Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo -Bara, amesema kwamba Chama hicho leo Mei 20, 2025 wanampokea Wakili Peter Madeleka kuwa mwanachama rasmi wa Chama hicho.
View attachment 3339842
View: https://www.youtube.com/live/ltZztd-LMP8?si=QPvqxVrzfZz-1DZC
View attachment 3339848
Madelaka: Amesema kwamba amejiunga na Chama hicho ili kuimalisha nguvu ya upinzani nchini.
Amesema kwamba kumekuwepo na changamoto pale inapotokea nchini kuna Chama cha upinzani kimoja chenye nguvu kikayimbishwa.
Akiulizwa swali na Mwandishi wa Habari: Kwamba kumekuwepo na madai kwamba anatumika kutokana na kuwai kuwa mtumishi wa umma kwenye nafasi ya Jeshi la Polisi, amejibu kwa kusema kwamba wanaosema hivyo ni wavivu wa kufikiri.
Ameongeza kwamba yeye siyo mtumishi wa kwanza kutoka kwenye vyombo vya usalama kuingia kwenye siasa mara baada ya kuacha utumishi.
Amesema ipo mifano mbalimbali ya watu kwenye vyama vya siasa ikiwemo CCM ambao wamepata nafasi za uongozi mara baada ya kuacha utumivishi wao kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.
Akijibu swali kwamba alikuwa Chama gani awali kabla ya kujiunga na ACT Wazalendo, amesema alikuwa kwenye Chama cha Chadema.
Amesema kwenye Jimbo ambalo yeye anatarajia kugombea hakuna Afisa yoyote wa Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) ambaye ataweza kupoka ushindi ambao ataupata, amesisitiza kwa kusema kwamba Mtu wa aina hiyo hayupo.
Kuhusu msimamo wake juu ya 'No reform No Election'
Amesema kwamba lengo la Chama chochote ni kushika madaraka, ambapo amesema kwamba akiwa na Chama cha ACT Wazalendo watatumia fursa hiyo kuonesha umma kuhusu uhalisia wa mabadiliko ambayo anadai kwamba CCM wamekuwa wanasema yamefanyika pamoja na kauli za kuaminisha umma kuwa uchaguzi utakuwa huru na haki.