PICHA: Mafuriko Maeneo mbalimbali jijjini Dar

PICHA: Mafuriko Maeneo mbalimbali jijjini Dar

Dar ni moja kati ya 'majiji' ya ajabu sana...
 
Sio suala la bonde, ni miundombinu mibovu. Kama Mbezi Makonde, Mbezi juu, Mbezi Tangi bovu nk ni bondeni inabidi Dar nzima ijengwe milimani.
Watu wanajenga kwenye mikondo ya maji wakitaka kuobdolewa UKAWA mnaenda mahakamani....
 
Hali iko hivi muda huu maeneo mbalimbali katika jiji letu la Dar
Kwa kweli inafaa tuchukue tahadhari na hizi barabara zetu za kibongo hasa kipindi hiki cha mvua.

Wadau kama upo sehemu nyingine yenye hatari kama hii, tupia picha au video ili kila mmoja achukue tahadhari.

Mbezi beach Tangi-Bovu

View attachment 342978

View attachment 342979
View attachment 342980

Maeneo ya Milenium Towers

View attachment 342960

View attachment 342964
Maeneo ya Posta Leo

View attachment 342969 View attachment 342970 View attachment 342972
View attachment 342973

Maeneo ya Mikocheni, Karibu na KFC
View attachment 342985
View attachment 342986

Hapa maji yanaingia ndani, wameweka mchanga mlangoni kuzuia

View attachment 342989
View attachment 342988 Kigamboni
imageuploadedbyjamiiforums1461837699-935606-jpg.342948
Asante mkuu na mimi nitazitundika za huku Kyela kesho ni balaa,sijui mitumbwi inapatikanika wapi kwa sasa
 
Mfano kuna viwanja vya serikali pugu...ni mchanga mtupu ...hata mvua inyesheje hakuna mafuriko...na Nyerere road haijawai kufurika ...labda kidoogo pale maeneo ya vingunguti ambako nako ni mkondo wa maji...lakini si kwa kiasi hiki cha mbezi beach...kunapitika shwari tu
 
Jamaa yangu mmoja gari iliingia maji nzima imeharibika sana
 
Mvua imezidi ila pia miundombinu sio rafiki kwa mvua hii ilitakiwa itafutwe kampuni kweli kwa ajili ya miundombinu na kuvuna hayo maji yaelekee usawa wa bahari au kuyatunza kwa ajili ya recicle kwa maji ya kunywa sema kwa siasa zetu sioni kama hili litawezekana...
 
Tatzo miundo mbinu sio rafiki

Kabisa.

Tatizo kubwa si low lying areas.

Tatizo kubwa ni drainage system.

Hata nyumbani kwako jinsi ambavyo umeitengeneza landscape ndiyo itaamua ni athari kiasi gani utakayoipata.

Mvua ya jana ilikuwa ndogo mno si ya kusababisha maji kiasi kile kukusanyika na kufanya ionekane kama ni mafuriko wakati hata hayakuwa mafuriko.

Hakuna mikondo ya kueleweka ya kusafirisha maji ya mvua. Kwanza hata itoke wapi huku kwenye hizi barabara zetu za makorongo na matope?

Kuna vidimbwi vingine ukiviona mvua ikiwa haijanyesha na ikiwa imenyesha huwezi kuamini.

Mfano mzuri pande za polisi Mabatini. Kuna drainage system gani pale? Au kule Makonde....kwanza sielewi hata watu wanaishi ishije huko!

Bado kabisa sijaona drainage system iliyo bora....hata hapo Posta penyewe haipo. Mvua kiasi tu ikinyesha lazima pafurike.
 
Hata Jangwani ni umasikini ndio unafanya serikali ifukuze watu...pale kungekuwa na miundo mbinu ni eneo strategic kabisa...ila mwananchi kama una uwezo chukua tahadhari na tafuta eneo lenye usalama...ukijena kwenye mkondo wa maji na kusubiri kulaumu serikali utasubiri sana...mwenye hasara ni wewe
 
Huko Bunju ukitaka kuja town haupiti mbezi beach kweli? Au kuna njia mbadala?
Ungejitahidi kuelewa point Mbezi mafuriko wanaishi nayo sisi wa Bunju tunayapita tu hapo kama tukiwa na safari za kutupitisha huko, lakini hatuishi na mafuriko huku Bunju, see the difference?.
 
Mvua imezidi ila pia miundombinu sio rafiki kwa mvua hii ilitakiwa itafutwe kampuni kweli kwa ajili ya miundombinu na kuvuna hayo maji yaelekee usawa wa bahari au kuyatunza kwa ajili ya recicle kwa maji ya kunywa sema kwa siasa zetu sioni kama hili litawezekana...

Mvua ya jana si ya kuleta sijui mafuriko.

Watu tushashuhudia mvua kubwa na hukuti maji yametuama sehemu kwenye makazi ya watu. Sana sana kinachotokea ni unakuta mabwawa ya kutengenezwa na watu maji yake yanaongezeka kwa sababu kuna mikondo ya kueleweka inayosafirisha maji kwenda huko.

Sasa hii Dar drainage system yake ni mbovu kuliko maelezo. Kama downtown kunafurika huko kwingine itakuwaje? Downtown iliyo karibu na bahari lakini bado kunajaa maji!

Hapo tatizo kubwa si ubonde....ni ukosefu tu wa miundomisingi bora ya kusafirisha maji.
 
Back
Top Bottom