PICHA: Mapokezi haya ya Viongozi wa CCM Taifa Mkoa wa Geita yana maana gani?

Vugu-Vugu

JF-Expert Member
Feb 24, 2017
1,109
1,265
Baada ya Sekretarieti ya CCM-Tanzania inayoongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Taifa Crde Daniel Chongolo kuwasili mkoa wa Geita limeibuka Shangwa na mabango kedekede yenye kumpongeza na kumtia moyo Rais Samia Suluhu Hassan,

Hii ni tafsiri chanya ya anayoyafanya Rais wetu katika kuliletea Taifa letu maendeleo endelevu,Furaha ni kubwa zaidi kuona vijijini wanachi walivyohamasika katika kuendelea kuiamini na hatimaye kuichagua CCM-Tanzania,Hakuna kama Samia




 

Attachments

  • Nov 15, Doc 2.pdf
    389.9 KB · Views: 38
Wamemkubali sana Rais Samia ndio maana yake jombaa kama hutaki acha,
 
Mulaaniwe.
Sio kwa matungulile, wala ndulele mekoni
Si kama kinjekitile, unga na maji ya mtoni
Ni kwa hilo jasho tele, Damu tabu za maskini
Nasema Mulaaniwe huu wimbo mpya mjini

Mkata mkato umemkata, kwenye simuni maskini
Wamdumishia ukata , yala! ni hospitalini
Haitoshi kutibika, akatutoka jamani
Nasema Mulaaniwe, mulaaniwe milele

Mtwana pamoja watwana , wakike tumwite nani
Kabisa tunalandana , jasho letu vietini
Bado twa beba mabwana, da! tupo utumwani
Mulaaniwe kwa jasho, mulaaniwe milele

Mapasipoti shidani, garama nao mlolongo
Fursa za ugaibuni, mnatufelisha wabongo
Tumewakosea nini, mwatupiga na magongo
Nasema mulaaniwe, na vizazi vyenu vyote
 
Mbona sijaona bango linalolalamika ughali wa maisha??
Au huko kwao maisha ni nafuu????
 
Aende mwingine unamsifia anayeruka na ndege zetu ughaibuni! Mnawavunja saana moyo waliokuja kuwatembelea!
 
Hapa ndo naonaga wtz hatuna akilini.bango linamtaja samia.kwani samia yuko geita?makada sijui tukoje.kyaaaaa😪😪😪😪
Vitongoji watapongezwa lini,
Miradi ina miaka zaidi ya 25yrs haijakamilika halafu wananchi tunanyanyua mabango ya pongezi.
Nyanyueni mabango yenye shida hao chawa wapeleke
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…