Pigo takatifu dhidi ya Chadema muda huu

Pigo takatifu dhidi ya Chadema muda huu

Halafu wewe Magonjwa mtambuka mbona una ujinga sana kichwani? Hivi isingekuwa upinzani hii jitihada ya serikali angalau kuwajibika kwa wananchi ingekuwepo? Mnaoombea upinzani ufutike nadhani kichwani mwenu mmejaza makamasi tu. Bila upinzani hata hii hapa kazi tu isingekuwepo.
Vizuri unaitambua slogan ya hapa kazi tu.hongera jomba
 
Muro si mtu wa njaa njaa kama unavyojaribu kufikiri. Ni aina ya watu wanaoridhika na walichonacho na aina ya watu wanaotafuta "self esteem" wala sio ulaji.

Amejitahidi kueleza kwa utulivu kiasi cha kuaminisha kuwa kuna matatizo ya msingi ndani ya CHADEMA. Kinachoshangaza ni kuwa anaonyesha tangu aingie, alikuwa hakubaliani au hapatani na mengi yanayoendelea ndani ya chama hicho kiasi cha kujiuliza alikuwa anafanya nini huko muda wote huo? He has all the time been against the Party and its leaders. Alikuwa anafanya utafiti au ushushushu?

Pili, inakuwaje anaondoka kipindi hiki ambapo watafuta fursa (opportunists) wengi wanahama CHADEMA baada ya kutishiwa na dola kuwa nafasi zao zitaminywa na chama kitanyongwa katika uchaguzi mkuu 2020? Tatu, cha kushangaza zaidi, anahamia NCCR-MAGEUZI of all parties? Anatarajia mema yepi huko?

Mtu aliyeridhika na maisha yake si rahisi kujihusisha na siasa za vyama Tanzania kiasi cha kupania kwenda NCCR ya Mbatia. Kuna fursa huyu naye anaifukuzia. Na anajua NCCR na Mbatia wameandaliwa nini na Serikali ya CCM. He’s just another smart politician. Hiyo press conference ni kuwaonyesha mabwana wapya uwezo wa kuibomoa CHADEMA kwa “hoja”. Muendelezo wa dirty politics.
 
Muro si mtu wa njaa njaa kama unavyojaribu kufikiri. Ni aina ya watu wanaoridhika na walichonacho na aina ya watu wanaotafuta "self esteem" wala sio ulaji.
kweli si mtu wa njaa, lakini ungeeleza njaa ipi? Mimi naona kama ana 'njaa' sana (ya haki). CCM - CHADEMA - NCCR - ..........?? Namshauri aanzishe chama kingine amabacho atakiongoza kama anavyotaka.
Katika maisha ya pamoja huwa kuna kukubaliana, kutokubaliana, na pia kukubaliana kutokubaliana, na pia kutengana. Kama kwako kila inapotokea kutokubaliana suluhu yako ni kutengana - sijui utatengana na wangapi!!
 
Amejitahidi kueleza kwa utulivu kiasi cha kuaminisha kuwa kuna matatizo ya msingi ndani ya CHADEMA. Kinachoshangaza ni kuwa anaonyesha tangu aingie, alikuwa hakubaliani au hapatani na mengi yanayoendelea ndani ya chama hicho kiasi cha kujiuliza alikuwa anafanya nini huko muda wote huo? He has all the time been against the Party and its leaders. Alikuwa anafanya utafiti au ushushushu?

Pili, inakuwaje anaondoka kipindi hiki ambapo watafuta fursa (opportunists) wengi wanahama CHADEMA baada ya kutishiwa na dola kuwa nafasi zao zitaminywa na chama kitanyongwa katika uchaguzi mkuu 2020? Tatu, cha kushangaza zaidi, anahamia NCCR-MAGEUZI of all parties? Anatarajia mema yepi huko?

Mtu aliyeridhika na maisha yake si rahisi kujihusisha na siasa za vyama Tanzania kiasi cha kupania kwenda NCCR ya Mbatia. Kuna fursa huyu naye anaifukuzia. Na anajua NCCR na Mbatia wameandaliwa nini na Serikali ya CCM. He’s just another smart politician. Hiyo press conference ni kuwaonyesha mabwana wapya uwezo wa kuibomoa CHADEMA kwa “hoja”. Muendelezo wa dirty politics.
Martin Luther alipayaona mapungufu ya kanisa katoliki. Akapambana kwa kuanisha kasoro na kutaka mabadiliko kwa kufanyia kazi hayo marekebisho

Alikaa muda mrefu sana akipambana na huo mfumo aliotaka urekebeshwe

Hakuamimi katika kulihama kanisa na kuanzisha kitu kingine. Aliamini katika mabadiliko ndani ya kanisa

Hata hivyo kanisa lilimpuuza na halikujishughulisha na hoja zake hadi akafa

Baada ya kifo chake wafuasi wake wakaona haina haja kuendelea kushawishi wasio shawishika. Wakaamua kuanzia taasisi yao na kuiita Lutheran.

Kuna kihindi kikifika lazima uelewe hawa watu wamekataa hoja nazo ziamini hivyo sina budi kwenda ninapoona nitasikilizwa

Yawezekana kweli ikawa ni katika kutafuta fursa maana ametangaza kuwa na nia ya kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya kinondoni

Lakini hii haiondoi ukweli wa alichokisema kwamba ndani ya chadema kuna vitu vya kufanyia kazi hasa hasa hili la ukosefu wa adabu kwa baadhi ya viongozi na wanachama
 
kweli si mtu wa njaa, lakini ungeeleza njaa ipi? Mimi naona kama ana 'njaa' sana (ya haki). CCM - CHADEMA - NCCR - ..........?? Namshauri aanzishe chama kingine amabacho atakiongoza kama anavyotaka.
Katika maisha ya pamoja huwa kuna kukubaliana, kutokubaliana, na pia kukubaliana kutokubaliana, na pia kutengana. Kama kwako kila inapotokea kutokubaliana suluhu yako ni kutengana - sijui utatengana na wangapi!!
Njaa niliyomaanisha ni ya pesa kwasababu mdau alikuwa anaelekea huko kwa kusema "wamefika bei"

Nikweli kabisa anaweza kuwa na njaa ya kupigania haki kwa kushika madaraka anayohisi yatamuwezesha kufanya hivyo

Katika dunia hii kuna watu asipopata kitu fulani huwa anaona bado hajafanikiwa. Hili siwezi kupingana nalo maana siku zote amekuwa akitamani hivyo. Kufikia kitu Abraham Maslow anakiita "self esteem"

Kuanzisha chama chake ni ushauri mzuri hasa unapokuwa hueleweki kwa "wenye chama" ( hata Professor Lumumba anakubali vyama vingi ni vya watu binafsi) lakini tukumbuke lengo lake si kupigania haki kwa kumiliki chama. Lengo lake ni kupigania haki kupitia madaraka iwe ya ubunge au zaidi ya hapo
 
Kwa hiyo?
...
Screenshot_20200528_190229_com.whatsapp.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muro waambie wapiga kura wako fungu ulilolipata...ili mzigawane usile wewe na mkeo tu ni dhambi kubwa.
 
Back
Top Bottom