Picha: Ni kama Wana Israel wakivuka bahari ya Shamu

mirindimo

JF-Expert Member
Nov 2, 2009
821
1,343
Mambo CCM inapenda kuyaona, hawa viumbe wa CCM hawataki waone unapata raha hasa wewe mlipa kodi utapigika kisawa sawa

IMG_9836.jpeg
 
Ishu sio ccm ni hali ya mvua kubwa na changamoto za miundombinu ambayo kwa uwingi wa mvua hizi inaelemewa. Mvua zinamwaga maji ndani ya muda mfupi tu mito inajaa.
 
Na ndiyo maana wengi wetu maneno kama ”ndugu mwananchi,lipa kodi kwa maendeleo ya taifa letu” tunayachukia tunayachukulia kama kelele maana hatuoni kinachofanyika
 
Na kuna greda ziko hapo takribani miaka miwili sasa zinachota pesa kila siku. Kufa kufaana
 
Tatizo ni serikali kwa maksudi kabisa kujisahaulisha kwamba, hilo eneo ni hatarishi kila majira ya mvua yanapofika,

Mvua zikianza, wanajidai kama watenga bajeti, bajeti yenyewe inaishia hewani tu, tatizo linabakia pale pale na kuzidi

Wananchi tuifanye nini serikali inayoongozwa na watu aina hii??
 
Kama vyeo vyenyewe miaka nenda watu wanapeana kwa kujuana! Ndiyo tutegemee maajabu!!! Mambo kama hayo lazima yatokee.
 
Jangwani, Dar Es Salaam Tanzania.
watanzania mateso haya yote tumeyataka sisi - CCM hawana jipya - we uliona wapi ukaidhinisha ujenzi wa kituo cha mabasi kando kando ya njia ya mto ? maji yapite wapi?
 
Back
Top Bottom