Pigo takatifu dhidi ya Chadema muda huu

Pigo takatifu dhidi ya Chadema muda huu

UOGA WA DEMOCRACY + UDHAIFU WA KIONGOZI + UKOSEFU WA ADABU = K

HAPO MWISHO "HAWANA ADABU"

Kwa kweli Mwenyekiti wao anafanya kazi nzuri sana ya Kubomoa Chama Chake Mwenyewe.
 
Kumbe ni umbea wa Tandale tena umeletwa na;
mtu wa tandale
wa jinsia ya 'ke'
Anaeishi kwa umbea
 
Kaongea kiswahili kama hujamwelewa m- contact prof Safari.
 
Umemwaga madini mazuri sana mkuu
Nimemsikiliza vizuri Mustapha Muro mwanzo mwisho

Halafu nimesoma comment zote za waliochangia huu mjadala hapa

Mustapha Muro namfahamu vizuri sana. Simfahamu kama mwanasiasa tu, bali namfahamu kama msomi mtaalamu wa networking engineering, aliyewahi kuwa mmoja wa watu muhimu kwa kushika top position kwenye hii mitandao ya simu unayoifahamu hasa Vodacom ambapo alifanya kazi kwa muda mrefu

Namfahamu kama mfanyabiashara na mdau muhimu katika sekta ya mawasiliano hapa Afrika mashariki kwa kuwa miongoni mwa wamiliki wa makampuni ya minara

Namfahamu kama Baba mwenye familia imara, kaka, mjomba na aina ya mtu mstaarabu na ni miongoni mwa watu wenye siasa za kistaarabu na za kisomi

Mwaka 2015 kipindi cha uchaguzi mke wake ndio alikuwa mtu muhimu wa mfumo uliotumiwa kukusanya kura toka mikoani

Kwa kifupi, yeye ndio alikuwa organizer wa wale vijana waliokamatwa hotelini wakikusanya na kuhakiki kura kutoka majimboni

Baada ya sakata lile, mke wake na baadhi ya wanafamilia wake walipitia wakati mgumu sana maana walikamatwa wote na kufunguliwa kesi tofauti kabisa ya human trafficking. Mke wake alisota segerea karibu mwezi mzima

Muro kama msomi na mtu mstaarabu anajua anachokiongea

Hoja inayotoka kwa Muro si ya kubeza hata kidogo. Ni mtu mzima na anafahamu mengi ndani ya chama na ndani ya nchi hii

Ni bahati mbaya sana wanachadema wengi hadi sasa bado wanaamini katika siasa za matusi, udhalilishaji na kukoseana adabu

Ni bahati mbaya sana chadema bado inaamini aina ya ukosoaji wa kina mdude mitandaoni

Namfahamu Bwana Malisa, ni mtu wa chadema. Anaandika sana mitandaoni. Anakosoa kwa hoja. Sikumbuki kama ameshawahi kuonekana mkosa adabu na kufunguliwa mashtaka ya uchochezi au udhalilishaji wa kimtandao

Ifike mahali tujadili hoja zinazotolewa kuliko kubeza na kujipa moyo kwamba chama kiko imara

Wanachadema wengi hata hamjui kwanini siku hizi Mnyika kawa kimya sana

Si jambo la kawaida sana wanamageuzi kama kina Mabere Malando, Prof. Safari na wengine wengi walioisapoti chadema nao wakawa wendawazimu kusema chadema haiko sawa

Kwanini? Lazima kuna kitu

Tuachane na hao wengine wanaolilia pesa ambazo wanafahamu kabisa kwanini walikuwa wanakatwa na miaka yote imekuwa hivyo

Tuachane na hao wanaolilia kudhalilishwa kingono kwasababu wanazozijua wao maana wanajua madawati rasmi ya kwenda kulalamika lakini hawakwenda

Tujadili hoja kama hizi za Muro. Ni hoja nzito zilizo na ushahidi na zinaweza kujadilika na kizuri zaidi hoja za Muro hazina majungu wala vijembe. Ni hoja ambazo zikichukuliwa zinaweza kukirudisha chama kwenye mstari

Huwezi kutaja umasikini wa Tanzania bila kuitaja CCM, huwezi kuisema serikali iliyoko madarakani bila kumtaja Magufuri. Hali kadhalika huwezi kutaja udhaifu unaotokea chadema bila kumtaja Mbowe!

Ifike mahali tukubali kwamba "huwezi kukwepa ngumi kwa kufumba macho"
 
Umemwaga madini mazuri sana mkuu
Hayo ni madini fake mkuu, kwa sisi tuliokulia machimboni tunayaita kakumba...mke wa muro hakuwahi kukamatwa kwenye hiyo inshu ya wale watu wa IT 41...analeta story za kinafki tu...acha kbs huo uzushi
 
Back
Top Bottom