngoja ya kwake na ya afya yake yatakapokuja mbeleni shenzi kabisa huyu bwana hana qualifications za kuwa PM wangu
 
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amewashangaa viongozi waandamizi wastaafu serikalini na CCM kuacha kuzungumzia malalamiko yao katika vikao halali kabla ya kukimbilia kwenye vyombo vya habari. "Vyama vina mifumo yao ya kuendesha shughuli zao … vina maeneo ya kusemea mambo yao na huko ndiko kusaidia chama na kuweka mikakati ya kukiendeleza," alisema Waziri Mkuu alipozungumza na wahariri wa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam jana.

Alikuwa akijibu swali kuhusu viongozi wa CCM wakiwamo wastaafu, kulumbana na umoja wa vijana wa chama hicho hadharani badala ya kutumia vikao halali vilivyopo. Alisema kutoa madukuduku kwa kutumia magazeti kabla hata ya kukataliwa katika vikao halali vilivyopo, si dhamira nzuri. "Kama malalamiko yako uliyatolea katika vikao halali na ukakataliwa kusikilizwa na hivyo ukaamua kutoka na kuyasema nje, hilo halina tatizo. "Na hasa viongozi wastaafu. Hawa wana fursa ya ziada, wana uhuru hata wa kumwona Rais na kusema naye, wakitumia uzoefu walionao kumsaidia hata yeye," alisema Pinda.

Aliasa kuwa si picha nzuri kuona kana kwamba viongozi hao wanakataliwa kusikilizwa katika vikao na hivyo kuamua kuyasema hadharani. "Msiwe waoga kusema ndani ya vikao halali kwani huko ndiko hasa pa kujenga na si kusemea kwingine … huko ndiko kukisaidia chama na kupanga mikakati zaidi ya kukiimarisha," alishauri Pinda.

HabariLeo

Pakitokea milimbano yenu mnataka kuitana vyumbani muhongane na kumaliza kwa kupeana deals, hivi Pinda uchoki kuwanyonga watanzania na sera zenu za wizi? Dhamira ni kitu gani na democracy na transparency vina maana gani kwako? Pinda usitupotezee muda.

Watanzani tunajua lugha ya kizarendo na lugha ya kifisadi. We have seen all.​
 
hapa tunajadili watu au issues? hata kama mtu humpendi jaribu kusikiliza hoja yake.

hivi pinda nae ni Rastafarian ......

get up stand up.... stand up for your right ....... Robert Marley (Bob)
 
Angekuwa anacharuka namna hii anapoongea dhidi ya ufisadi uliokithiri nchini, basi ufisadi ungeshakuwa history katika nchi yetu.


03_11_53mswc.jpg

THE Prime Minister, Mr Mizengo Pinda, stresses a point during a meeting with editors in Dar es Salaam on Monday. (Photo by Fadhili Akida)

Pinda == Vuvuzela ya mafisadi, hana mawazo original.
 
Sasa Pinda ungependa wao waongelee vikaoni si nawe usubiri ili ukaongelee hayo huko huko kwenye vikao vyenu vya CCM wakati unaangaliana macho kwa macho na Sitta pamoja na Sumaye. Ukiongea wakiwapo na watakupatia mawazo yao moja kwa moja.

Pinda unatupa picha kua wewe ni mwoga na migizaji tu. CCM wote mnaogopana kweli kweli matokeo yake kila mtu yuko vyake vyake na maigizo.
 
Kama kawaida yake Pinda! He's acting as a shock absorber of the gvt and part. Whenever there is hot issue inayowaumiza vichwa viongozi, yeye ndiye anakuja kupoza! Amesahau kuwa ukishapoteza mwelekeo/dira, taratibu haziwezi kufuata tena maana mnakuwa mmepagawa na kila m1 anatafuta pakujishika! Poor Pinda. Hata yeye hakuufuata utaratibu anaotaka ufuatwe! Usikute tu Shigela amesikia maana hakawii kumjibu na comedy ikaendelea!
 
Hivi huyu Pinda huko UWT alipokuwa kabla ya kuingia TAMISEMI alikuwa na Cheo gani?.....mbona analialia sana..halafu mlalamishi sana...KWANI YEYE KWANINI ALIROPOKA MAJUKWAANI ALIVYOKWENDA CHATO..NA ASIMWELEKEZE WAZIRI MWENZAKE MH MAGUFULI KWENYE VIKAO VYA BARAZA LA MAWAZIRI?AU KWA HILO HAJUI KWAMBA KUNA SEHEMU ZA KUONGELEA MAMBO KAMA HAYO?
HUYU SASA ANATUMIWA KAMA BIG G.
 
kwa mara ya kwanza nimeona Pinda akitoa msimamo wa kukemea kundi mmoja, siku zote huwa anaogopa kuelemea kundi lolote but safari hii kawabeza wenzake wakati anye ni mstaafu ajae!
Pinda ni mnafiki mkubwa kuliko kiongozi yeyote nchii coz daima huwa hataki kuudhi kundi lolote na hivyo kupelekea kuokuwa na msimamo dhabiti na ndio chanzo cha mambo mengi kuyumba nchini
 
Nijuavyo wanaoongea sirini ni Wachawi na Wanga kwa lengo la kumdhuru mtu na kula nyama za victim wao, au kupanga kuwa tumesha mla mtoto wa fulani, sasa ni zamu ya fulani naye alete mwanae tumle!
Huwa hawana ujasiri wa kubainisha shughuli zao hadharani.
Mnataka kumla nani safari hii?
 
Unajua Pinda anapenda kuonekana Goodboy...mnafiki tu.Pinda ni mfano mbaya wa viongozi wa kizazai kilichopo madarakani,yeye ni muumini mkubwa wa siasa za kizandiki za CCM.Kazi anayo
Huyu bwana ni mnafiki ajabu!!!,ukiangalia kauli yake na matendo yake ni mwongo wa kufa mtu,hata maoni aliyoyatoa jana kwa kuwasema wastaafu naamini hakutakiwa kuyatoa zaidi ya kujibu kuwa yatazungumzwa kwenye vikao,au yeye ni tofauti!?,mfano angalia suala la magufuli kwa jinsi alivyoropoka jukwaani ni maajabu!kwani kikao cha baraza la mawaziri hakikuwepo?au yeye mwenyewe kwa nafasi yake anauwezo wa kumwita waziri yeyote na kumshauri,mbona hakufanya hivyo?hata kama alifanya hivyo hakusikilizwa na yeye kuamua kulipuka basi hana hekima,kuna njia nyingi tu za kistaarabu za kumshauri mtu,ukifatilia kwa makini pinda amechangia kwa kiasi kikubwa serikali kukosa mwelekeo kwani yeye ndiyo mtendaji wa serikali,siyo kwamba namtetea lowasa ila baada ya yeye (lowasa) kuondoka mambo yameenda hovyo zaidi,kazi yake kutaka kufurahisha kila upande,amekuwa mtu wa kulalamika na kuishi kwa kudhani!
 
Back
Top Bottom