PICHA: Mererani mwanajeshi ajitoa mhanga

PICHA: Mererani mwanajeshi ajitoa mhanga

likelihood kuwa huyu sio mwanajeshi ila ni pandikizi ni kubwa,coz hiyo uniform haipo tena imebadilishwa,lkn kama ni mwanajeshi, kutokana na kiapo chake,na taratibu na masharti ya ajira ya jeshi,huyo hana kazi tena,,,,,pole yake kama alidhani ni mzaha na masihara ya kushabikia vitu asivyoelewa madhara yake.
 
ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo,

karibu kamanda wa ukweli kwenye kambi ya watetezi wa wanyonge.
 
Naona atangulie tu kujifukuzisha kazi mwenyewe kama yule mwenzake wa Morogoro....ILA Kuna ISHARA fulani imeonekana kwa serikali na chama cha magamba
 
Magwanda ya kijeshi yanauzwa kila uchochoro wa mitumba! sasa gwanda hilo halinishangazi maana tangu turuhusu mitumba sio shida tena kujipatia gwanda la jeshi!
Wapuuzi kama nyie ndio mnaifikisha Nchi kubaya kwa kuwa viongozi walio madarakani wakisoma thread ya kichwa kama chako wanabweteka wakichukulia hivyo unavyowaza wewe.

Kitendo cha kijana Mwanausalama [Mwanajeshi] kusupport siasa wai wazi si cha kuchukulia mzaa kihivyo unavyochukulia kama kuuza karanga barabarani.Kitendo cha huyo kijana kujitanabaisha hivyo waziwazi,jua kweli kajitoa Muhanga wa kweli.Wewe nae hapa na wapuuzi wengine wa aina yako unaona sawa na unaleta Comedy.

Kujitoa muhanga kwa askari huyo,ujui ni askari wangapi wataigiwa na mori huo,na pia ni ishara kuwa pia mambo si shwari kwenye majeshi yetu.Huyu ni kijana ambae yuko tayari kwa lolote ujui kesho wangapi watajitokeza nao kuingia kwenye sura ya taswira hii.

Tunapaswa kuiona hii katika picha ya ndani sana kuwa tumefika wapi na mambo haya.Ndio maana tunategemea Mwanajeshi wa Tanzania kuwa mvumilivu mpaka dakika ya mwisho, unapoona mlinzi wako wa uhai nae anaanza kuona maluwee lue jua basi wewe mwenyewe uko hatarini, tena hatarini kweli kweli.

For real this is very interesting issue kwa kumalizia mwaka na TASWIRA magumashi yanafika mwisho, walioko madarakani tia maji tia maji............!!!
 
sina hakika kama kweli atakuwa mwanajeshi kama hatawajibishwa maana nadhani wanajeshi hawaruhusiwi kuonyesha msimamo wao au kujihusisha na vyama vya siasa moja kwa moja.
 
Narudia hii haijawahi tokea! vyovyote vile huyu ndio askari wa kwanza kwa majeshi yote kujilipua hivi!

Mkuu MTAZAMO kwa mambo yanavyokwenda hii nchi hawa wapo wengi tu. Its a matter of time!
 
Mwanajeshi mmoja ameamua kujitoa mhanga na yuko tayari kufukuzwa kwaajili ya CHADEMA maana amechoshwa na maisha magumu ya kwake binafsi na ndugu zake...
View attachment 76434
Lema, Nassari na mwanajeshi aliyeamua kusema yupo tayari kufukuzwa kwa ajili ya CDM LEO kwenye mkutano Mererani
Tumejaribu kuangalia ktk kumbukumbu zetu tumebaini kwamba hatuna mwanajeshi wa namna hiyo.
Sasa tunajipanga kushitaki Lema kwa kosa la kumiliki uniform za jeshi uku akijua ni kosa kubwa kisheria.

By Mwamunyange.
 
Nafikiri ya jeshi tuwaachie jeshi,aliyejitoa katoa ya moyoni,ila niulize Nassari toka tumekuchagua mbona umetutelekeza? Tumebakia kukusikia tu,jimboni kwako hutembelei vijijini ukafahamu yanayojiri!! au ndo tuvute subira? 2015 ni karibu jitahidi ufanye la kujivunia..
 
Magwanda ya kijeshi yanauzwa kila uchochoro wa mitumba! sasa gwanda hilo halinishangazi maana tangu turuhusu mitumba sio shida tena kujipatia gwanda la jeshi!

Mtajipambambanua kwa njia nyingi lakini sawa na mwanaume asiye na kizazi ... Bado mtanunua hadi nguo za mgambo wa jiji,za manesi na madr alafu mpige nao picha.... Hata kwa macho tu mtoto mdogo anajua huyo kibaka tu kaokotwa mtaani kavalishwa nguo .

Hata hizo nguo zinapatikana hata kwenye maduka zinaendana na kombati.La kushangaza hakuna.Angejitaja jina hapo sawa.Siasa ndo hizo wazee.

Katika sheria za kijeshi huwezi kuvaa nguo inayofanana na sare ya Kijeshi tena imekamilka kuanzia Suruali, Combat, na kofia kisha ukajianika hadharani pasipo kukumbana na mkono wa sheria wa kijeshi.

Je, mnamkumbuka yule jamaa alikamatwa Morogoro akiwa amevaa sare za jeshi na ikiwa hakuwa askari Jeshi???

JE, alipatwa na maswahiba gani baada ya kukamatwa???

Acheni kuongea kiushabiki!!!!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Lema na makamanda wenzako tunakushukuru,kwani wiki hii yote humu jamnvini mjadala utakuwa huyu kamanda safi sana,

maana mawakala wa pale Lumumba wameshaanza maneno yao yenye kichefuchefu
 
Naona atangulie tu kujifukuzisha kazi mwenyewe kama yule mwenzake wa Morogoro....ILA Kuna ISHARA fulani imeonekana kwa serikali na chama cha magamba
Naona wewe umefanya kinyume...wenzio wanapulizaga kwanza kisha ndio wanang'ata.Wewe umeng'ata kwanza kisha ndio ukapuliza lol.
 
Maxence Melo

Hairuhusiwi comrade, ipo wazi kwenye "volumes", ingawa una haki ya kupiga kura, huruhusiwi kushiriki siasa kwa kuwa mwanachama wa chama chochote, kupigia kampeni chama chochote na hasahasa kwenda kwenye mkutano wa kisiasa na mavazi ya kijeshi.., hii ni miongozo ipo kwenye vitabu,

kama mtu atafanya lolote kupingana na hiyo miongozo anachukuliwa hatua.haijalishi ni ccm au cdm, hayo ni makosa.na kama ni mwanajeshi kweli, trust me, leo haiishi huyo jamaa tayari atakua ameshaandika maelezo mengi sana kujieleza kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu.

Ikumbukwe, maana ya kuwekwa miongozo ya namna hii ni kwamba jeshi halina chama, jeshi linawajibika kwa amiri jeshi mkuu aliyechaguliwa na wananchi bila kujali chama.na ndio maana halisi ya miongozo ya namna hiyo.

Bottom line ni makosa hayo haijalishi imefanywa na nani kwa chama gani.
 
Last edited by a moderator:
Magwanda ya kijeshi yanauzwa kila uchochoro wa mitumba! sasa gwanda hilo halinishangazi maana tangu turuhusu mitumba sio shida tena kujipatia gwanda la jeshi!

Hebu jaribu kubeba hata begi la jeshi tu, halafu uje utusimulie yatakayokusibu kama utaweza kusalimika.
 
Narudia hii haijawahi tokea! vyovyote vile huyu ndio askari wa kwanza kwa majeshi yote kujilipua hivi!
...Kuna yule polisi aliyejilipua Dodoma wakati wa mkutano mkuu wa magamba naye vipi? aliporudi morogoro akawakabidhi makolokolo yao akala kona!..
 
Tumejaribu kuangalia ktk kumbukumbu zetu tumebaini kwamba hatuna mwanajeshi wa namna hiyo.
Sasa tunajipanga kushitaki Lema kwa kosa la kumiliki uniform za jeshi uku akijua ni kosa kubwa kisheria.

By Mwamunyange.


Mjitayarishe kuwakana wanajeshi wote kama ndiyo hivi. Hawa si kama madaktari ama walimu wanaoweza kugoma utokana na sheria zao, ila askari wengi wa vyeo vya chini halizao kimaisha ni ngumu mno.
 
Tumejaribu kuangalia ktk kumbukumbu zetu tumebaini kwamba hatuna mwanajeshi wa namna hiyo.
Sasa tunajipanga kushitaki Lema kwa kosa la kumiliki uniform za jeshi uku akijua ni kosa kubwa kisheria.

By Mwamunyange.

Kwani lema ndiye amevaa hizo Gwandwa? Au wanataka wakashindwe tena Mahakamani?

TUMBIRI (Upanga, Dar es Salaam - Tanzania),
tumbiri@jamiiforums.com
 
Back
Top Bottom