Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,112
Ni makosa kumfananisha Mangula na Dr.Slaa kwani kwa kuangalia CHADEMA kilikuwaje na kikoje hivi sasa, ndipo utapata jibu la ni nani anaweza kuwa juu ya mwenzie.Ni hoja dhaifu kusema Mangula ameongoza watu 6mln wakati tunajua Watanzania ni zaidi ya hao.Kiongozi mzuri ni yule anayewaongoza hata neutral members na kuwavutia upande wake kitu ambacho kimeonekana kwa Dr.Slaa. Kwa upande mwingine tunapima"leadership supporting hand", kwa upande wa Mangula alikuwa na wakuu wa mikoa na wilaya ambao ni wajumbe wa kamati za siasa wakati Dr.Slaa anategemea wabunge na sehemu ambako hakuna wabunge hutumia juhudi binafsi kuwashawishi watu na kuonesha uhai wa chama. Sababu nyingine ni UCHUMI WA VYAMA: Mangula ameongoza ccm chenye vyanzo vingi vya mapato kama vile majengo na viwanja vya michezo kama Kirumba na ruzuku kubwa hivyo kuwa na mazingira mazuri ya kuwalipa viongozi wa ngazi za chini ili kuwatia hamasa ya kuimarisha chama pamoja na kumudu gharama za uenezi, Lakini Dr.Slaa amefanikiwa bila fedha!