PICHA: Rais Kikwete katika ziara rasmi Ottawa, Canada

PICHA: Rais Kikwete katika ziara rasmi Ottawa, Canada

..labda JK akirudi ataufufua ule mradi wa farasi ulioanzishwa na Edward Sokoine[r.i.p].
 
Si ndo nchi inayo vuna almasi za watanzania!(kahama mining) hapo baada ya kupanda hao farasi madini yatachotwa bure wakati PAYE zinatumaliza watanzania, mpaka Mungu arudi tutabakia mifupa.
 
Kapokelewa airport na waziri wa mambo ya nje? Wazungu wanatudharau hivyo. waziri mkuu au gavanaa walikuwa bize?
hivi mtu kama Jimmy Sinclair anakufikiriaje wewe?
 
Hivi kwa nini Jk asimpe shavu siku moja moja Dr na yeye akasafishe macho inaweza ikapunguza hasira zake.
 
Jamani huo ndiyo utaratibu wa nchi za kifalme, Rais wetu mpendwa asingekataa mapokezi ya namna ile!
 
Give a "DOG" a good name & ........

ABG@ work!
 
madini yetu yooote barick wamebeba kwa mikataba ya hovyo. Hicho anachokirimiwa ni matusi kwa Wadanganyika.
 
PICHA ZAIDI

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA ZIARA RASMI OTTAWA, CANADA



ot17.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha wageni huku akiangaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada Mhe. John Baird baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Macdonald Cartier jijini Ottawa, Canada, kwa ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Jumatano Oktoba 4, 2012


ot5.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba fupi baada ya kuwasili katika viwanja vya jumba la Rideau jijini Ottawa, Canada, katika hatua yake ya kwanza ya ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Jumatano Oktoba 4, 2012. Jumba hilo ndilo makazi na ofisi rasmi ya Gavana Jenerali wa Canada tangia mwaka 1867 ambapo pamoja na kuishi humo pia hapo ndipo hutumika kwa kuwatunukia wananchi wa Canada waliofanya vyema, pa kupokelea wageni mashuhuri wa nchi za nje na pia ndipo anapofanyia shughuli zote za kitaifa akiwa kama mwakilishi wa Malkia wa Uingereza.
ot7.jpg

ot8.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na Gavana Jenerali wa Canada Mhe. David Johnson na mkewe Mama Sharon Johnson kuingia jumba la Rideau jijini Ottawa, Canada, katika hatua yake ya kwanza ya ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Jumatano Oktoba 4, 2012
ot9.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika mazungumzo na Gavana Jenerali wa Canada Mhe. David Johnson na mkewe Mama Sharon Johnson na viongozi wa serikali ya nchi hiyo katika jumba la Rideau jijini Ottawa, Canada, katika hatua yake ya kwanza ya ziara rasmi ya siku mbili jijini humo Jumatano Oktoba 4, 2012




 
Anapokewa na waziri wa mambo ya nje, kiongozi mkuu wa nchi kasafiri, au ndio wamemchoka JK
 
ot18.jpgasipofanya hivyo tutakufa na njaa jamaaani......haya viwanda vya uongo anzeni manufacturing sasa:lol:
 
Wanamjua alivyo mpenda makuu. Madini yetu wanaiba na kumpumbaza. Nasikia ataongea kwenye chuo cha Carleton sijui atasema nini jamaa huyu ambaye usomi unampiga chenga? Tusubiri vichekesho na vituko. Natamani hata Salma angepewa nafasi ili afichue umamamuma wake.
 
Teh! teh! teh! ....

Eti jamani hivi Bagamoyo kuna Farasi kweli?! ...

Dah! ... utalii mwingine huu! ... naona jamaa alifikiria baada ya kutoka kubembea Jamaica ... akaona staili hii (ya kupanda farasi) bado hajatoka nayo!! ..
 
Arudi home kama ni kupanda mnyama tutampandisha punda , wa Tanzania tunasafarindefu saaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaana
 
''Mwanajeshi'' wetu mbona ''marching'' yake haiendani na hao wanajeshi wengine?.......left....right......left......... right

attachment.php
mimi nime-focus zaidi kuangalia hii john travolta yake anayokanyagia.inaonekana ni genuine na sio fake.hakika ametokelezea.
 
Kwa kweli kwa kiwango hicho cha anasa na wenzetu walivyokwishamfahamu kiongozi wetu alivyo, bado tu mtu utakua haujaanguka sahihi ya kuuza nchi hata bila ya kusoma na kutafakari aina ya mikataba unayoingia?????
 
tanzania people naomba muache ushamba huyu ndiye rais ambaye amebahatika na hamana mwingine tutakae mpata safari zake zote zina mafanikio nchi yetu inamaaendeleo makubwa sana angalia nchi za jirani.Rais ana khaki kubwa kupokelewa na heshma kubwa angalieni alivyopokelewa kwa heshma bwana mtachukia sana nai hapendi kueshimika??hongera sana mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom