PICHA: Rais Kikwete katika ziara rasmi Ottawa, Canada

PICHA: Rais Kikwete katika ziara rasmi Ottawa, Canada

attachment.php


amenikumbusha idd amini aliposhika dola akawashikisha adabu wazungu kumchukua mzegamzega, hapa wazungu pekee wanamvuta kikwete kwenye farasi. Duh, hujaumbwa hujaumbika.
hata muhindi hapa nchini anaweza kukubeba mabegani kama wewe ni purchasing manager kwenye taasisi kubwa hapo usishangae hata kulabwa miguu wazungu watalamba ya jk umesahau migodi ya barric wenyewe wapo huko cnd?

 
Aisee ukiwa na marafiki ni jambo la muhimu sana kujua wanakuchukuliaje, how worth you are to them. Au wewe upo nao kwa maslahi yao tu otherwise your TP. Washauri wa mzee kuweni wakweli hata kuonyesha uwajibikaji wenu. Tutegemee FDI nyingi ambazo 100 percent inarudi kwao. CANADA barick etc America Gas, for real hakuna urafiki kati ya mzungu na black aslani tutakuwa watumwa mpaka tupate akili . Wabongo we are cursed isee.
 
Lazima walipe baada ya kuwapa utajiri mkubwa wa madini yetu. Is JK who went to Canada akiwa waziri wa nje kufanya maongezi nao na leo wanaua hawaguswi wanazidi kujikita kwenye mikataba ya kuwalinda.

Mlitegemea nini kama si kwenda kuangalia kama cut lake liko poa na hasa muda huu anao elekea mwishoni mwa uongozi? Mbona hajaenda Pakstan au Afghanstan?

Tuna kazi kubwa
 
Sultani mangungo wa msovelo. Hii kitabu naimiss ipo kwenye history eeeh.
 
Protocol rasmi imekua hivyo? basi ni kwa ajili ya kumlainisha.

Tom umewai ona rais amealikwa na kutembelea TZ kiserikali? Inatakiwa apokelewe, akague gwaride la heshima, na mengineyo mengi ikiwemo dhifa at the state house! Ukiangalia picha utaona JK kapokewa, tofauti na kawaida amewekwa kwenye gari la farasi, haya tunayaona sana Canada, UK, Australia na mengineyo ndani ya protocol!! Mimi ni mpinzani sana wa JK katika usendeshajio wa serikali lakini kwenye hili tuache yasiyo maana bana!!!

Hiyo ni state visit!!!
 
Lazima walipe baada ya kuwapa utajiri mkubwa wa madini yetu.Is JK who went to Canada akiwa waziri wa nje kufanya maongezi nao na leo wanaua hawaguswi wanazidi kujikita kwenye mikataba ya kuwalinda .Mlitegemea nini kama si kwenda kuangalia kama cut lake liko poa na hasa muda huu anao elekea mwishoni mwa uongozi ? Mbona hajaenda Pakstan au Afghanstan ? Tuna kazi kubwa

Jamani utajiri wa madini ni wetu, lakini pia ni sisio wenyewe ndo tumetengeneza sera mbovu ya madini!!! FYI wanaochimba madini si serikali ya Canada ni makampuni ya Canada na nchi zenginezo, Rais hawezi alikwa kwa ziara ya kiserikali akazungumzie cuts/kickbacks kwenye business isiyofanywa na serikali!!

Tuache kupiga tu domo bana!!!
 
Kweli JK ni dhaifu, yeye ni kupenda munyenga tu, hadi amefanya kila kuona kuwa urais ni simpo sana, Jamaa anatia aibu kweli
 
Kwa kweli kwa kiwango hicho cha anasa na wenzetu walivyokwishamfahamu kiongozi wetu alivyo, bado tu mtu utakua haujaanguka sahihi ya kuuza nchi hata bila ya kusoma na kutafakari aina ya mikataba unayoingia?????

Mnh...........!
 
Jamani hiyo ndiyo protocol ya ziara rasmi ya kikazi!!! Sasa ulitaka iweje mkuu?
Watu hawakatai kuwa hiyo ndo protocol. Suala hapa ni kuwa ikishakumbukwa hiyo protocol basi na hamu ya kukaa nyumbani inaisha!
 
