Physics ya A- Level inanitesa

Physics ya A- Level inanitesa

Nakumbuka kuna kitabu flani cha physics wakati tupo a level tulikuwa tunakiita 'kijiji'..kina rangi ya njano.. Kilikuwa kina nondo za kufa mtu.. Ila maswali yake sasa.. unaweza ukatumia siku nzima kusolve swali moja..afu na bado ukakosa.. Uskate tamaa kijana.. Sku hizi kuna learning materials nyingi sana..
 
Tunatofautiana, binafsi projectile mm niliiona afadhar ukilinganisha na mzik wa electronics, electromgnetism na wave, ninacho kushaur dg, km bd mpk sasa haijakukaa kichwan vzr, physics isikupotezee mda sana, Cha msing n kuisoma kuepuka F au E, upate angalau D, halaf nguvu nying peleka kweny C & B.
Physics Ktk elimu yang ya A Level ilichukua zaid ya 75% lkn mwisho wa siku nilitambaa na liji karai sawa na Bios na Chemistry, kwa ufaulu wa mwaka wetu ndoto za MD zilikatka hapo, ila wenzangu waliopigwa na machare mapema waliipotezea P, wakalala mbele na C & B mwisho wa siku wakatoka na A zao Mbili na E au D za physics Now wako zao MD. Na km ulichagua sayansi piga shule dogo, mm tangu nilipoanza kusoma sayansi mpk leo hii chuo mwaka wa nne sijawah kunenepa nipo km antena, na ukiniona n km kuna nati zime loose kichwan, mpk kuna kpn nilijuta. Unasubiliwa na pepa 11 kweny necta kaa ukijua hilo.
 
Mechanics visub-topic vyake vyote vinazingua hivyo hivyo. Komaa tu hamna namna. Upande wangu Physics ya Advance sitaki hata kuisikia, ilinitesa sana ingawa nilikuwa naiweza lakini mwisho ilinitenda sivyo.
 
Physics ya advance haitaki mihemko, unaweza maliza kusoma subtopic na ukafanya maswali 15 yote ukakosa, lakini kama uko makini, kila swali unalokosa lazima utambue wapi ulikosea, eventually mambo huenda sawa, usikate tamaa, kwa ufupi projectile motion ndio mteremko, vilima vinakuja
 
Dogo,
Watu watakwambia hiyo subtopic ni rahisi, But trust me Mechanics inahitaji Nguvu ya Ziada. Hiyo kitu hata Mimi ilinisumbua mwanzoni.. Badae nikaipatia.
Tafuta aliyeielewa akupumzikie hiyo utaiona rahisi tu..
Labda nikutoe wasiwasi
Hiyo projectile ina kaswali ka marks 5-10 kwenye paper 1,
Na huenda lisiwepo pia,
Kuwa focused,
Kuna topics rahisi (RAHISI MNO) form six kama Modern Physics, Umeme, Wave, Heat, Electronics ambazo ukizimaster Vizuri zitakupa 60% na hiyo mechanics ikakupa hata 20% basi ushatoboa.
Mechanics ni Pana sana na hupoteza Muda kwa wengi.
Nakushauri, unatakiwa kufauru pepa ya Form six, No matter what.
Hivyo basi Kuanzia LEO somea NECTA,
ikitokea unapata namba za Viatu kwenye pepa za Ndani hilo lisikukatishe Tamaa, ni Kawaida kwa hizi kombi zetu.
Narudia, Somea NECTA kuanzia leo, ndio elimu yetu ilivyo.

Mimi nlitoka NECTA na mitihani ya ndani sikuwahi pata 50%
Nlikuja kuwaacha midomo wazi raia kwenye Mock.
Dogo Chapa kazi.

Lastly, Discussions ni kila kitu. Chagua marafiki mnaofanana malengo,
Sisi tulikuwa na group la mtu tano,,tulikuwa tunafanya discussion kila siku kuanzia saa tisa usiku hadi saa moja Asubuhi, na wote tulitoboa.(wote kwa ufaulu wa One na two)
 
Ivii dogo ukikojoa mkojo huwa unandoka kaumbali fulani eti ukiwa umesimama??

Tafuta initial velocity na trajectory yake.

Phyz ni Tamu sana dogo, komaa utatoka.

Mie tcha aliwahi kunipanikisha nilipoanza form 5, alinifundisha projectile motion na measurement zikaisha kwa dk 40 sikuamini lakini sikukata tamaa nilifanya maamuzi ya kukomaa na nilifaulu. Nikabahatika kuchomoka na Div I yangu nzuri ya PCB
 
Umesoma kweli phys ya advance ww?

Phys ya advance unapoanza lazima uchezee 30,30 za kutosha halafu huko mbeleni ndo utaanza kupata A kama utajibidiisha maana topics za mbele ni nyepesi sana

Halafu kingine phys usiposoma kama ndo umeingia form five ukifundishwa kitu halafu usipitie ukija kusoma tena utaona as if mambo ni mapya kabisa na hujawahi kukutana nayo .
Mkuu advance nimesoma PCB so physics naielewa vizuri...mathematics na physics ni formula tu na derivations zake...ukielewa hivyo haikusumbui hata kidogo
 
Basi inaonekana ulikuwa mbovu sana kwenye phys

Yani hata electrostatic ilikuwa inakushinda??

Aisee ,am sorry to say but ulivamia kombi

Hizo wave,electrostatic na heat ni topics nyanya sana

At least hiyo electromagnetism ingawaje nayo ni nyepesi sana ila ina formula nyingi sana.
Sawa engineer
 
yaan mkuu hiyo topic ndiyo rahisi kupita maelezo.. sema wewe unameza hauelewi ndo maana inakushinda..!!!!

projectile bila kuchora hupati swali lake..!
 
Dogo,
Watu watakwambia hiyo subtopic ni rahisi, But trust me Mechanics inahitaji Nguvu ya Ziada. Hiyo kitu hata Mimi ilinisumbua mwanzoni.. Badae nikaipatia.
Tafuta aliyeielewa akupumzikie hiyo utaiona rahisi tu..
Labda nikutoe wasiwasi
Hiyo projectile ina kaswali ka marks 5-10 kwenye paper 1,
Na huenda lisiwepo pia,
Kuwa focused,
Kuna topics rahisi (RAHISI MNO) form six kama Modern Physics, Umeme, Wave, Heat, Electronics ambazo ukizimaster Vizuri zitakupa 60% na hiyo mechanics ikakupa hata 20% basi ushatoboa.
Mechanics ni Pana sana na hupoteza Muda kwa wengi.
Nakushauri, unatakiwa kufauru pepa ya Form six, No matter what.
Hivyo basi Kuanzia LEO somea NECTA,
ikitokea unapata namba za Viatu kwenye pepa za Ndani hilo lisikukatishe Tamaa, ni Kawaida kwa hizi kombi zetu.
Narudia, Somea NECTA kuanzia leo, ndio elimu yetu ilivyo.

Mimi nlitoka NECTA na mitihani ya ndani sikuwahi pata 50%
Nlikuja kuwaacha midomo wazi raia kwenye Mock.
Dogo Chapa kazi.

Lastly, Discussions ni kila kitu. Chagua marafiki mnaofanana malengo,
Sisi tulikuwa na group la mtu tano,,tulikuwa tunafanya discussion kila siku kuanzia saa tisa usiku hadi saa moja Asubuhi, na wote tulitoboa.(wote kwa ufaulu wa One na two)
Phys unapoanza form five lazima ikutese sana huo ndio ukweli

Mechanics inasumbua sana hasa umkute mwalimu anayejua kukunja pepa

Lakini huko mbeleni phys inakuwa nyanya sana kiasi kwamba kuchomoka na A ni jambo la kawaida sana
 
Physics ya advance haitaki mihemko, unaweza maliza kusoma subtopic na ukafanya maswali 15 yote ukakosa, lakini kama uko makini, kila swali unalokosa lazima utambue wapi ulikosea, eventually mambo huenda sawa, usikate tamaa, kwa ufupi projectile motion ndio mteremko, vilima vinakuja
Phys unapokutana na swali kwa mara probability ya kulipata hilo swali ni ndogo sana
 
Sio kila kitu utakiweza kwenye maisha ya kujifunza...mfano mimi nilipomaliza mtihani wa tahosa nikalala mbele kisa ilikuwa Organic tu kwenye chemistry...lakini leo hii Fundi viatu maridadi sana hapa mitaa ya Posta.
 
Acha uvivu ingia mtandaoni kuna pdf notes nyingi tu za projectile
 
Habari wanajamvi ??

Wanajamvi mimi ni mwanafunzi niliyemaliza kidato cha nne mwaka jana(2016), ufaulu wangu katika masomo ya sayansi ni mzuri hivyo nina mipango ya kwenda Advanced level comb PCB au PCM

Lakini tangu nilipo anza kusoma physics yaani nakata tamaa maana kuna ki subtopic kinaitwa PROJECTILE MOTION yaana kila nikifanya swali lake nakosa. Please wanajamvi naombeni ushauri wenu katika somo hili.

Maana kubadilisha comb siwez sababu nilisoma TECHNICAL SCHOOL hivyo siwez soma comb za art wala CBG.

Dogo marisasi na madubwana mengine yanayochanja mbuga principles zake zipo kwenye hiyo topic kaza buti
 
Mkuu maswal yanayonisumbua sana ni ya kuprove
hata kuprove lazima uchore kwanza ndo yanakuwa mteremko... yaan kufanya bila kuchora ujue unajua sana.. ila kwa anayeelewa lazima aanze kwa kuchora..!
 
Back
Top Bottom