Bobwe1
JF-Expert Member
- Apr 8, 2014
- 396
- 95
Baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa "wasamaria wema" kuwa Mansoor anamiliki bunduki nilidhani jambo la kwanza ilikuwa ni kupitia rekodi za wamilki bunduki na kuhakikisha kuwa Mansoor anaruhusiwa au aruhusiwi kumiliki bunduki. Kitendo cha polisi kuvamia nyumbani kwa Mansoor na kikosi cha FFU ni uonevu mtupu.
Kweli mkuu cha kujiuliza je hao wasamaria wema walitoa taarifa kama mansoor anamiliki silaha au anamiliki idadi kubwa ya risasi?kwa sababu polisi wanafahamu kuwa mansoor anacho kibali cha kuwa na silaha lakini walienda nyumbani kwa mansor wakakuta anamiliki risasi nyingi,hii maana yake ni kwa jeshi la polisi kufanya ukaguzi kwa raia wote wenye vibali vya kumiliki silaha na sio kwa mansoor isije kuwa na hao wanamiliki idadi kubwa ya risasi.