Mwenzenu ameenda kuwahakikishia kuwa yale mabadiliko ya sheria ya madini yaliyoongera mrahaba, utekelezaji atahakikisha anaukwepa hadi atoke madarakani!!!

Ni mwendo wa kutembeza bakuli tu!!

Mkuu hapo umenena. Atapewa ka-msaada kiduchu halafu atachekelea kama ....... Nyerere aliyasema yote. Atakaporudi atatuambia kama sio ziara zake za kuhemea tungelikuwa tumekufa njaa. Kazi kweli kweli
 
Sina tatizo na ziara zake ziwe za binafsi, Kiserikali au vipi, poa tu! maana huwa sioni tofauti ya JK kuwepo nchini au kutokuwepo. Kinachoniuma ni deni atakaloliachia taifa atakapokabidhi madaraka kwa mwingine.
 
Mbona sijawai kuona USA akifanyiwa hivi.!

Swali zuri sana! Canada ni mfaidika mkubwa sana wa miradi ya migodi ya Tanzania. kwa namna yoyote ile, Tanzania ni nchi muhimu sana kwa Canada, manake pato lao litokanalo na 'uwekezaji' wao nchini Tanzania ni kubwa maradufu... Hivyo kiongozi yoyote wa Tz ambaye anasimamia maslahi haya ya wacanada, lazima ataheshimika sana na kupewa hadhi ya juu sana aendapo Canada! Marekani sio mfaidika wa kihivyo so haihitaji kumpa 'mshkaji' treatment ya aina hiyo!
 
Sawa hizi kelele haziwazuii kulala ,lakini kumbukeni hata Gaddaffi alisema hivyo hivyo na mwishowe aliishia mtaroni!! Kuna siku hiyo nyumba mtaikimbia!

Hiyo siku ni after 2015 yeye kamaliza awamu yake plus good time kibao!!! sasa,mjanja nani?
 
Unaacha mipaka yetu ina porwa na malawi wewe unaenda kuvutwa na mikokoteni ya wanyama? Si Arusha ipo inayo beba maji kutoka visimani? kweli watanzania mzigo mnao. Ole wako utoke madarakani ukituonyesha nchi yetu imebaki nusu.

iko siku atazungumzia raha ya kuendeshwa na gari la farasi linaloendeshwa na wazungu! atawauliza nyie wamatumbi kama mmewahi kuisikia hiyo raha! am so sure personally jamaa atakuwa anajisikia kama yuko peponi! ni vile tu ni mtu mzima lkn angeweza angekuwa meno yote nje kama mtoto wa miaka 7 akifurahia gari la farasi! na kwa vile wenzetu wanamjua udhaifu huu wake, wa kupenda matanuzi, watampa matanuzi yote...ili wao waendelee kuchuma migodini kwa kasi zaidi....nguvu zaidi....!
 
Nikimwangalia JK na uongozi wake, sitaki kabisa kusikia wale wanaotangaza nia na kuanza kuandaa mitandao ya Urais. Nawaogopa kama Mwl Nyerere alivyotuasa.
 
ahhhaaa hili TAIFA kweli Rais tunaye, hivi kagame huwa naenda kwenye anasa na tafrija namna hii? anapokelewa na waziri wa mambo ya Nje, duh heshima ya tanzania Nje kwisha.

Sasa wewe ulitaka apokelewe na nani? Yeye mwenyewe ni Waziri wa Mambo ya Nje, kama unabisha hesabu safari za Membe na Vasco ndio utajua nani ni Waziri wa mambo nje
 
Ndio alichoenda kufanya huko kupewa heshima na kupanda farasi, Rais kweli tunae na tuna safari ndefu sanaaaaa

Mbona anaonekana kuwa na WOGA kwenye huo mkokoteni wa farasi? Si ndo vitu anavyopenda yeye? Mbembea n.k.
 
kweli tanzania tuna dharilishwa sana tuweni makini na marais waina hii mimi sijafurahishwa kwa rahisi kuburuzwa kwenye farasi sijui kama anauelewa wa kina kwa kiasi gani. maana hapa hata bodigard wake siwaoni yaani ni aibu kwenda mbele
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom