BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1696395177327.png

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), iimetangaza bei kikomo za bidhaa za Mafuta zilizoanza kutumika leo Oktoba 4, 2023 ambapo kwa Dar es Salaam Petroli ni Tsh. 3,281, Dizeli 3,448 na Mafuta ya Taa Tsh. 2,943 ikiwa na ongezeko la Tsh. 68 kwa kila Lita.

Tanga, Petroli ni Tsh. 3,327, Dizeli 3,494, Mafuta ya Taa Tsh. 2,989 na Mtwara, Petroli itauzwa Tsh. 3,353, Dizeli Tsh. 3,520 na Mafuta ya Taa Tsh. 3,016 ambapo EWURA imesema ongezeko hilo linatokana na kupanda kwa 4.21% ya Gharama za Mafuta katika Soko la Dunia.

Aidha, EWURA imesema gharama za uagizaji Mafuta zimepanda hadi kufikia 17% kwa Petroli, 62% kwa Dizeli na 4% kwa Mafuta ya Taa. Pia, Bei za Mafuta zimeathiriwa na uamuzi wa wazalishaji wakubwa wa Mafuta duniani (OPEC+) waliopunguza uzalishaji pamoja na vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa dhidi ya
Urusi.

========
1696395213226.png
 
View attachment 2771211
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), iimetangaza bei kikomo za bidhaa za Mafuta zilizoanza kutumika leo Oktoba 4, 2023 ambapo kwa Dar es Salaam Petroli ni Tsh. 3,281, Dizeli 3,448 na Mafuta ya Taa Tsh. 2,943 ikiwa na ongezeko la Tsh. 68 kwa kila Lita.

Tanga, Petroli ni Tsh. 3,327, Dizeli 3,494, Mafuta ya Taa Tsh. 2,989 na Mtwara, Petroli itauzwa Tsh. 3,353, Dizeli Tsh. 3,520 na Mafuta ya Taa Tsh. 3,016 ambapo EWURA imesema ongezeko hilo linatokana na kupanda kwa 4.21% ya Gharama za Mafuta katika Soko la Dunia.

Aidha, EWURA imesema gharama za uagizaji Mafuta zimepanda hadi kufikia 17% kwa Petroli, 62% kwa Dizeli na 4% kwa Mafuta ya Taa. Pia, Bei za Mafuta zimeathiriwa na uamuzi wa wazalishaji wakubwa wa Mafuta duniani (OPEC+) waliopunguza uzalishaji pamoja na vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa dhidi ya
Urusi.

========
View attachment 2771212
ewura ni matapeli
 
Hapo ruzuku ya 100 bilioni inatolewa kila mwezi. Tunaipongeza Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama
Wapunguze zile kodi ipo 26% kwenye mafuta hiyo ruzuku hata wasipotoa wakatoa baadhi ya kodi kichefuchefu za mafuta life itaenda sawa...
 
Tutafute wawekezaji vya vyeo vya juu kitaifa. Wenye maono. Na definition sahihi ya Kiongozi
 
na bado mtatema bungo,na mamayao yuko kwa wawekezaji kule anaangalia maonesho ya mboga mboga sijui takataka gani, yaani Mungu atuhurumie wadanganyika.
 
Back
Top Bottom