singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,452
- 8,104
Habarini wanajamvi wa Jf
Natumaini wote wazima na ni wenye furaha, sitaki kuongea mengi Zaidi na kama uzi unavyojieleza na mimi leo nimeamua kuleta kwenu kisa changu hiki ambacho naamini kwa namna moja ama nyingine kinaweza kuwa na msaada mkubwa kwa baadhi ya watu, lakini pia huenda ushauri wenu hapa ukasaidia baadhi ya watu ambao huenda wanapitia hali kama niliopitia mimi.
Nitatumia muda wangu kuandika kisa hiki mpaka kiishe majina yote nitakayotumia sio ya ya kweli na nitasimulia mpaka mwisho kadri akili yangu itakavyoweza kuniruhusu kuendelea kuandika.
NB :Hii sio chai bali ni maji ya uhai.
Mwaka 2014 ndio mwaka ambao nilimaliza kidato cha nne ndani ya shule moja ya serikali inayopatikana mkoani Tanga Wilaya ya Lushoto..
Baada ya kufanya mtihani wa kidato cha nne na kumaliza salama nilikuwa nikijiamini sana kwamba nitafaulu na kwenda kidato cha tano , moja ya sababu ilionifanya nijiamini ni kutokana na kuwa na matokeo mazuri tokea nikiwa kidato cha kwanza , lakini pia namna mtihani nilivyoufanya.
Basi baada ya kukaa nyumbani miezi kadhaa hatimae matokeo yalitoka na kama nilivyotegemea niliweza kufaulu kwa ufaulu wa ‘Dinstiction’ Gpa ya 4.1 first class, kwa wale ambao mnakumbuka mwaka wetu wa 2014 matokeo yalikuwa yakipangwa kwa mfumo wa GPA.
Ilikuwa ni furaha kwangu kufaulu kwenda kidato cha tano na kwa wakati huu niliona ndoto zangu za kuwa Daktari zinakwenda kutimia.
Wakati wote wa masomo ya O-level nilikuwa nikiishi kwa Shangazi yangu aliekuwa akiishi Lushoto mjini kwani shule niliokuwa nikisomea ilikuwa ya Day na hata nilipomaliza kidato cha nne nilibakia hapo hapo kwa shangazi mpaka matokeo yalivyotoka , basi nilipongezwa hapa na pale na Baba shangazi na Shangazi mwenyewe kwa kufaulu , huku ndugu kutoka kijijini akiwemo mama yangu pia walinipongeza kwa kufaulu , Mzee alitutoka miaka kadhaa nyuma nikiwa Darasala nne hivyo nilikuwa na mzazi mmoja tu.
Basi baada ya miezi michache kupita hatimae selection zilitoka na nikachaguliwa kwenda shule moja iliokuwa ikiitwa Kantalamba , kusema ukweli sikujua kwanini nilichaguliwa hii shule kwani sikua nimeichagua , kombi niliochaguliwa ilikuwa ni PCM , shule ilikuwa huko Sumbawanga mkoa wa Rukwa .
Ndugu zangu akiwemo Shangazi Mkubwa Anaesimamia Mirathi yetu baada ya kuona nimetupwa mbali huko waligoma mimi kwenda shule hio kwani kulikuwa ni mbali sana , Baba Shangazi yeye alikuwa anakomalia niende huko huko, huku akifanya mpango wa kunihamishia shule za karibu, Baba shangazi yangu yeye alikuwa mwalimu mkuu wa shule flani hapo hapo Lushoto mjini na alikuwa na koneksheni ndio maana alitaka niende huko huko Kantalamba , lakini shangazi zangu wao walikomaa wakasema ni mbali na isitoshe kombi sio niliokuwa nikiitaka maana nilikuwa nnikitaka PCB.
Basi baada ya mazungumzo ya ndugu kuisha hatimae maamuzi yakawa niende Dar kwa baba mdogo yeye atanitafutia shule ya Private ,Ada haikuwa tatizo kutokana na kwamba mzee alikuwa mwalimu na mirathi yake ilitoka kipindi nikianza form one kwa hio pesa ilikuwepo .
Baba mdogo aliweza kupata shule kabla hata ya mimi kuanza safari ya kwenda Dar, shule aliopata ilikuwa ni ya jeshi maeneo flani hivi ya Mwenge
Nilipitia changamoto kubwa sana nikiwa ndani ya hii shule na hapa ndipo misukosuko ya kukatisha tamaa ilipoanzia ….. Inaendelea Baada ya dakika tano
Bonyeza kiungo kusoma kipande kinachofata
Sehemu ya Pili
Sehemu ya tatu
Sehemu ya nne
Sehemu ya tano
Sehemu ya sita
Sehemu ya saba
Natumaini wote wazima na ni wenye furaha, sitaki kuongea mengi Zaidi na kama uzi unavyojieleza na mimi leo nimeamua kuleta kwenu kisa changu hiki ambacho naamini kwa namna moja ama nyingine kinaweza kuwa na msaada mkubwa kwa baadhi ya watu, lakini pia huenda ushauri wenu hapa ukasaidia baadhi ya watu ambao huenda wanapitia hali kama niliopitia mimi.
Nitatumia muda wangu kuandika kisa hiki mpaka kiishe majina yote nitakayotumia sio ya ya kweli na nitasimulia mpaka mwisho kadri akili yangu itakavyoweza kuniruhusu kuendelea kuandika.
NB :Hii sio chai bali ni maji ya uhai.
Mwaka 2014 ndio mwaka ambao nilimaliza kidato cha nne ndani ya shule moja ya serikali inayopatikana mkoani Tanga Wilaya ya Lushoto..
Baada ya kufanya mtihani wa kidato cha nne na kumaliza salama nilikuwa nikijiamini sana kwamba nitafaulu na kwenda kidato cha tano , moja ya sababu ilionifanya nijiamini ni kutokana na kuwa na matokeo mazuri tokea nikiwa kidato cha kwanza , lakini pia namna mtihani nilivyoufanya.
Basi baada ya kukaa nyumbani miezi kadhaa hatimae matokeo yalitoka na kama nilivyotegemea niliweza kufaulu kwa ufaulu wa ‘Dinstiction’ Gpa ya 4.1 first class, kwa wale ambao mnakumbuka mwaka wetu wa 2014 matokeo yalikuwa yakipangwa kwa mfumo wa GPA.
Ilikuwa ni furaha kwangu kufaulu kwenda kidato cha tano na kwa wakati huu niliona ndoto zangu za kuwa Daktari zinakwenda kutimia.
Wakati wote wa masomo ya O-level nilikuwa nikiishi kwa Shangazi yangu aliekuwa akiishi Lushoto mjini kwani shule niliokuwa nikisomea ilikuwa ya Day na hata nilipomaliza kidato cha nne nilibakia hapo hapo kwa shangazi mpaka matokeo yalivyotoka , basi nilipongezwa hapa na pale na Baba shangazi na Shangazi mwenyewe kwa kufaulu , huku ndugu kutoka kijijini akiwemo mama yangu pia walinipongeza kwa kufaulu , Mzee alitutoka miaka kadhaa nyuma nikiwa Darasala nne hivyo nilikuwa na mzazi mmoja tu.
Basi baada ya miezi michache kupita hatimae selection zilitoka na nikachaguliwa kwenda shule moja iliokuwa ikiitwa Kantalamba , kusema ukweli sikujua kwanini nilichaguliwa hii shule kwani sikua nimeichagua , kombi niliochaguliwa ilikuwa ni PCM , shule ilikuwa huko Sumbawanga mkoa wa Rukwa .
Ndugu zangu akiwemo Shangazi Mkubwa Anaesimamia Mirathi yetu baada ya kuona nimetupwa mbali huko waligoma mimi kwenda shule hio kwani kulikuwa ni mbali sana , Baba Shangazi yeye alikuwa anakomalia niende huko huko, huku akifanya mpango wa kunihamishia shule za karibu, Baba shangazi yangu yeye alikuwa mwalimu mkuu wa shule flani hapo hapo Lushoto mjini na alikuwa na koneksheni ndio maana alitaka niende huko huko Kantalamba , lakini shangazi zangu wao walikomaa wakasema ni mbali na isitoshe kombi sio niliokuwa nikiitaka maana nilikuwa nnikitaka PCB.
Basi baada ya mazungumzo ya ndugu kuisha hatimae maamuzi yakawa niende Dar kwa baba mdogo yeye atanitafutia shule ya Private ,Ada haikuwa tatizo kutokana na kwamba mzee alikuwa mwalimu na mirathi yake ilitoka kipindi nikianza form one kwa hio pesa ilikuwepo .
Baba mdogo aliweza kupata shule kabla hata ya mimi kuanza safari ya kwenda Dar, shule aliopata ilikuwa ni ya jeshi maeneo flani hivi ya Mwenge
Nilipitia changamoto kubwa sana nikiwa ndani ya hii shule na hapa ndipo misukosuko ya kukatisha tamaa ilipoanzia ….. Inaendelea Baada ya dakika tano
Bonyeza kiungo kusoma kipande kinachofata
Sehemu ya Pili
Sehemu ya tatu
Sehemu ya nne
Sehemu ya tano
Sehemu ya sita
Sehemu ya saba