[PICHA] Maandamano ya CHADEMA Mkoa wa Mara

[PICHA] Maandamano ya CHADEMA Mkoa wa Mara

..Chadema wasijaribu hata siku moja kumfukuza Shibuda.

..wanapaswa kujifunza makosa waliyoyafanya kwa Kafulila.

Sikubaliani wewe mkuu, mi nadhani Chama kiongozwe na 'policy''. Chadema wakianza kumuogopa mtu ndio mwanzo wa matatizo. Angalia CCM sasa hivi wanamatatizo makubwa sababu tu wanamuogopa Chenge/RA/EL.

Hapa simaanishi kuwa wamfukuze tu Shibuda, hapana nina maana wafuate taratibu hadi itakapofika wakati wa kumfukuza.

Kuhusu Kafulila mimi nadhani uamuzi wa kumfukuza ulikuwa sahihi kabisa. Huwezi kuwa na watu wawili watatu wanaotaka kuvuruga chama kwa masilahi yao binafsi. Alipoondoka Chadema akasema ni chama cha ukoo na ukabila, lakini ni huyo huyo alikua kiongozi CDM masaa 24 kabla hajaondoka. Angalia Kafulila ndiye ameungana na CCM kuyumbisha kanuni za bunge in favor of CCM ili apate uwaziri kivuli.

Ni kutokana na vurugu za akina Kafulila na Hamad Rashid Makinda akapata mwanya wa kuchagua akina Lowasa na January huku wapinzani wakipigana wao kwa wao. The bottomline ni upuuzi wa Kafulila na hisia za kulipa kisasi. Uzembe huu wa Kafulila unadhihiirisha maamuzi sahihi ya CDM.

Maelezo yangu hapo juu ni mifano ya viongozi wanaodhani wao ni Chama. Chama kijengwe kama taasisi na si watu. Alikuwepo Mtei, akaja Bob Makani, sasa Mbowe na atakuja mwingine n.k ndio taasisi inavyokuwa si kuogopa fulani akiondoka chama kitakufa.
 
Kumalizika kwa maandamano hayo kwa amani kuna jibu moja tu kuhusu Arusha,......

Kuna mtu mkubwa serikalini alitoa amri ya kunyunyizia binadamu risasi,awajibishwe
 
REGIA,

Mimi nadhani uongee na akina Mnyika/Halima/Slaa/Mbowe/Kiwelu/Wenje n.k kuhusu Jambo lifuatalo:

Siamini kuwa Chadema kama chama hakina idara ya mawasiliano ya jamii. Hivi inakuwaje watu wanaomba picha kutoka katika mikutano yenu? Ninyi mnapaswa kuleta picha na si watu waombe.

Hii ilikuwa kazi ya idara ya mass communication and mobilization. Msafara wa viongozi wa juu Chadema hauna mpiga picha!! Nina hakika kama mngetangaza nafasi ya mtu kujitolea katika umati tunaouona wangejitolea watu zaidi 100. Hata kwa malipo mgempatia kijana transport na pesa za kumwezesha isingefikia mahali watu wategemee picha za simu.

Ushauri: kila mkoa uwe na mpiga picha rasmi wa Chama, awe tayari kwa mambo kama haya, chama kimuwezeshe! Please Chadema deserves better than this!
 
Asante mkuu Nguruvi3 kabla sijasoma huu ujumbe wako kwa Regia nilikuwa nataka nimwandikie Regia atuwakilishe ili uanzishwe hata mfuko kwa ajili ya kupata mawasiliano hasa picha wakati wa mikutano ya chama chetu.

Basi ujumbe mkuu umeutoa, nadhani wengi wetu tungeunga mkono suala hilo. Huo mfuko usihusishwe na maswala mengine ya chama kwanza. Lile suala la kuchangina Chadema kama chama liendelee kivyake.

Ikiwa mfuko utakuwa na akiba ya kutosha wanaweza kupanua wigo wa matumizi. Nipo tayari kuuchangia mfuko ukianziswa. Naoma Mheshimiwa Regia, na wengine ndani ya viongozi wa Chadema wauanzishe, tutauchangia mara.
 
Sikubaliani wewe mkuu, mi nadhani Chama kiongozwe na 'policy''. Chadema wakianza kumuogopa mtu ndio mwanzo wa matatizo. Angalia CCM sasa hivi wanamatatizo makubwa sababu tu wanamuogopa Chenge/RA/EL.

Hapa simaanishi kuwa wamfukuze tu Shibuda, hapana nina maana wafuate taratibu hadi itakapofika wakati wa kumfukuza.

Kuhusu Kafulila mimi nadhani uamuzi wa kumfukuza ulikuwa sahihi kabisa. Huwezi kuwa na watu wawili watatu wanaotaka kuvuruga chama kwa masilahi yao binafsi. Alipoondoka Chadema akasema ni chama cha ukoo na ukabila, lakini ni huyo huyo alikua kiongozi CDM masaa 24 kabla hajaondoka. Angalia Kafulila ndiye ameungana na CCM kuyumbisha kanuni za bunge in favor of CCM ili apate uwaziri kivuli.

Ni kutokana na vurugu za akina Kafulila na Hamad Rashid Makinda akapata mwanya wa kuchagua akina Lowasa na January huku wapinzani wakipigana wao kwa wao. The bottomline ni upuuzi wa Kafulila na hisia za kulipa kisasi. Uzembe huu wa Kafulila unadhihiirisha maamuzi sahihi ya CDM.

Maelezo yangu hapo juu ni mifano ya viongozi wanaodhani wao ni Chama. Chama kijengwe kama taasisi na si watu. Alikuwepo Mtei, akaja Bob Makani, sasa Mbowe na atakuja mwingine n.k ndio taasisi inavyokuwa si kuogopa fulani akiondoka chama kitakufa.

Nashauri Shibuda apuuzwe, alimradi wananchi wa Maswa wanapata haki yao, kwa vile ndiyo waliompa kura. Kumfukuza sasa haitaleta manufaa makubwa kuliko kumpuuza, atengwe kiaina. Binafsi nilimwona msaliti mara baada ya uchaguzi, shida yake ilikuwa ubunge wa Maswa, sawa kaupata lakini mtazamo amerudi CCM, Apuuzwe, atengwe, wananchi wa maswa wataona wenyewe, 2015 awekwe mgombea mwingine kupitia Chadema.

Nadhani wasaliti sio Shibuda tu, wapo wengine pia, tufungue macho.
 
Shibuda wala asifukuzwe alimradi kaisaidia CDM kuongeza ruzuku na wabunge wa viti maalum keshamaliza kazi yake.
 
Chadema wako juu wanakubalika pande nyingi za tanzania ukiacha maeneo ya kusini ambako sasa wameanza kuwaamsha watu huko kutoka usingizini.
 
Wakuu Salaam!!!

Yale maandamano ya Kanda ya Ziwa leo yanahamia Mkoa wa Mara baada ya jana kuingia Geita, Sengerema, Misungwi, Kwimba na Ukerewe. Maandamano yatakuwa Musoma kuanzia Viwanja vya Bweri mpaka Uwanja Mkendo Musoma Mjini. Msafara wa Vikosi toka Mwanza mjini unatarajiwa kupokelewa na Mbunge wa Musoma Mijini Vincent Nyerere.

Dalili zinaonesha kuwa na leo CHADEMA itaiteka Musoma kwa jinsi ambavyo watu wamejipanga na kujiandaa kwa hamu maandamano haya. Maandamano yanatarajiwa kuanza saa 7 mchana.

Aluta Continua.

Kutoka Kitangiri Mwanza
Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Thank you for keeping us informed. We wish you the best! This time 'lazima kieleweke'.
 
REGIA,
Mimi nadhani uongee na akina Mnyika/Halima/Slaa/Mbowe/Kiwelu/Wenje n.k kuhusu Jambo lifuatalo.
Siamini kuwa Chadema kama chama hakina idara ya mawasiliano ya jamii. Hivi inakuwaje watu wanaomba picha kutoka katika mikutano yenu? Ninyi mnapaswa kuleta picha na si watu waombe.
Hii ilikuwa kazi ya idara ya mass communication and mobilization. Msafara wa viongozi wa juu Chadema hauna mpiga picha!! Nina hakika kama mngetangaza nafasi ya mtu kujitolea katika umati tunaouona wangejitolea watu zaidi 100. Hata kwa malipo mgempatia kijana transport na pesa za kumwezesha isingefikia mahali watu wategemee picha za simu.

Ushauri: kila mkoa uwe na mpiga picha rasmi wa Chama, awe tayari kwa mambo kama haya, chama kimuwezeshe! Please Chadema deserves better than this!

Good idea!
 
Kumalizika kwa maandamano hayo kwa amani kuna jibu moja tu kuhusu Arusha,......

Kuna mtu mkubwa serikalini alitoa amri ya kunyunyizia binadamu risasi,awajibishwe
Some truth here!...

Huyo mtu alikuwa anamtumikia nani?
 
Ninadhani ikiwezekana SHIBUDA akalishwe na kamati ya maadli aeleze mwelekeo wake. Unaweza ukaacha kumbe unaacha uozo akija kulipuka chama kinakuwa kama yale yaliyomkuta LYATONGA NCCR MAGEUZI. Mimi ninadhani upinzani unatoka roho sio wa kinafiki. CCM wanatafuta njia ya kuingia iliwaanza kukisambaratisha CHADEMA. Mkiona shibuda haelekei msisite kuchukua hatua za haraka.
 
Kamanda mwema vipi, hukupata taarifa zozote za kiintelijensia safari hii, naona vijana wanachanja mbuga tu
 
Kamanda mwema vipi, hukupata taarifa zozote za kiintelijensia safari hii, naona vijana wanachanja mbuga tu
Anasubilia wafike Arusha ndiyo taarifa za kiintelijensia zitatolewa....
 
Hatutaacha maandamano mpaka kieleweke , tumenyonywa vya kutosha na viongozi, watu wamejifanya miungu
ipo siku itakuwa kweli , tunahitaji mabadiliko ya kweli.
 
tumechoshwa na ufisadi kila kitu wanachakachua, inabidi serikari ya ccm ijipange upya , zaidi yatawafika ya TUNISIA NA MISRI
 
JK unaona mambo hayo? Unachekwa tu hivi sasa, Magogoni patakuwa hapatoshi bora ufanye kitu cha maana na kuanza kufungasha virago.
 
SErikali ya ccm inanyanganya wananchi mashamba yao , angalia mza MKURUGENZI anajigawia viwanja pamoja na maswaiba wake , kilicho baki ni kuuana tu, mtu ameishi eneo hilo tangu 1930, mwaka 2009 uje umwambie hatakiwi kuishi hapo aende wapi na eneo hamjampa , kwa hali hii viongozi mamuluki muwe macho mtakufa sana
 
Nawaomba wana jamvi, watakapo ingia wale ndugu zetu wa mlengo wa kushoto tusipoteze muda kujibisha nao...Asanteni

Safi sana!! Ignoring them is the best way to expose their foolishness!!!
 
Back
Top Bottom