Nyie chekeni na magaidi tu, mtauona moto wao na upumbavu wenu wa kuchanganya siasa na uamsho utakwisha ghafla, boko haram wakubwa!
Nafikiri haujajua tatizo linaanzia wapi, sio kila kitu unaleta siasa na chuki zisizo na tija. Ni vizuri comment as a great thinker ili wadau wafaidike na ndio "MOTO" ya JF au kaa kimya sikiliza wajuzi.
Anyway turudi kwenye mada, Mr Mansoor anaruhusiwa kisheria kumiliki silaha za aina hiyo na pia anaruhusiwa kumiliki idadi ya risasi alizokutwa nazo ikiwa tu anamaelezo yanayo jitosheleza na nyaraka zinazoonyesha amepata risasi hizo kihalali. Ndio ipo sheria inayo limit kiasi cha risasi anachoruhusiwa raia lakini kinaweza kuongezeka kama kuna maelezo ya ziada kutoka kwa mhusika kwa mfano ukienda shooting training utahitaji risasi nyingi au kuna watu wanakwenda hunting for two weeks unafikiri atakwenda na risasi ngapi?
risasi zipo aina nyingi ukiangalia kwenye picha ya hizo risasi alizokamatwa nazo utaona zipo za bastola 9mm ambazo rangi yake tofauti na nyingine ina maana kuna hard na soft sasa je sheria ina specify kiwango cha risasi kwa ujumla au kwa kila aina? shortgun hali kadhalika zipo SG,LG,BB,SLUG etc...
Tatizo lingine kubwa ni Zanzibar hairuhusu raia kumiliki silaha lakini kibali unachopewa ni cha serikali ya jamhuri ya muungano na Zanzibar ikiwa part ya jamhuri, wizara ya mambo ya ndani ni moja ndio maana Vuai Nahodha alikuwepo pale, sasa usisahau mtu hapewi kibali mpaka apitie hatua kadhaa za kiuchunguzi!! unataka kuniambia wizara ilishindwa kugundua kwamba Mansoor ni mzanzibari na Zanzibar hairuhusu raia wake kumiliki silaha?? labda bwana Mansoor alipewa silaha akiwa kama mkazi wa bara lakini bado kibali ni cha Jamhuri ya muungano wa Tanzania Zanzibar ikiwemo ndani ya jamhuri hiyo!! usisahau moja ya sheria za kumiliki silaha ni lazima uwe nayo sehemu unayoishi huwezi kuiacha mji mwingine na wewe unaishi mji mwingine otherwise you have to surrender to police.
Hitimisho langu kuna mkinzano mkubwa wa kisheria, police hawapo tayari kumkamata mtu kwa kesi ya aina hii kwa sababu sheria haipo sawa. Kumkamata Mansoor kutaibua madudu mengi kuhusu udhaifu wa wizara na itakua aibu kwao,
Walitaka kumkomoa lakini am sure it will backfire Haaa Haaaa Haaaa.