PICHA: Mafuriko Maeneo mbalimbali jijjini Dar

PICHA: Mafuriko Maeneo mbalimbali jijjini Dar

nyani ngabu ni kweli unachosema eti maji yanazidi posta na bahari ipo mita 400 mbele ni ukosefu tuu wa akili mkuu miundombinu mnayosema haiji yenyewe hata huko sio kwamba ilikuepo tuu akili zao za kutatua changamoto zinazowazunguka ndio zinefanya kuwe ivyo..
 
Hahaaaa hadi millennium towers kulifurika.

Really? I guess na hapo ni bondeni.

Narudia tena....drainage....drainage.....drainage!
 
Nimezaliwa Dar...nini kukaa...nayajua mabonde yooote milima na tambalale...
ok! Hongera sana! Mimi ni mmoja wa wakaz wa maeneo ya mbezi beach, Mkuu miundo mbinu ndiyo chanzo cha hayo yote, Angalia posta inovyobadilika mvua Ikinyesha sasa nako ni mabonden?
 
ok! Hongera sana! Mimi ni mmoja wa wakaz wa maeneo ya mbezi beach, Mkuu miundo mbinu ndiyo chanzo cha hayo yote, Angalia posta inovyobadilika mvua Ikinyesha sasa nako ni mabonden?
haijalishi nani yuko responsible kwa haya mafuriko...maji yanaingia ndani hayaingii??? kwa pesa uliyonayo usingeweza pata sehemu isiyo na karaha???!! ulivyokuwa unanunua ulijua kuwa kuna mafuriko ya kudumu au uliingizwa mkenge???!

Kusema serikali haijengi miundo mbinu haisaidiii...jisaidie pale unapoweza...epuka kujenga mabondeni
 
Na wakazi wa daresalamu siku hizi wachafu..unakuta wametupa mifuko ya Rambo miferejini...lazima ifurike...
Kule posta nasikia mchina alipewa tenda ya kukarabati mifereji...akatoa bomba kubwa kaweka dogo...nilisikia sijui kama ni kweli...toka arekebishe ndio hivyo...mvua kidogo mafuriko hayooo....zamani city centre hakukua na shida kabisa...
Nimesoma o'level katikati ya mji sijawai kuona mafuriko miaka yangu minne (1990s)
 
Mvua ya jana si ya kuleta sijui mafuriko.

Watu tushashuhudia mvua kubwa na hukuti maji yametuama sehemu kwenye makazi ya watu. Sana sana kinachotokea ni unakuta mabwawa ya kutengenezwa na watu maji yake yanaongezeka kwa sababu kuna mikondo ya kueleweka inayosafirisha maji kwenda huko.

Sasa hii Dar drainage system yake ni mbovu kuliko maelezo. Kama downtown kunafurika huko kwingine itakuwaje? Downtown iliyo karibu na bahari lakini bado kunajaa maji!

Hapo tatizo kubwa si ubonde....ni ukosefu tu wa miundomisingi bora ya kusafirisha maji.

Texas - Flash Flood Emergency in Houston After 12 Inches of Rain in 24 Hours - FloodList

houston-floods-april-2016-600x400.jpg


2-houston-floods-april-2016-600x413.jpg
 
Na wakazi wa daresalamu siku hizi wachafu..unakuta wametupa mifuko ya Rambo miferejini...lazima ifurike...
Kule posta nasikia mchina alipewa tenda ya kukarabati mifereji...akatoa bomba kubwa kaweka dogo...nilisikia sijui kama ni kweli...toka arekebishe ndio hivyo...mvua kidogo mafuriko hayooo....zamani city centre hakukua na shida kabisa...
Nimesoma o'level katikati ya mji sijawai kuona mafuriko miaka yangu minne (1990s)
Hata mimi najiuliza hivi zamani kulikuwa hakuna mvua?? Sijawahi kuona mafuriko ya aina hii enzi hizo, mvua kidogo tu maji kila mahali.
 
WATABIRI WA HALI YA HEWA WALITOA TAADHALI LAKINI TATIZO HAWATOI USHAURI WATU WAFANYA NINI... POLENI, MASKINI HAPO MAENEO YA MBEZI TANK BOVU KUNA KAKA YANGU .... SIJUI YUKO NA HALI GANI... EBU NIMPIGIE SHEM NIJUE KINACHOENDELEA HAPO
umpigie shemu eti eee! basi sawa kaka kakosa usafiri, wala usijali tuko peke yetu
 
nawaza maji taka tu yanavyokanyagwa na kuingia masebuleni...kipindupindu kitaisha vipi?
kwa nchi ambayo ni kubwa ki eneo tulitakiwa tukwepe haya maji..mafuriko hayazuiliwi kwa mikono...
Kama nchi tajiri tu yanawatoa jasho si ndo kwa mipango gani tutaepuka mafuriko...dawa ni kama una ela tafuta eneo zuri...ukisubiri mipango miji utasubiri sana
Kuna baadhi ya maeneo watu walishajenga kitambo na wakakaa vizuri, anakuja tajiri mmoja anajenga kwenye mkondo wa maji alafu anapiga fence kubwa na maji lazima yabadili mwelekeo tu kwenda kwenye makazi ya watu.
 
Kuna siku tulienda kuangalia kiwanja na mshikaji maeneo ya makonde mbezi ya kimara...kiwanja kilikuwa kikuuubwa afu bei ndogo ukilinganisha na uzuri wa kile kiwanja ...
Tuakkubaliana kabisa kuwa tunaleta ela siku inayofuata...Mungu mkubwa...mvua si ikanyesha...aisee gari ilikuwa na four wheel lakini tulishuka na kuanza kutembea kwa miguu maana ilikuwa inateleza hakuna maelezo...dongo la mfinyazi haswa...
Tulivyofika tukamwambia yule mama tutakuja tena siku nyingine...nahisi aligundua tumeshtuka...akaanza ooh mtashirikiana na wenzenu majirani kutengeneza hii barabara...hahahaha...tutengeneze barabara sie tanroads...
Yani tulishukuru mmno...from that day ikawa formula...kiwanja kizuri utakijua wakati wa masika
Hapo naona tatizo sio kiwanja ila ni barabara, na kwa taarifa tu barabara nyingi za huku zimeimarishwa na wanainchi wenyewe.
 
bado lawama zinazostahili ziwafkie huko serikalin. ni vitu vya kuepukika
 
Back
Top Bottom